< Matendo 27 >
1 Ilipoamuliwa kwamba tunatakiwa tusafiri kwa maji kwenda Italia, walimkabidhi Paulo na wafungwa wengine kwa afisa mmoja wa jeshi la Kiroma aliyeitwa Julio, wa Kikosi cha Agustani.
Kui oli otsustatud, et me purjetame Itaaliasse, anti Paulus ja mõned teised vangid üle sadakonna ülemale Juuliusele, kes kuulus keiserlikku väesalka.
2 Tukapanda meli kutoka Adramitamu, ambayo ilikuwa isafiri kandokando ya pwani ya Asia. Hivyo tukaingia baharini. Aristaka kutoka Thesolanike ya Makedonia akaenda pamoja nasi.
Me astusime Adramüttionist laeva peale, mis pidi sõitma Aasia provintsi ranniku sadamatesse, ja me lahkusime merele. Meiega oli Tessaloonikast pärit makedoonlane Aristarhos.
3 Siku iliyofuata tukatua nanga katika mji wa Sidoni, ambapo Julio alimtendea Paulo kwa ukarimu na akamruhusu kwenda kwa rafiki zake kupokea ukarimu wao.
Järgmisel päeval me randusime Siidonis; ja Juulius kohtles Paulust lahkesti ning lubas tal minna oma sõprade juurde, et need saaksid tema eest hoolt kanda.
4 Kutoka hapo tukaenda baharini tukasafiri kuzunguka kisiwa cha Kipro ambacho kilikuwa kimeukinga upepo, kwa sababu upepo ulikuwa ukitukabili.
Sealt me läksime uuesti merele ja purjetasime Küprose varjus, sest tuuled olid vastu.
5 Baada ya kuwa tumesafiri katika maji yaliyo karibu na Kilikia na Pamfilia, tukaja Mira, mji wa Lisia.
Kui olime Kiliikia ja Pamfüülia ranniku lähedal üle avamere purjetanud, saabusime Müürasse Lüükias.
6 Pale yule afisa wa jeshi la Kiroma, akaikuta meli kutoka Alexandria ambayo ilikuwa isafiri kuelekea Italia. Akatupandisha ndani yake.
Ja kui sadakonna ülem leidis sealt Aleksandria laeva, mis purjetas Itaaliasse, pani ta meid selle pardale.
7 Baada ya kuwa tumesafiri polepole kwa siku nyingi na hatimaye tukawa tumefika kwa taabu karibu na Kinidas, upepo haukuturuhusu tena kuelekea njia hiyo, hivyo tukasafiri kandokando ya kivuli cha Krete tukiukinga upepo, mkabala na Salmone.
Palju päevi liikusime vaevaliselt edasi ja meil oli raskusi saada Knidose kohale. Ja kui tuul ei lasknud meid randa, siis me purjetasime Kreeta varju Salmoone kohal.
8 Tukasafiri kandokando ya pwani kwa ugumu, mpaka tukafika mahali palipoitwa Fari Haveni ambayo iko karibu na mji wa Lasi.
Liikusime vaevaga mööda rannajoont ning jõudsime paika, mida kutsutakse Heaks Sadamaks ja mille lähedal on Lasaia linn.
9 Tulikuwa tumechukua muda mwingi sana, na muda wa mfungo wa Kiyahudi ulikuwa umepita pia, na sasa ilikuwa ni hatari kuendelea kusafiri. Hivyo Paulo akatuonya,
Me olime kaotanud palju aega ja laevasõit oli muutunud ohtlikuks, sest lepituspäev oli möödas. Nii hoiatas Paulus neid:
10 na kusema, “Wanaume, naona safari ambayo tunataka tuichukue itakuwa na madhara na hasara nyingi, siyo tu ya mizigo na meli, lakini pia ya maisha yetu.”
„Mehed, ma näen, et meie reis saab olema katastroofiline ja toob suurt kahju laevale ja lastile ning ka meie enda elule.“
11 Lakini afisa wa jeshi la Kiroma akamsikiliza zaidi bwana wake na mmiliki wa meli, kuliko mambo yale ambayo yalizungumzwa na Paulo.
Kuid sadakonna ülem järgis tüürimehe ja laevaomaniku nõuandeid, selle asemel et Paulust kuulata.
12 Kwa sababu bandari haikuwa sehemu rahisi kukaa wakati wa baridi, mabaharia wengi wakashauri tusafiri kutoka pale, ili kwa namna yoyote tukiweza kuufikia mji wa Foinike, tukae pale wakati wa baridi. Foinike ni bandari huko Krete, na inatazama kaskazini mashariki na kusini mashariki.
Ja et sadam oli talvitamiseks kõlbmatu, otsustas enamus, et peaksime edasi sõitma, lootes jõuda Fööniksisse ja seal talvituda. See oli Kreetal asuv sadam, mis oli avatud edelasse ja loodesse.
13 Upepo wa kusini ulipoanza kuvuma polepole, mabaharia wakafikiri wamepata kile ambacho walikuwa wanakihitaji. Wakang'oa nanga na kusafiri kandokando ya Krete karibu na pwani.
Aga kui õrn lõunatuul hakkas puhuma, nägid nad oma võimalust. Nad hiivasid ankru ja liikusid mööda Kreeta rannajoont.
14 Lakini baada ya muda mfupi upepo mkali, ulioitwa Wa kaskazini mashariki, ukaanza kutupiga kutoka ng'ambo ya kisiwa.
Aga üsna pea sööstis saare poolt alla marutuul, mida hüütakse kirdemaruks.
15 Wakati meli ilipolemewa na kushindwa kuukabili upepo, tukakubaliana na hali hiyo, tukasafirishwa nao.
See kiskus laeva endaga kaasa. Kuna kursil püsimine oli võimatu, siis lihtsalt triivisime.
16 Tukakimbia kupitia ule upande uliokuwa unaukinga upepo wa kisiwa kiitwacho Kauda; na kwa taabu sana tulifanikiwa kuuokoa mtumbwi.
Väikese Kauda saare varjus oli torm natuke vaiksem ja me suutsime hädavaevu toime tulla päästepaadiga.
17 Baada ya kuwa wameivuta, walitumia kamba kuifunga meli. Waliogopa kwamba tungeweza kwenda kwenye eneo la mchanga mwingi la Syiti, hivyo wakashusha nanga na waliendeshwa kandokando.
Mehed tõmbasid selle pardale. Seejärel tõmmati köied laeva alt läbi, et seda koos hoida. Ja kuna kardeti paiskuda Sürtise liivaribadel madalikule, võeti purjed maha ja jäeti laev triivima.
18 Tulipigwa kwa nguvu sana na dhoruba, hivyo siku iliyofuata mabaharia wakaanza kutupa mizigo kutoka melini.
Aga laev sai tormist nii palju vintsutada, et järgmisel päeval loopisid nad osa lasti merre.
19 Siku ya tatu, mabaharia wakaanza kuyatoa maji kwa mikono yao wenyewe.
Kolmandal päeval heitsid nad oma kätega üle parda ka laeva varustuse.
20 Wakati ambapo jua na nyota hazikutuangazia kwa siku nyingi, bado dhoruba kubwa ilitupiga, na matumaini kwamba tungeokolewa yalitoweka.
Aga kui mitu päeva ei paistnud ei päikest ega tähti ja maru läks väga kangeks, kaotasime lõpuks lootuse jääda ellu.
21 Baada ya kuwa wameenda muda mrefu bila chakula, hapo Paulo akasimama katikati ya mabaharia akasema, “Wanaume, mlipaswa mnisikilize, na tusingengo'a nanga kutoka Krete, ili kupata haya madhara na hasara.
Pärast seda, kui nad olid pikka aega olnud söömata, tõusis Paulus nende ette ja ütles: „Mehed, te oleksite pidanud minu sõna kuulama ja Kreetalt mitte väljuma. Siis te oleks vältinud neid purustusi ja kahju.
22 Na sasa nawafariji mjitie moyo, kwa sababu hakutakuwa upotevu maisha kati yenu, isipokuwa hasara ya meli tu.
Nüüd ma aga kutsun teid olema julged, sest keegi teie seast ei hukku, hukkub ainult laev.
23 Kwa sababu usiku uliopita malaika wa Mungu, ambaye huyo Mungu mimi ni wake, na ambaye ninamwabudu pia - malaika wake alisimama pembeni mwangu
Täna öösel seisis minu kõrval selle Jumala ingel, kelle oma ma olen ja keda ma ka teenin
24 na kusema, “Usiogope Paulo. Lazima usimame mbele ya Kaisari, na tazama, Mungu katika wema wake amekupa hawa wote ambao wanasafiri pamoja nawe.
ja ütles: „Ära karda, Paulus! Sa pead jõudma keisri ette; ja Jumal on sulle kinkinud kõigi nende elud, kes koos sinuga sõidavad.“
25 Hivyo, wanaume, jipeni moyo, kwa sababu namwamini Mungu, kwamba itakuwa kama nilivyoambiwa.
Seepärast, mehed, olge julged, sest ma usun Jumalat, et kõik sünnib täpselt nii, nagu mulle on öeldud!
26 Lakini lazima tuumie kwa kupigwa katika baadhi ya visiwa.”
Sellegipoolest peame ühel saarel maale minema.“
27 Ulipofika usiku wa kumi na nne, tulipokuwa tukiendeshwa huko na huko kwenye bahari ya Adratik, kama usiku wa manane hivi, mabaharia walifikiri kwamba wamekaribia nchi kavu.
Neljateistkümnendal ööl triivisime me ikka veel Aadria merel, kui südaöö paiku tajusid meremehed, et me läheneme maale.
28 Walitumia milio kupima kina cha maji na wakapata mita thelathini na sita, baada ya muda mfupi wakapima tena wakapata mita ishirini na saba.
Loodimisel nad leidsid, et vesi oli umbes nelikümmend meetrit sügav. Kui nad natukese aja pärast olid edasi jõudnud, loodisid nad uuesti ja leidsid, et vesi oli kolmkümmend meetrit sügav.
29 Waliogopa kwanza tunaweza kugonga miamba, hivyo wakashusha nanga nne kutoka katika sehemu ya kuwekea nanga na wakaomba kwamba asubuhi ingekuja mapema.
Kartes, et me paiskume karile, heitsid nad laeva ahtrist välja neli ankrut ja jäid ootama päevavalgust.
30 Wale mabaharia walikuwa wanatafuta namna ya kuitelekeza ile meli na walizishusha majini boti ndogo ndogo za kuokolea maisha, na wakajifanya kwamba wanatupa nanga kutoka sehemu ya mbele ya boti.
Aga kui meremehed püüdsid laevast põgeneda ja hakkasid päästepaati merre laskma, teesklesid nad, nagu tahaksid nad veel mõne ankru laeva ninast sisse lasta.
31 Lakini Paulo akamwambia yule askari wa jeshi la Kiroma na wale askari, “Hamuwezi kuokoka isipokuwa hawa watu wanabaki kwenye meli”.
Siis Paulus ütles sadakonna ülemale: „Kui need mehed ei jää laeva, siis te ei pääse eluga!“
32 Kisha wale askari wakakata kamba za ile boti na ikaachwa ichukuliwe na maji.
Siis lõikasid sõdurid katki köied, mis päästepaati hoidsid, ja lasid sellel minema triivida.
33 Wakati mwanga wa asubuhi ulipokuwa unajitokeza, Paulo akawasihi wote angalau wale kidogo. Akasema, “Hii ni siku ya kumi na nne mnasuburi bila kula, hamjala kitu.
Vahetult enne päikesetõusu kutsus Paulus neid kõiki sööma. „Viimased neliteist päeva, “ütles ta, „olete te olnud pinge all ja ilma toiduta – te pole midagi söönud.
34 Hivyo nawasihi mchukue chakula kidogo, kwa sababu hii ni kwa ajili ya kuishi kwenu; na hakuna hata unywele mmoja wa vichwa vyenu utakaopotea.
Nüüd soovitan teil midagi süüa. Te peate ellu jääma. Mitte keegi teist ei kaota peast ühtki juuksekarva!“
35 Alipokwisha kusema hayo, akachukua mkate akamshukuru Mungu mbele ya macho ya kila mtu. Kisha akaumega mkate akaanza kula.
Kui ta seda oli öelnud, võttis ta leiva, tänas Jumalat nende kõikide ees, murdis ja hakkas sööma.
36 Kisha wote wakatiwa moyo na wao wakachukua chakula.
Siis nende kõikide meel läks heaks ja nad võtsid ka leiba.
37 Tulikuwa watu 276 ndani ya meli.
Kokku oli meid laeval kakssada seitsekümmend kuus inimest.
38 Walipokwisha kula vya kutosha, waliifanya meli nyepesi kwa kutupa ngano ndani ya bahari.
Kui nende kõhud said täis, kergendasid nad veel laeva, heites vilja merre.
39 Ilipokuwa mchana, hawakuitambua nchi kavu, lakini wakaona sehemu ya nchi kavu iliyoingia majini iliyokuwa na mchanga mwingi. wakajadiliana kama wanaweza kuiendesha meli kuelekea hapo.
Kui valgeks läks, siis nad ei tundnud, mis maa see on; aga nad nägid liivase rannaga lahte, kuhu nad otsustasid, kui nad suudavad, laeva ajada.
40 Hivyo wakazilegeza nanga wakaziacha baharini. Katika muda huo huo wakazilegeza kamba za tanga na wakaiinua sehemu ya mbele kuelekea kwenye upepo, hivyo wakaelekea kwenye hiyo sehemu ya mchanga mwingi.
Nad raiusid ankrud lahti ja jätsid need merre; samal ajal sidusid lahti tüüriaerude köied ja seadsid esipurje tuulde ning püüdsid juhtida laeva ranna poole.
41 Lakini wakaja mahali ambapo mikondo miwili ya maji inakutana, na meli ikaelekea mchangani. Na ile sehemu ya mbele ya meli ikakwama pale na haikuweza kutoka, lakini sehemu ya mbele ya meli ikaanza kuvunjika kwa sababu ya ukali wa mawimbi.
Ent nad sattusid liivaseljakule ja ajasid laeva sinna kinni. Laeva käil tungis sinna sisse ja jäi kinni, ahter purunes aga lainte möllus tükkideks.
42 Mpango wa wale askari ulikuwa ni kuwaua wafungwa, ili kwamba hakuna ambaye angeogelea na kutoroka.
Sõdurid kavatsesid vangid ära tappa, et ükski neist ei pääseks ujudes põgenema.
43 Lakini yule askari wa jeshi la Kiroma alitaka kumwokoa Paulo, hivyo akausimamisha mpango wao; na akawaamuru wale ambao wanaweza kuogelea, waruke kutoka melini kwanza na waende nchi kavu.
Aga sadakonna ülem tahtis päästa Pauluse elu ja takistas neil plaani täide viimast. Ta käskis neil, kes oskavad ujuda, üle parda hüpata ja maale ujuda.
44 Kisha wanaume wengine watafuata, wengine juu ya vipande vya mbao na wengine juu ya vitu vingine kutoka kwenye meli. Kwa njia hii ikatokea kwamba wote tutafika salama nchi kavu.
Teised pidid sinna jõudma plankudel või muudel laevaosadel. Sel viisil jõudsid kõik tervelt maale.