< 2 Timotheo 1 >
1 Paulo mtume wa Yesu Kristo kwa mapenzi ya Mungu, sawasawa na ahadi ya uzima ulio ndani ya Kristo Yesu,
Paul, an apostle of Jesus Christ through the will of God, according to the commandment of life which is in Christ Jesus,
2 kwa Timotheo mwana mpendwa: Neema, rehema na amani toka kwa Mungu Baba na Kristo Yesu Bwana wetu.
to Timothy, my beloved child. Grace, mercy, peace from God our Father and Jesus Christ our Lord.
3 Ninamshukuru Mungu, ambaye ninamtumikia kwa nia njema kama walivyofanya baba zangu, ninapokumbuka daima katika maombi yangu. Usiku na
I give thanks to God, whom I serve from my ancestors with a clean conscience, as I have incessant mention of you in my prayers, night and day
4 mchana ninatamani kukuona, ili kwamba nijawe na furaha. Ninayakumbuka machozi yako.
longing to see you, remembering your tears, in order that I may be filled with joy;
5 Nimekuwa nikikumbushwa kuhusu imani yako halisi, ambayo hapo kwanza ilikaa kwa bibi yako Loisi na mama yako Yunisi. Na nina hakika ya kwamba imani hiyo inakaa ndani yako pia.
having received the remembrance of the unhypocritical faith which is in you; which dwelt first in your grandmother Lois, and your mother Eunice; and, I am persuaded that it is in you also.
6 Hii ndiyo sababu nakukumbusha kuchochea karama ya Mungu iliyomo ndani yako kwa njia ya kuwekewa mikono yangu.
On account of which cause I remind you to revive and refire the gift of God which is in you by the laying on of my hands.
7 Kwa kuwa Mungu hakutupa roho ya woga, bali ya nguvu na upendo na nidhamu.
For God has not given us the spirit of cowardice; but of power and divine love and prudence.
8 Kwa hiyo usiuonee haya ushuhuda kuhusu Bwana wetu, wala wangu mimi Paulo mfungwa wake. Bali ushiriki mateso kwa ajili ya injili sawasawa na uweza wa Mungu.
Therefore do not be ashamed of the testimony of our Lord, nor me his prisoner: but suffer affliction for the sake of the gospel according to the power of God;
9 Ni Mungu aliyetuokoa na kutuita kwa wito mtakatifu. Hakufanya hivi kulingana na kazi zetu bali kulingana na neema na mpango wake mwenyewe. Alitupatia mambo haya katika Kristo Yesu kabla ya nyakati kuanza. (aiōnios )
the one having saved us, and called us with a holy calling, not according to our works, but according to his own purpose and grace, which was given to us in Christ Jesus before the eternal times, (aiōnios )
10 Lakini sasa wokovu wa Mungu umekwishafunuliwa kwa kuja kwa mwokozi wetu Kristo Yesu. Ni Kristo aliyeikomesha mauti na kuleta uzima usiokoma kwa nuru ya injili.
but now having been made manifest through the appearing of Jesus Christ our Saviour, the one having indeed destroyed death, and lighted up life and immortality through the gospel,
11 Kwa sababu hiyo nilichaguliwa kuwa mhubiri, mtume na mwalimu.
unto which I have been placed a herald, and an apostle, and teacher:
12 Kwa sababu hii nateseka pia, lakini sioni haya kwa kuwa namjua yeye niliyekwisha kumuamini. Nina hakika kuwa yeye anaweza kukitunza kile nilichokikabidhi kwake hata siku ile.
on account of which cause I indeed suffer these things: but I am not ashamed; for I know whom I have believed, and am persuaded that he is able to stand guard over that which is committed unto me unto that day.
13 Ukumbuke mfano wa ujumbe wa uaminifu uliousikia toka kwangu, pamoja na imani na upendo ulio ndani ya Kristo Yesu.
Hold fast the form of sound words which you heard with me, in the faith and divine love which is in Christ Jesus:
14 Yatunze Mambo mazuri aliyokukabidhi Mungu kupitia Roho Mtakatifu aishiye ndani yetu.
stand guard over the beautiful deposit through the Holy Ghost who dwells in us.
15 Unajua ya kuwa, wote waishio katika Asia waliniacha. Kwenye kundi hili wamo Figelo na Hemogene.
You know this, that all who are in Asia, of whom are Phygelus and Hermogenes have turned away from me.
16 Bwana airehemu nyumba ya Onesiforo kwa kuwa mara nyingi aliniburudisha na hakuionea aibu minyororo yangu.
May the Lord grant mercy to the family of Onesiphorus, because frequently he refreshed me, and was not ashamed of my chain,
17 Badala yake, alipokuwa Roma alinitafuta kwa bidii na akanipata.
and, being in Rome, he diligently sought me, and found me.
18 Mungu amjalie kupata rehema kutoka kwake siku ile. Kama alivyonisaidia nilipokuwa Efeso, wewe wajua vyema.
May the Lord grant unto him to find mercy with the Lord in that day. And so many things as he ministered in Ephesus, you know better.