< Amosi 6 >
1 Ole wao wanaostarehe katika Sayuni, na kwa wale ambao wameokoka katika nchi ya mlima wa Samaria, watu mashuhuri bora wa mataifa, ambao nyumba ya Israeli huja kwa ajili ya msaada!
Woe to! the [people] at ease in Zion and those [who] trust in [the] mountain of Samaria [the] distinguished [people] of [the] first of the nations and they will come to them [the] house of Israel.
2 Viongozi wenu husema, “Pita kwenda Kalne na mkatazame; kutoka huko nendeni hadi Hamathi, mji mkubwa; kisha nendeni chini hata Gathi ya Wapelestina. Je ni wabora kuliko falme zenu mbili? Je kuna mpaka mkubwa kuliko mpaka wenu?”
Pass over Calneh and see and go from there Hamath-Rabbah and go down Gath of [the] Philistines ¿ [are they] good more than the kingdoms these or? great [is] territory their more than territory your.
3 Ole wao wale waiwekao siku ya majanga na kufanya ufalme kuwa kinyume kusogea karibu.
Those [who] push away a day evil and you have brought near! a seat of violence.
4 Wamelala juu ya vitanda vya pembe na kupumzika juu ya viti vyao. Wakala wana kondoo kutoka kwenye kundi na ndama kutoka kwenye zizi.
Those [who] lie on beds of ivory and [people] sprawled out on couches their and [those who] eat lambs from [the] flock and calves from [the] midst of [the] stall.
5 Wanaimba nyimbo za kijinga kwenye muziki wa kinubi; wanatunga kwenye vyombo kama vya Daudi.
Those [who] improvise on [the] mouth of the lyre like David they have devised for themselves instruments of song.
6 Wanakunywa mvinyo kutoka kwenye bakuli na kujipaka mafuta wenyewe kwa mafuta ya marahamu, lakini hawahuzuniki juu ya mateso ya Yusufu.
Those [who] drink in bowls of wine and [the] best of oils they smear and not they were sickened on [the] ruin of (Joseph *L(abh)*)
7 Hivyo sasa watakwenda utumwani pamoja na watumwa wakwanza, na kelele za hao waliojinyoosha zitapita.
therefore now they will go into exile at [the] head of [those who] go into exile and it will come to an end [the] revelry of sprawled out [people].
8 “Mimi Bwana Yahwe, nimeapa kwa nafsi yangu -hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo, Mungu wa majeshi, naizira fahari ya Yakobo; nachukia boma zake. Kwa hiyo nitautoa huo mji pamoja vyote vilivyomo humo.”
He has sworn [the] Lord Yahweh by self his [the] utterance of Yahweh God of hosts [am] loathing I [the] pride of Jacob and fortresses his I hate and I will deliver up [the] city and what fills it.
9 Itakuja kuhusu kwamba kama kuna wanaume kumi waliobakia kwenye nyumba moja, watakufa.
And it will be if they will remain ten men in a house one and they will die.
10 Wakati ndugu wa mtu huyo atakapokuja kuchukua miili yao-yule ambaye awachomaye baada ya kuleta maiti katika nyumba-kama akisema kwa mtu katika nyumba, “Je kuna mtu yuko pamoja nawe?” Vipi kama yule akisema, “Hapana.” Kisha atasema, “Kaa kimya, kwa kuwa hatulitaja jina la Yahwe.”
And he will lift up him loved one his and [the one who] burns him to bring out bones from the house and he will say to [the one] who [is] in [the] innermost parts of the house ¿ still [is anyone] with you and he will say no and he will say hush! for not to bring to remembrance [the] name of Yahweh.
11 Tazama, Yahwe atatoa amri, na nyumba kubwa itapigwa kuwa vipande vipande, na nyumba ndogo kuwa na nyufa.
For here! Yahweh [is] commanding and someone will strike the house great fragments and the house small rubble.
12 Je farasi watakimbia juu ya mteremko wa miamba? Je mtu atalima huko na ng'ome? Bado mmegeuza haki kuwa sumu na tunda la haki kuwa uchungu.
¿ Do they run! on the crag[s] horses or? does anyone plow with oxen for you have turned into poison justice and [the] fruit of righteousness into wormwood.
13 Ninyi mnaofurahia juu ya Lo Debari, msemao, “Je hatukuchukua Karnaimu kwa nguvu zetu wenyewe?”
The joyful [people] to Lo Debar who say ¿ not by own strength our have we taken for ourselves Karnaim.
14 Lakini tazama, nitainua juu yenu taifa, nyumba ya Israeli-hivi ndivyo asemavyo Bwana Yahwe, Mungu wa majeshi. Watawatesa ninyi kutoka Lebo Hamathi hata kijito cha Araba.”
For here I [am] about to raise up on you O house of Israel [the] utterance of Yahweh [the] God of hosts a nation and they will oppress you from Lebo Hamath to [the] wadi of Arabah.