< 1 Timotheo 6 >

1 Wale wote walio chini ya nira kama watumwa wawachukulie mabwana zao kama wenye heshima zote, wanatakiwa kufanya hivyo ili jina la Mungu na mafundisho yasitukanwe.
Let the servants so many as are under the yoke, esteem those who are their masters worthy of all honor, in order that the name and doctrine of God may not be blasphemed.
2 Watumwa wenye mabwana waaminio wasiwadharau kwa sababu wao ni ndugu. Badala yake, wawatumikie zaidi. Kwa sababu mabwana wanaosaidiwa kazi zao ni waamini na wanapendwa. Fundisha na kuyatangaza mambo haya.
But let those that have faithful masters not despise them, because they are brethren; but rather let them serve them, because they are the faithful and beloved who are partaking of the benefaction. Command these things and exhort them.
3 Iwapo mtu fulani anafundisha kwa upotovu na hayapokei maelekezo yetu yenye kuaminika, ambayo ni maneno ya Bwana wetu Yesu Kristo, iwapo hawalikubali fundisho liongozalo kwenye utauwa.
If any one teaches another doctrine, and does not give heed to the sound words which belonged to our Lord Jesus Christ, and to the doctrine which is according to godliness;
4 Mtu huyo anajivuna na hajui chochote. Badala yake, ana vurugu na mabishano juu ya maneno. Maneno haya huzaa wivu, ugomvi, matukano, shuku mbaya,
he has been inflated, knowing nothing, but doting about questions and controversies, from which come envy, strife, blasphemies, evil surmisings,
5 na vurugu za mara kwa mara kati ya watu wenye akili zilizoharibika. Wanaiacha kweli. Wanafikiri kwamba utauwa ni njia ya kuwa matajiri”
wranglings of men having been corrupted as to their mind and turned away from the truth, considering that gain is godliness.
6 Sasa utauwa na kuridhika ni faida kubwa.
Godliness with contentment is great gain,
7 Kwa maana hatukuja na chochote duniani. Wala hatuwezi kuchukua chochote kutoka duniani.
for because we have brought nothing into the world, we are not able to carry any thing out;
8 Badala yake, tutosheke na chakula na mavazi.
however having food and raiment we shall be contented with these.
9 Sasa hao watakao kuwa na mali huanguka katika majaribu, katika mtego. Huanguka katika upumbavu mwingi na tamaa mbaya, na katika kitu chochote kinachowafanya watu wazame katika maangamizi na uharibifu.
But those wishing to be rich fall into temptation and a snare and many foolish and hurtful lusts, which drown the people in destruction and perdition.
10 Kwa kuwa kupenda fedha ni chanzo cha aina zote za uovu. Watu ambao hutamani hiyo, wamepotoshwa mbali na imani na wamejichoma wenyewe kwa huzuni nyingi.
For the love of money is a root of all evils: which some seeking after have wandered from the faith, and pierced themselves through with many sorrows.
11 Lakini wewe mtu wa Mungu, yakimbie mambo hayo. Fuata haki, utauwa, uaminifu, upendo, usitahimilivu, na upole.
But you, O man of God, fly from these things; and pursue righteousness, godliness, faith, divine love, patience, meekness.
12 Piga vita vizuri vya imani. Shikilia uzima wa milele ulioitiwa. Ilikuwa ni kwa sababu hii kwamba ulitoa ushuhuda mbele ya mashahidi wengi kwa kile kilicho chema. (aiōnios g166)
Fight the good fight of faith, lay hold on eternal life, into which you have been called, and witnessed a beautiful testimony before many witnesses. (aiōnios g166)
13 Nakupa amri hii mbele za Mungu, anayesababisha vitu vyote kuishi, na mbele ya Yesu Kristo, aliyenena iliyo kweli kwa Pontio Pilato:
I charge you before God, who creates life in all things, and Jesus Christ, who witnessed a beautiful testimony before Pontius Pilate,
14 itunze amri kwa ukamilifu, pasipo mashaka, hadi ujio wa Bwana wetu Yesu Kristo.
that you keep the commandment, spotless and pure, unto the appearing of our Lord Jesus Christ:
15 Mungu atadhihirisha ujio wake kwa wakati sahihi- Mungu, Mbarikiwa, nguvu pekee, Mfalme anayetawala, Bwana anayeongoza.
which the blessed and only Sovereign, the King of the kings, and Lord of the lords, will manifest in his own due times;
16 Peke yake anaishi milele na akaaye katika mwanga usiokaribiriwa. Hakuna mtu awezaye kumwona wala awezaye kumtazama. Kwake iwe heshima na uweza wa milele. Amina. (aiōnios g166)
he alone having immortality, inhabiting light unapproachable; whom no one of men has seen, or is able to see: to whom be honor and power eternal. Amen. (aiōnios g166)
17 Waambie matajiri katika ulimwengu huu wasijivune, na wasitumaini katika utajiri, ambao siyo wa uhakika. Badala yake, wanapaswa kumtumaini Mungu. Ambaye hutupatia utajiri wote wa kweli ili tufurahie. (aiōn g165)
Charge the rich in this world not to think high things, nor to hope in uncertain riches, but in God, who richly supplies us all things for our enjoyment; (aiōn g165)
18 Waambie watende mema, watajirike katika kazi njema, wawe wakarimu, na utayari wa kutoa.
that they do good, be rich in good works, be cheerful givers, ready communicators;
19 Katika njia hiyo watajiwekea msingi mzuri kwa mambo yajayo, ili kwamba waweze kushika maisha halisi.
laying up for themselves a good foundation for the future, that they may lay hold on the life which is life indeed.
20 Timotheo, linda kile ulichopewa. Jiepushe na majadiliano ya kipumbavu na mabishano yenye kujipinga ambayo kwa kwa uongo huitwamaarifa.
O Timothy, stand guard over that which has been committed to you, avoiding unsanctified, empty talks and oppositions of knowledge falsely so called,
21 Baadhi ya watu huyatangaza mambo haya, na hivyo wameikosa imani. Neema na iwe pamoja nawe.
which some proclaiming have made shipwreck concerning the faith. Grace be with you.

< 1 Timotheo 6 >