< Matendo 28 >

1 Tulipofikishwa salama, tulitambua kwamba kisiwa kinaitwa Malta.
Kui me olime tervelt maale pääsenud, saime teda, et saart hüütakse Maltaks.
2 Watu wenyeji wa pale si tu kwamba walitupa ukarimu wa kawaida, bali waliwasha moto na kutukaribisha sote, kwa sababu ya mvua na baridi iliyokuwa ikiendelea.
Saare elanikud osutasid meile ebatavalist lahkust. Nad süütasid lõkke ja võtsid meid selle äärde, sest sadas vihma ja oli külm.
3 Lakini Paulo alipokuwa amekusanya mzigo wa kuni na kuuweka motoni, nyoka mdogo mwenye sumu akatoka kwenye zile kuni kwa sababu ya lile joto, na akajizungusha kwenye mkono wake.
Paulus korjas hunniku hagu, ja kui ta selle tulle pani, tuli kuumusest välja rästik, kes ta kätte kinni hakkas.
4 Watu wenyeji wa pale walipoona mnyama ananing'inia kutoka kwenye mkono wake, wakasemezana wao kwa wao, “Mtu huyu hakika ni muuaji ambaye ametoroka baharini, lakini haki haimuruhusu kuishi.”
Kui saare elanikud nägid ussi tema käe küljes rippumas, ütlesid nad üksteisele: „See mees peab küll mõrtsukas olema! Õiguse jumalanna ei luba tal siin elada, kuigi ta on merest pääsenud.“
5 Lakini yeye akamtupia huyo mnyama katika moto na hakupata madhara yoyote.
Paulus aga viskas ussi tulle ja tal ei juhtunud mingit häda.
6 Wao walimngojea avimbe kwa homa au aanguke ghafla na kufa. Lakini baada ya kumwangalia kwa muda mrefu na kuona kwamba hakuna jambo ambalo si la kawaida kwake, walibadilisha mawazo yao na kusema alikuwa mungu.
Rahvas ootas, et ta paistetab üles või kukub surnult maha, aga kui nad nägid, et Paulusega ei juhtu midagi ebatavalist, mõtlesid nad ümber ja ütlesid, et ta on jumal.
7 Basi mahali pale karibu palikuwa na ardhi ambayo ilikuwa mali ya mkuu wa kisiwa, mtu aliyeitwa Pablio. Alitukaribisha na kutukarimu kwa siku tatu.
Selle paiga lähedal oli mõis, mis kuulus saare valitsejale Publiusele. Tema võttis meid vastu ja võõrustas meid heldelt kolm päeva.
8 Ilitokea kwamba baba wa Pablio alishikwa na homa na ugonjwa wa kuhara. Na Paulo alipomwendea, aliomba, akaweka mikono juu yake, na kumponya.
Publiuse isa lamas aga palaviku ja kõhutõvega voodis. Paulus läks tema juurde ja pani palvetades käed tema peale ning tegi ta terveks.
9 Baada ya hili kutokea, watu wengine pale kisiwani waliokuwa wanaumwa pia walikwenda na waliponywa.
Kui see oli sündinud, tulid sinna ka teised saarel olevad haiged, ja said terveks.
10 Watu wakatuheshimu kwa heshima nyingi. Tulipokuwa tunajiandaa kusafiri, walitupa vile tulivyovihitaji.
Ja nemad austasid meid mitmel viisil, ja kui me olime valmis merele minema, andsid nad meile teekonna jaoks kõik vajaliku.
11 Baada ya miezi mitatu, tulisafiri ndani ya meli ya Iskanda ambayo ilikuwa imepigwa baridi hapo kisiwani, ambayo viongozi wake walikuwa ndugu wawili mapacha.
Kolme kuu pärast me läksime sealt merele Aleksandria laevaga, mis oli saarel olnud ületalve ja mille tunnuseks oli Dioskuuride kuju.
12 Baada ya kuwa tumetua katika mji wa Sirakusa, tulikaa pale siku tatu.
Me randusime Sürakuusas ja jäime sinna kolmeks päevaks.
13 Kutokea pale tulisafiri tukafika katika mji wa Regio. Baada ya siku moja upepo wa kusini ulitokea ghafla, na baada ya siku mbili tukafika katika mji wa Putoli.
Sealt me sõitsime edasi ja saabusime Reegiumi. Ja kui järgmisel päeval tõusis lõunatuul, jõudsime teisel päeval Puteolisse.
14 Huko tuliwakuta baadhi ya ndugu na tulikaribishwa kukaa nao kwa siku saba. Kwa njia hii tukaja Rumi.
Sealt me leidsime vendi ja õdesid, kelle kutsel jäime nende juurde seitsmeks päevaks. Ja nii me tulime Rooma.
15 Kutoka huko wale ndugu, baada ya kuwa wamesikia habari zetu, walikuja kutupokea huko soko la Apias na Hotel tatu. Paulo alipowaona wale ndugu alimshukuru Mungu akajitia ujasiri.
Ja kui sealsed vennad ja õed meist kuulda said, tulid nad meile vastu Appiuse Foorumini ja Tres Tabernani. Neid inimesi nähes tänas Paulus Jumalat ning sai julgustust.
16 Tulipoingia Roma, Paulo aliruhusiwa kuishi peke yake pamoja na yule askari aliyekuwa akimlinda.
Kui me olime saabunud Rooma, lubati Paulusel omaette elada ühe sõduri valve all.
17 Basi ilikuwa baada ya siku tatu Paulo aliwaita pamoja wale wanume waliokuwa viongozi kati ya Wayahudi. Walipokuja pamoja, alisema kwao, “Ndugu, pamoja na kwamba sijafanya kosa lolote kwa watu hawa au kufanya kinyume na taratibu za mababa zetu waliotutangulia, nilitolewa kama mfungwa kutoka Yerusalemu hadi kwenye mikono ya Warumi.
Kolm päeva hiljem kutsus Paulus kokku juutide juhid. Kui need olid kogunenud, ütles Paulus neile: „Mu vennad, kuigi mina ei ole teinud midagi meie rahva ja esivanemate kommete vastu, vahistati mind Jeruusalemmas ja anti üle roomlaste kätte.
18 Baada ya kunihoji, walitamani kuniacha huru, kwa sababu kulikuwa hakuna sababu kwangu mimi ya kustahili adhabu ya kifo.
Ja kui need mind üle kuulasid, tahtsid nad mind vabaks lasta, sest mul ei olnud ühtki surmasüüd.
19 Lakini wale Wayahudi walipoongea kinyume cha shauku yao, nililazimika kukata rufaa kwa Kaisaria, japokuwa haikuwa kana kwamba naleta mashtaka juu ya taifa langu.
Aga kui juudid olid selle vastu, olin ma sunnitud pöörduma keisri poole. Mul polnud mingit kavatsust oma rahva vastu süüdistust esitada.
20 Kwa sababu ya kukata kwangu rufaa, hivyo, niliomba kuwaona na kuongea nanyi. Ni kwa sababu ya kile ambacho Israel anaujasiri kwacho, nimefungwa na kifungo hiki.
Sel põhjusel palusin teid näha ja teiega rääkida. Iisraeli lootuse pärast ma olen kinni ahelates.“
21 Kisha wakamwambia, “Hatujawahi kupokea barua kutoka Yudea kukuhusu wewe, wala hakuna ndugu aliyekuja na kutoa taarifa au kusema neno lolote baya kuhusu wewe.
Aga nemad vastasid: „Me ei ole saanud Juudamaalt ühtegi kirja sinu kohta ega ole tulnud siia ühtegi inimest, kes sinust oleks midagi paha teatanud või rääkinud.
22 Lakini tunataka kusikia kutoka kwako unafikiri nini kuhusu hili kundi la watu hawa, kwa sababu inajulikana kwetu kwamba linaongea kinyume kila mahali.”
Aga me tahame siiski sinu käest kuulda, mida sa mõtled, sest me teame, et selle lahkusu vastu räägitakse kõikjal.“
23 Walipokuwa wametenga siku kwa ajili yake, watu wengi zaidi walimwijia mahali alipokuwa anaishi. Alisema lile jambo kwao na kushuhudia kuhusu ufalme wa Mungu. Alijaribu kuwashawishi kuhusu Yesu, kwa namna zote mbili kutoka katika sheria za Musa na kutoka kwa manabii, kuanzia asubuhi hadi jioni.
Nad korraldasid ühel päeval Paulusega kokkusaamise ja siis tuli veel rohkem inimesi sinna, kus ta viibis. Neile ta tunnistas ja seletas hommikust õhtuni Jumala riigist ning veenis Moosese Seaduse ja Prohvetite põhjal uskuma Jeesusesse.
24 Baadhi yao walishawishika kuhusu mambo yale yaliyosemwa, wakati wengine hawakuamini.
Mõned lasksid end öeldust veenda, teised aga ei suutnud uskuda.
25 Waliposhindwa kukubaliana wao kwa wao, waliondoka baada ya Paulo kulisema jambo hili moja, “Roho Mtakatifu alisema vyema kupitia Isaya nabii kwa baba zenu.
Jõudmata ühisele nõule, lahkusid nad pärast seda, kui Paulus oli öelnud oma viimase sõna: „Püha Vaim rääkis tõtt prohvet Jesaja kaudu teie esivanematele:
26 Alisema, 'Nenda kwa watu hawa useme, “Kwa masikio yenu mtasikia, lakini hamtaelewa; Na kwa macho yenu mtaona lakini hamtatambua.
„Mine selle rahva juurde ja ütle: „Te küll kuulate, aga ei mõista, te küll vaatate, aga ei näe.“
27 Kwa ajili ya mioyo ya watu hawa imekuwa dhaifu, masikio yao yamesikia kwa taabu, wamefumba macho yao; ili kwamba wasijekutambua kwa macho yao, na kusikia kwa masikio yao, na kuelewa kwa mioyo yao, na kugeuka tena, na ningeliwaponya.”'
Selle rahva süda on kalestunud ja nende kõrvakuulmine on nüri ja nad on sulgenud oma silmad. Muidu nad näeksid oma silmadega ja kuuleksid oma kõrvadega ja mõistaksid südamega ning pöörduksid, ja ma teeksin nad terveks.“
28 Kwa hiyo, mnapaswa kujua kwamba huu wokovu wa Mungu umepelekwa kwa watu wa Mataifa, na watasikiliza.” (Zingatia: Mstari huu
Siis olgu teile teada, et see Jumala pääste on läkitatud teistele rahvastele ja nemad võtavad seda kuulda!“
29 “Wakati alipokuwa amesema mambo haya, wayahudi waliondoka, wakiwa na mashindano makubwa kati yao.,” haumo kwenye nakala bora za kale).
Kui ta seda oli öelnud, läksid juudid ära omavahel ägedalt vaieldes.
30 Paulo alikaa katika nyumba yake ya kupanga kwa miaka yote miwili, na aliwakaribisha wote waliokuja kwake.
Paulus jäi kaheks aastaks oma üürimajja ja võttis vastu kõiki, kes tema juurde tulid.
31 Alikuwa akihubiri ufalme wa Mungu na alikuwa akifundisha mambo juu ya Bwana Yesu Kristo kwa ujasiri wote. Hakuna aliyemzuia.
Ta kuulutas Jumala riiki ning õpetas Issandast Jeesusest Kristusest julgelt ja takistusteta!

< Matendo 28 >