< 2 Wafalme 25 >

1 Ilitokea kwamba katika mwaka wa tisa wa utawala wa mfalme Sedekia, katika mwezi wa kumi, na siku ya kumi ya huo mwezi, Nebukadreza mfalme wa Babeli alikuja pamoja na jeshi lake lote kwa ajili ya kupigana dhidi ya Yerusalemu. Akaweka kambi kuelekeana nayo, na wakajenga ukuta kuizunguka.
W dziewiątym roku jego panowania, dziesiątego miesiąca, dziesiątego [dnia tego] miesiąca, Nabuchodonozor, król Babilonu, wraz z całym swoim wojskiem wyruszył przeciw Jerozolimie, rozbił obóz pod nią i zbudował przeciwko niej szańce dokoła.
2 Hivyo mji huo ulizungukwa mpaka miaka kumi na moja ya utawala wa Sedekia.
I miasto było oblężone aż do jedenastego roku króla Sedekiasza.
3 Katika siku ya tisa ya mwezi wa nne wa huo mwaka, njaa ilikuwa kali sana kwenye huo mji kwamba hapakuwa na chakula kwa ajili ya watu wa nchi.
A w dziewiątym dniu [czwartego] miesiąca wzmógł się głód w mieście i nie było chleba dla ludu [tej] ziemi.
4 Wakati huo ule mji ulikuwa umebomoka ndani, na wapiganaji wote wakakimbia usiku kwa njia ya lango kati ya kuta mbili, karibu na bustani ya mfalme, ingawa Wakaldayo walikuwa wote wameuzunguka mji. Mfalme akaenda kuelekea upande wa Araba.
Kiedy zrobiono wyłom [w murze] miasta, wszyscy wojownicy [uciekli] w nocy przez bramę między dwoma murami obok królewskiego ogrodu. Chaldejczycy zaś znajdowali się dokoła miasta, a [król] uszedł w stronę pustyni.
5 Lakini jeshi la Wakaldayo likamfuata mfalme Sedekia na kumchukua katika tambarare ya bonde la Mto Yoradani karibu na Yeriko. Jeshi lake lote lilitawanyika wakamwacha.
I wojsko Chaldejczyków ścigało króla, i dogoniło go na równinach Jerycha, a całe jego wojsko rozpierzchło się od niego.
6 Wakamkamata mfalme na kumleta mpaka kwa mfalme wa Babeli huko Ribla, ambapo walipitisha hukumu juu yake.
Pojmali więc króla i przyprowadzili go do króla Babilonu, do Ribla, gdzie ten wydał na niego wyrok.
7 Kama kwa watoto wa Sedekia, wakawachinja mbele ya macho yake. Kisha akamtoa macho Sedekia, wakamfunga pingu, na kumpeleka hadi Babeli.
I synów Sedekiasza zabili na jego oczach, a Sedekiaszowi wyłupili oczy, zakuli go spiżowymi łańcuchami i uprowadzili do Babilonu.
8 Basi katika mwezi wa tano, katika siku ya saba ya mwezi, ambapo ulikuwa mwaka wa kumi na tisa wa utawala wa Nebukadreza mfalme wa Babeli, Nebuzaradani, mtumishi wa mfalme wa Babeli na amrijeshi wa walinzi wake, wakaja hadi Yerusalemu.
W piątym miesiącu, siódmego [dnia] tego miesiąca – był to dziewiętnasty rok Nabuchodonozora, króla Babilonu – do Jerozolimy przybył Nebuzaradan, dowódca gwardii, sługa króla Babilonu;
9 Akaichoma moto nyumba ya Yahwe, nyumba ya mfalme, na nyumba zote za Yeruselemu; pia kila jengo la muhimu katika mji akayachoma.
I spalił dom PANA i dom króla; wszystkie domy Jerozolimy i wszystkie wielkie budowle spalił ogniem.
10 Kama kwa kuta zote zilizoizunguka Yerusalemu, jeshi lote la Wababeli ambao walikuwa chini ya amrishi wa walinzi wakaziharibu.
Całe wojsko Chaldejczyków, które było z dowódcą gwardii, zburzyło mury wokół Jerozolimy.
11 Basi watu waliokuwa wamebaki ambao walikuwa wameondoka katika mji, wale waliokuwa wameasi kwa mfalme wa Babeli, na mabaki ya watu-Nebuzadani, amiri jeshi wa mlinzi, wakachukuliwa kwenda utumwani.
Resztę ludu, która pozostała w mieście, zbiegów, którzy przeszli do króla Babilonu, oraz resztę pospólstwa Nebuzaradan, dowódca gwardii, uprowadził do niewoli.
12 Lakini amiri jeshi wa mlinzi aliwaacha baadhi ya maskini wa nchi ili wafanye kazi kwenye shamba la mizabibu na kulima.
Lecz dowódca gwardii pozostawił niektórych spośród ubogich tej ziemi, aby byli winogrodnikami i rolnikami.
13 Na zile nguzo za shaba ambazo zilikuwa kwenye nyumba ya Yahwe, na misimamio na bahari ya chuma ambayo ilikuwa kwenye nyumba ya Yahwe, Wakaldayo wakazivunja vipande vipande na kubeba shaba kuirudisha Babeli.
Chaldejczycy rozbili kolumny z brązu, które były w domu PANA, podstawy i morze z brązu, które było w domu PANA, a brąz z nich przenieśli do Babilonu.
14 Masufuria, mabeleshi, makasi, vijiko, na vyombo vyote vya shaba ambavyo kuhani alivyokuwa amevitunza kwenye hekalu-Wakaldayo wakavichukua vyote.
Zabrali też kotły, szufle, nożyce, miski oraz wszystkie naczynia z brązu, których używano do służby.
15 Masufuria ya kuhamisha majivu na mabakuli ambayo yalikuwa yametengenezwa kwa dhahabu, na yale yaliyotengenezwa kwa fedha-yule nahodha wa mlinzi wa mfalme akavichukua pia.
Dowódca gwardii zabrał kadzielnice, miednice i to, co było ze złota, jako złoto, i to, co było ze srebra, jako srebro;
16 Zile nguzo mbili, ile bahari, na vile vitako ambavyo Suleimani alivitengeneza kwa ajili ya nyumba ya Yahwe shaba ya vyombo hivyo vyote haikuwa na uzani.
Dwie kolumny, jedno morze, podstawy, które wykonał Salomon dla domu PANA, a nie było można [zmierzyć] wagi brązu tych wszystkich przedmiotów.
17 Urefu wa ile nguzo ya kwanza ulikuwa ridhaa kumi na nane, na kichwa cha shaba kilikuwa juu yake. Na urefu wa kichwa ulikuwa ridhaa tatu, pamoja na mapambo ya wavu na makomamanga yote yakizunguka kwenye hicho kichwa, vyote vilikuwa vimetengenezwa kwa shaba. Na ile nguzo nyingine ilikuwa vivyo hivyo kama ile ya kwanza pamoja na wavu wake.
Osiemnaście łokci wysokości miała jedna kolumna, a głowica na niej była z brązu. Wysokość głowicy wynosiła trzy łokcie, a siatka i jabłka granatu naokoło głowicy – wszystko było z brązu. Tak samo było na siatce drugiej kolumny.
18 Yule amiri jeshi wa mlinzi akamchukua Seraya kuhani mkuu, pamoja za Sefania, yule kuhani wa pili, na walinzi watatu wa kwenye lango.
Dowódca gwardii zabrał też najwyższego kapłana Serajasza, drugiego kapłana Sofoniasza i trzech stróżów progu.
19 Kutoka mjini akamchukua mlinzi, afisa mmoja ambaye aliyekuwa msimamizi wa maaskari, na watu watano ambao walikuwa wakimshauri mfalme, ambao walikuwa bado katika mji. Pia alimchukua mfungwa wa afisa jeshi la mfalme, kwa ajili ya kuandika watu kwenye jeshi, pamoja na watu sitini muhimu kutoka hiyo nchi ambao walikuwa katika mji.
Z miasta zaś zabrał dworzanina, który był przełożonym nad wojownikami, pięciu spośród tych, którzy stawali przed królem, a znaleziono ich w mieście, naczelnego pisarza wojskowego dokonującego poboru ludu tej ziemi oraz sześćdziesięciu mężczyzn spośród ludu tej ziemi, których znaleziono w mieście.
20 Kisha Nebuzaradani, amiri wa mlinzi, akawachukua na kuwapeleka kwa mfalme Babeli huko Ribla.
Tych pojmał Nebuzaradan, dowódca gwardii, i zaprowadził do króla Babilonu do Ribla.
21 Mfalme wa Babeli akawaua huko Ribla katika nchi ya Hamathi. Kwa njia hii, Yuda akaiacha nchi yake kwenda utumwani.
I król Babilonu pobił ich, i uśmiercił w Ribla, w ziemi Chamat. Tak został uprowadzony Juda ze swojej ziemi.
22 Na wale watu waliokuwa wamebakia katika nchi ya Yuda, wale ambao Nebukadreza mfalme wa Babeli aliwaacha, akamuweka Gedalia mwana wa Ahikamu, mwana wa Shafani, msimamizi wao.
Nad ludem zaś, który jeszcze pozostał w ziemi Judy, a który Nabuchodonozor, król Babilonu, zostawił, ustanowił on Gedaliasza, syna Achikama, syna Szafana.
23 Kisha wakati maamiri wote wa majeshi, wao na watu wao, waliposikia kwamba mfalme wa Babeli amemfanya Gedalia kuwa liwali, wakaenda kwa Gedalia huko Mispa. Hawa watu walikuwa Ishmaeli mwana wa Nethania, Yohanani mwana wa Karea, Seraya mwana wa Tanhumethi Mnetofa, na Yezania mwana wa Mmaaka-wao na watu wao.
A gdy wszyscy dowódcy wojska usłyszeli, oni i ich ludzie, że król Babilonu ustanowił Gedaliasza namiestnikiem, przyszli do Gedaliasza do Mispy. Byli to: Izmael, syn Netaniasza, Jochanan, syn Kareacha, Serajasz, syn Tanchumeta Netofatyta, i Jaazaniasz, syn Maakatczyka, oni i ich ludzie.
24 Gedalia akafanya kiapo kwa watu wake na kuwaambia, “Msiwaogope Wakaldayo. Muishi katika nchi na kumtumikia mfalme wa Babeli, na itakuwa vema kwenu.”
Wtedy Gedaliasz przysiągł im i ich ludziom: Nie bójcie się służyć Chaldejczykom. Mieszkajcie w ziemi i służcie królowi Babilonu, a będzie wam dobrze.
25 Lakini ilitokea kwamba katika mwezi wa saba Ishmaeli mwana wa Nethania mwana wa Elishama, kutoka familia ya kifalme, wakaja na watu kumi na kumshambulia Gedalia. Gedalia akafa, pamoja na watu wa Yuda na Wababeli ambao walikuwa pamoja nae huko Mizpa.
Lecz w siódmym miesiącu przybył Izmael, syn Netaniasza, syna Eliszamy, z rodu królewskiego, a z nim dziesięciu ludzi, i pobili Gedaliasza, i umarł, a także Żydów i Chaldejczyków, którzy byli z nim w Mispie.
26 Kisha wale watu wote, kutoka chini kwenda juu, na maamiri wa jeshi, wakainuka na kwenda Misri, kwasababu walikuwa wanawaogopa Wababeli.
Wówczas cały lud, od najmniejszego do największego, oraz dowódcy wojsk powstali i poszli do Egiptu, bo się bali Chaldejczyków.
27 Ilitokea baadaye katika mwaka wa thelathini na saba wa utumwa wa Yekonia mfalme wa Yuda, katika mwezi wa kumi na mbili, siku ya ishirini na saba ya mwezi, Evil-merodaki mfalme wa Babeli akamtoa Yekonia mfalme wa Yuda kutoka gerezani. Hii ilitokea katika mwaka ambao Evil-Merodaki alipoanza kutawala.
A w trzydziestym siódmym roku uprowadzenia Joachina, króla Judy, dwunastego miesiąca dwudziestego siódmego [dnia] tego miesiąca, Ewil-Merodak, król Babilonu, w pierwszym roku jego panowania, ułaskawił Joachina, króla Judy, i [wypuścił go] z więzienia.
28 Akaongea naye kwa ukarimu na kumpatia kiti kizuri zaidi kuliko kile cha wafalme wengine ambao walikuwa pamoja naye Babeli.
Rozmawiał z nim łaskawie i wystawił jego tron ponad tron innych królów, którzy [byli] z nim w Babilonie.
29 Evil-Merodaki akamvua Yekonia nguo za gerezani,
Zdjął też jego szaty więzienne i jadł chleb zawsze w jego obecności przez wszystkie dni swego życia.
30 na Yekinia akala siku zote kwenye meza ya mfalme katika maisha yake yote yaliyokuwa yamebakia.
Codziennie otrzymywał od króla stałe utrzymanie, przez wszystkie dni swego życia.

< 2 Wafalme 25 >