< Amosi 1 >

1 Haya ni mambo yanayoihusu Israeli ambayo Amosi, mmoja wa wachungaji katika Tekoa, aliyapokea katika ufunuo. Alipokea haya mambo katika siku za Uzia mfalme wa Yuda, na pia katika siku za Yeroboamu mwana wa Yoashi mfalme wa Israeli, miaka miwili kabla ya tetemeko la aridhi.
Paroles d’Amos, un des éleveurs de troupeaux à Tekoa, qui prophétisa sur Israël durant le règne d’Ouzia, roi de Juda, et de Jéroboam, roi d’Israël, deux ans avant le tremblement de terre.
2 Alisema, “Yahwe atanguruma kutoka Sayuni; atainua sauti yake kutoka Yerusalemu. Malisho ya wachungaji yatanyamaza kimya; kilele cha Karmeli kitanyauka.”
Il dit: "L’Eternel rugit de Sion, de Jérusalem il fait entendre sa voix: les pacages des bergers en sont assombris, le sommet du Carmel en est desséché."
3 Hivi ndivyo Yahwe asemavyo: “Kwa dhambi tatu za Damaskasi, hata kwa nne, sintobadilisha adhabu, kwa sababu wameipura Gileadi kwa vyombo vya chuma.
Ainsi parle l’Eternel: "A cause du triple, du quadruple crime de Damas, je ne le révoquerai pas, mon arrêt: parce qu’ils ont foulé le pays de Galaad avec des herses de fer.
4 Nitapeleka moto kwenye nyumba ya Hazaeli, na utaiteketeza ngome za Ben Hadadi.
Aussi déchaînerai-je le feu contre la maison de Hazaël, pour qu’il dévore les palais de Ben-Hadad.
5 Nitazivunja komeo za Damaskasi na kumkatilia mbali mtu ambaye aishiye katika Biqati Aveni, na pia yule mtu ashikaye fimbo ya kifalme katika Beth Edeni. Na watu wa shamu watakwenda utumwani hata Kiri,” asema Yahwe.
Je briserai les verrous de Damas, j’exterminerai les habitants du Val de Perversité et le porte-sceptre de la maison de Délices. Le peuple d’Aram ira en exil à Kir, dit l’Eternel."
6 Hivi ndivyo Yahwe asemavyo: “Kwa dhambi tatu za Gaza, hata nne, sintobadilisha adhabu, kwa sababu waliwachukua mateka watu wote, kuwaweka juu ya mkono wa Edomu.
Ainsi parle l’Eternel: "A cause du triple, du quadruple crime de Gaza, je ne le révoquerai pas, mon arrêt: parce qu’ils ont déporté des exilés en masse pour les livrer à Edom.
7 Nitatuma moto kwenye kuta za Gaza, na kuziteketeza ngome zake.
Aussi déchaînerai-je le feu contre les murs de Gaza, pour qu’il en dévore les palais.
8 Nitamkatilia mbali yule mtu aishiye katika Ashdodi na mtu ashikaye fimbo ya kifalme kutoka Ashkeloni. Nitaugeuza mkono wangu dhidi ya Ekroni, na mabaki ya Wafilisti wataangamia,” asema Bwana Yahwe.
J’Exterminerai les habitants d’Asdod et le porte-sceptre d’Ascalon; je dirigerai ma main contre Ekron, pour que périsse le reste des Philistins, dit le Seigneur Dieu."
9 Hivi ndivyo Yhawe asemavyo: “Kwa dhambi tatu za Tiro, hata kwa nne, sintobadili adhabu, kwa sababu waliwapelekea watu wote wa Edomu, na wamevunja agano lao la undugu.
Ainsi parle l’Eternel: "A cause du triple, du quadruple crime de Tyr, je ne le révoquerai pas, mon arrêt: parce qu’ils ont livré des captifs en masse à Edom, sans se souvenir de la fraternelle alliance.
10 Nitapeleka moto kwenye kuta za Tiro, nao utaziteketeza ngome zake.”
Aussi déchaînerai-je le feu contre les murs de Tyr, pour qu’il en dévore les palais."
11 Hivi ndivyo Yahwe asemavyo, “Kwa dhambi tatu za Edomu, hata kwa nne, sintobadilisha adhabu, kwa sababu alimfuatilia ndugu yake kwa upanga na kutupilia mbali huruma zote. Hasira yake ikaendelea kuwa kali, na ghadhabu yake ikabaki milele.
Ainsi parle l’Eternel: "A cause du triple, du quadruple crime d’Edom, je ne le révoquerai pas, mon arrêt: parce qu’il a poursuivi son frère avec l’épée, étouffant toute pitié; parce que sa colère ne cesse de faire des victimes, et qu’il se complaît dans une haine sans fin.
12 Nitapeleka moto juu ya Temani, na utaziteketeza nyumb a za kifalme za Bozra.”
Aussi déchaînerai-je le feu contre Têmân, pour qu’il dévore les palais de Boçra."
13 Hivi ndivyo Yahwe asemavyo, “Kwa dhambi tatu za watu wa Amoni, hata kwa nne, sintobadilisha adhabu, kwa sababu wamewapasua wanawake wa Gileadi wenye mimba, ili waweze kupanua mipaka yao.
Ainsi parle l’Eternel: "A cause du triple, du quadruple crime des fils d’Ammon, je ne le révoquerai pas, mon arrêt: parce qu’ils ont éventré les femmes enceintes de Galaad, en vue d’étendre leur territoire.
14 Nitawasha moto katika kuta za Raba, nao utaziteketeza nyumba za kifalme, pamoja na kupiga kelele katika siku ya vita, pamoja na dhoruba katika siku ya kimbunga.
Aussi mettrai-je le feu aux murs de Rabba, pour qu’il en dévore les palais, au milieu des cris de guerre, au jour du combat, au milieu de la tempête, au jour de l’ouragan.
15 Mfalme wao ataenda utumwani, yeye na maafisa wake pamoja,” asema Yahwe.
Malcom ira en exil, lui et ses dignitaires, tous ensemble, dit l’Eternel."

< Amosi 1 >