< Matendo 12 >
1 Wakati huo mfalme Herode akanyosha mkono wake kwa baadhi ya wale wanaotoka kwenye kusanyiko ili kuwatesa.
En ce temps-là, le roi Hérode porta les mains sur quelques-uns de l’Eglise pour les tourmenter.
2 Akamwuua Yakobo nduguye Yohana kwa upanga.
Il fit mourir par le glaive Jacques, frère de Jean.
3 Baada ya kuona kuwa inawapendeza Wayahudi, akamkamata na Petro tena. Hii ilikuwa wakati wa mikate isiyochachwa.
Et voyant que cela plaisait aux Juifs, il fit aussi prendre Pierre. Or c’étaient les jours des azymes.
4 Alipomkamata, akamweka gerezani na akaweka vikosi vinne vya askari ili kumlinda, alikuwa akitarajia kumpeleka kwa watu baada ya Pasaka.
Lorsqu’il l’eut pris, il le mit en prison, le confiant à la garde de quatre bandes de quatre soldats chacune, voulant, après la pâque, le produire devant le peuple.
5 Petro akawekwa gerezani, lakini maombi yakafanywa kwa bidii na kusanyiko kwa ajili yake kwa Mungu.
Ainsi Pierre était gardé dans la prison. Mais l’Eglise faisait à Dieu, sans interruption, des prières pour lui.
6 Siku kabla Herode hajaenda kumtoa, Usiku huo Petro alikuwa amelala katikati ya maaskari wawili, akiwa amefungwa na minyororo miwili, na walinzi mbele ya mlango walikuwa wakilinda gereza.
Or la nuit même d’avant le jour où Hérode devait le produire, Pierre dormait entre deux soldats, lié de deux chaînes, et des gardes devant la porte gardaient la prison.
7 Tazama, malaika wa Bwana ghafla akamtokea na nuru ikang'aa ndani. Akampiga Petro ubavuni na kumwamsha akisema, “Amka haraka.”ndipo minyororo aliyokuwa amefungwa ikafunguka kutoka mikononi mwake.
Et voilà qu’un ange du Seigneur se présenta, et une lumière brilla dans la prison; alors l’ange, frappant Pierre au côté, le réveilla, disant: Lève-toi promptement. Et les chaînes tombèrent de ses mains.
8 Malaika akamwambia, “Vaa nguo zako na vaa viatu vyako.” Petro akafanya hivyo. Malaika akamwambia, “Vaa vazi lako na unifuate.”
Alors l’ange lui dit: Ceins-toi et mets la chaussure à tes pieds. Et il fit ainsi. Et l’ange dit: Prends ton vêtement autour de toi, et suis-moi.
9 Hivyo Petro akamfuata Malaika na akatoka nje. Hakuamini kilichofanywa na malaika kama ni cha kweli. Alidhani anaona maono.
Et sortant, il le suivait, et il ne savait pas que ce qui se faisait par l’ange fût véritable; car il croyait avoir une vision.
10 Baada ya kupita lindo la kwanza na la pili, wakafika kwenye geti la chuma la kuingilia kwenda mjini, likafunguka lenyewe kwa ajili yao. Wakatoka nje wakashuka kwenye mtaa, mara Malaika akamwacha.
Or ayant passé la première et la seconde garde, ils vinrent à la porte de fer qui mène à la ville; elle s’ouvrit d’elle-même à eux. Et, sortant, ils s’avancèrent dans une rue; et aussitôt l’ange le quitta.
11 Petro alipojitambua, akasema, “Sasa nimeamini kuwa Bwana alimtuma Malaika wake ili kunitoa katika mikono ya Herode, na kwa matarajio ya watu wote wa uyahudi.”
Alors Pierre, revenu à lui, dit: Maintenant je reconnais véritablement que Dieu a envoyé son ange, et qu’il m’a soustrait à la main d’Hérode et à toute l’attente du peuple juif.
12 Baada ya kujua haya, akaja kwenye nyumba ya Mariamu mama yake Yohana ambaye ni Marko; Wakristo wengi walikusanyika wakiomba.
Et, réfléchissant, il vint à la maison de Marie, mère de Jean, qui est surnommé Marc, où beaucoup de personnes étaient assemblées et priaient.
13 Alipobisha kwenye mlango wa kizuizi, mtumishi mmoja msichana anayeitwa Roda akaja kufungua.
Or, comme il frappait à la porte, une jeune fille, nommée Rhode, vint pour écouter.
14 Alipotambua ni sauti ya Petro, kwa furaha akashindwa kuufungua mlango; badala yake, akakimbia ndani ya chumba; na kuwajulisha kuwa Petro amesimama mbele ya Mlango.
Dès qu’elle reconnut la voix de Pierre, transportée de joie, elle n’ouvrit pas la porte, mais, rentrant en courant, elle annonça que Pierre était à la porte.
15 Hivyo, Wakasema kwake, “Wewe ni mwendawazimu” lakini alikazia kuwa ni kweli ni yeye. Wakasema “Huyo ni malaika wake.”
Ils lui dirent: Tu es folle. Mais elle assurait qu’il en était ainsi. Sur quoi ils disaient: C’est son ange.
16 Lakini Petro aliendelea kubisha, na walipofungua mlango, wakamwona na wakashangaa sana. Petro akawanyamazisha kwa mkono kimya kimya na akawaambia jinsi Bwana alivyomtoa kutoka Gerezani. akasema,
Cependant Pierre continuait de frapper. Et lorsqu’ils eurent ouvert, ils le virent et furent dans la stupeur.
17 “Wajulishe haya mambo Yakobo na ndugu zake.” Kisha akaondoka akaenda sehemu nyingine.
Mais lui, leur faisant de la main signe de se taire, raconta comment le Seigneur l’avait tiré de la prison, et il dit: Annoncez ces choses à Jacques et à nos frères. Et étant sorti, il s’en alla dans un autre lieu.
18 Kulipokuwa mchana, kukawa na huzuni kubwa kati ya askari, kuhusiana na kilichotokea kwa Petro.
Quand il fit jour, il n’y eut pas peu de trouble parmi les soldats, au sujet de ce que Pierre était devenu.
19 Baada ya Herode kumtafuta na hakumwona akawauliza walinzi na akaamuru wauawe. Akaenda kutoka uyahudi mpaka Kaisaria na kukaa huko.
Hérode l’ayant fait chercher, et ne l’ayant point trouvé, fit donner la question aux gardes, et commanda de les mener au supplice; puis il descendit de Jérusalem à Césarée, où il séjourna.
20 Herode alikuwa na hasira juu ya watu wa Tiro na Sidoni. Wakaenda kwa pamoja kwake. Wakawa na urafiki na Blasto msaidizi wa mfalme, ili awasaidie. Kisha wakaomba amani, kwa sababu nchi yao ilipokea chakula kutoka katika nchi ya mfalme.
Il était irrité contre les Tyriens et les Sidoniens. Mais ils vinrent d’un commun accord vers lui, et Blaste, chambellan du roi, ayant été gagné, ils demandaient la paix, parce que leur pays tirait sa subsistance des terres du roi.
21 Siku iliyokusudiwa Herode alivaa mavazi ya kifalme na kukaa kwenye kiti chake cha kifalme, na akawahutubia.
Ainsi, au jour fixé, Hérode, revêtu du vêtement royal, s’assit sur son trône, et il les haranguait.
22 Watu wakapiga kelele, “Hii ni sauti ya mungu wala si sauti ya mwanadamu!”
Et le peuple applaudissait, criant: C’est le discours d’un dieu et non d’un homme.
23 Mara ghafla malaika akampiga, kwa sababu alikuwa hakumpa Mungu utukufu; akaliwa na chango na akafa
Et soudain un ange du Seigneur le frappa, parce qu’il n’avait point rendu gloire à Dieu; et, mangé des vers, il expira.
24 Lakini neno la Mungu likakua na kusambaa.
Cependant la parole de Dieu croissait et se multipliait.
25 Baada ya Barnaba na Sauli kukamilisha huduma yao wakatoka pale wakarejea Yerusalemu, wakamchukua na Yohana ambaye jina la kuzaliwa ni Marko.
Et Barnabé et Saul, leur mission remplie, revinrent de Jérusalem, ayant pris avec eux Jean, qui est surnommé Marc.