< 2 Wathesalonike 3 >

1 Na sasa, ndugu, tuombeeni, kwamba neno la Bwana liweze kuenea na kutukuzwa, kama ilivyo pia kwenu.
Por lo demás, hermanos míos, oren por nosotros para que la palabra del Señor avance con mayor gloria;
2 Ombeni kwamba tuweze kuokolewa kutoka katika uovu na watu waasi, kwa kuwa si wote wana imani.
Y para que seamos liberados de los hombres necios y malvados; porque no todos tienen fe.
3 Lakini Bwana ni mwaminifu, ambaye atawaimarisha ninyi na kuwalinda kutoka kwa yule mwovu.
Pero el Señor es verdadero, quien les dará fortaleza y los mantendrá a salvo del mal.
4 Tunaujasiri katika Bwana kwa ajili yenu, kwamba mnatenda na mtaendelea kutenda mambo ambayo tunawaagiza.
Y tenemos fe en el Señor acerca de ustedes, que están haciendo y harán las cosas que les hemos mandado.
5 Bwana aweze kuongoza mioyo yenu katika upendo na katika uvumilivu wa Kristo.
Y que sus corazones sean guiados por el Señor para que comprendan que profundo es el amor de Dios por ustedes y a la paciencia de Cristo.
6 Sasa tunawaagiza, ndugu, katika jina la Bwana Yesu Kristo, kwamba mwepuke kila ndugu ambaye anaishi maisha ya uvivu na siyo kwa kutokana na desturi ambazo mlipokea kutoka kwetu.
Ahora les damos órdenes, hermanos, en el nombre de nuestro Señor Jesucristo, para mantenernos alejados de todos aquellos cuyo comportamiento no está bien ordenado y en armonía con la enseñanza que recibieron de nosotros.
7 Kwa kuwa ninyi wenyewe mnajua ni sawa kwenu kutuiga sisi. Hatukuishi miongoni mwenu kama wale ambao hawakuwa na nidhamu.
Ustedes mismos están acostumbrados a tomarnos como ejemplo, porque nuestra vida entre ustedes fue gobernada por orden,
8 Na hatukula chakula cha mtu yeyote bila kukilipia. Badala yake, tulifanya kazi usiku na mchana kwa kazi ngumu na kwa shida, ili tusiweze kuwa mzigo kwa yeyote katika ninyi.
Y no tomamos comida de ningún hombre por nada, sino que trabajamos duro noche y día para no ser una carga a ninguno de ustedes:
9 Tulifanya hivi si kwa sababu hatuna mamlaka. Badala yake, tulifanya hivi ili tuwe mfano kwenu, ili kwamba mweze kutuiga sisi.
No porque no tengamos el derecho, sino para convertirnos en un ejemplo para que ustedes puedan hacer lo mismo.
10 Wakati tulipokuwa pamoja nanyi tuliwaagiza, “Ikiwa mmoja wenu hataki kufanya kazi, na asile.”
Porque aun cuando estábamos con ustedes, les dimos órdenes, diciendo: Si alguno no quisiera trabajar, que tampoco coma.
11 Kwa kuwa tunasikia kwamba baadhi wanaenenda kwa uvivu miongoni mwenu. Hawafanyi kazi lakini badala yake ni watu wasio na utaratibu.
Porque ha llegado a nuestros oídos que hay algunos entre ustedes cuyo comportamiento es descontrolado, que no trabajan en absoluto, pero están demasiado interesados en los asuntos de los demás.
12 Sasa hao nao tunaagiza na kuwaasa katika Bwana Yesu Kristo, kwamba lazima wafanye kazi kwa utulivu na kula chakula chao wenyewe.
Ahora, a los tales, damos órdenes y exhortamos pedimos en el Señor Jesús que, trabajen tranquilamente, y para ganarse la vida.
13 Lakini ninyi, ndugu, msizimie roho katika kufanya yaliyo sahihi.
Y ustedes, mis hermanos, no se cansen de hacer el bien.
14 Ikiwa mtu yeyote hataki kutii neno letu katika waraka huu, mwe makini naye na msiwe na ushirika pamoja naye, ili kwamba aweze kuaibika.
Y si alguno no presta atención a lo que hemos dicho en esta carta, toma nota de ese hombre, y aléjate de él, para que se avergüence.
15 Msimchukulie kama adui, lakini mwonyeni kama ndugu.
No lo tengan por enemigo, pero corríjanlo como hermano.
16 Bwana wa amani mwenyewe awape amani wakati wowote katika njia zote. Bwana awe nanyi nyote.
Ahora el Señor de la paz mismo te dará paz en todo tiempo y en todo sentido. Que el Señor esté con todos ustedes.
17 Hii ni salam yangu, Paulo, kwa mkono wangu mwenyewe, ambayo ni alama katika kila waraka. Hivi ndivyo niandikavyo.
Estas palabras de amor para ustedes al final están en mi puño y letra, así firmo todas mis cartas, y esta es la marca de cada carta mía.
18 Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iweze kuwa nanyi nyote.
La gracia de nuestro Señor Jesucristo sea con todos ustedes.

< 2 Wathesalonike 3 >