< 2 Wafalme 11 >
1 Basi Athalia, mama yake na Ahazia, alipoona kwamba mtoto wake amekufa, aliinuka na kuwaua watoto wote wa kifalme.
Then Athaliah the mother of Ahaziah when she saw that her sonne was dead, she arose, and destroyed all the Kings seede.
2 Lakini Yehosheba, binti wa mfalme Yehoramu na dada wa Ahazia, akamchukua Yoashi mwana wa Ahazia, na kumficha mbali mwa miongoni mwa watoto wa mfalme waliokuwa wameuawa, wakati wote pamoja na mlezi wake; akawaweka kwenye chumba cha kulala. Wakamficha kutoka Athalia kwa hiyo hakuuawa.
But Iehosheba the daughter of King Ioram, and sister to Ahaziah tooke Ioash the sonne of Ahaziah, and stale him from among the Kings sonnes that shoulde be slaine, both him and his nource, keeping them in the bed chaber, and they hid him from Athaliah, so that he was not slaine.
3 Alikuwa pamoja na Yehosheba, wamejificha kwenye nyumba ya Yahwe, kwa mda wa miaka sita, wakati Athalia alipotawala juu ya nchi.
And he was with her hid in the house of the Lord sixe yeere: and Athaliah did reigne ouer the land.
4 Katika mwaka wa saba, Yehoyada alituma ujumbe na kuleta maamiri jeshi mamia wa Wakari na wa walinzi, na kuwaleta kwake mwenyewe, ndani ya nyumba ya Yahwe. Akafanya agano pamoja nao, na kuwaapisha kiapo katika nyumba ya Yahwe. Kisha akawaonyesha mtoto wa mfalme.
And the seuenth yeere Iehoiada sent and tooke the captaines ouer hundreths, with other captaines and them of the garde, and caused them to come vnto him into the house of the Lord, and made a couenant with them, and tooke an othe of them in the house of the Lord, and shewed them the Kings sonne.
5 Akawaamuru, akisema, “Hivi ndivyo mnavyotakiwa kufanya. Theluthi yenu mtakaokuja kwenye Sabato mtakuwa mkiiangalia nyumba ya mfalme,
And he commanded them, saying, This is it that ye must doe, The third part of you, that commeth on the Sabbath, shall warde towarde the Kings house:
6 na theluthi mtakuwa langoni mwa Suri, na theluthi langoni nyuma ya walinzi.”
And another third part in the gate of Sur: and another thirde part in the gate behinde them of the garde: and ye shall keepe watche in the house of Massah.
7 Makundi mengine mawili ambayo hayatumikii Sabato, Mtayalinda juu ya nyumba ya Yahwe kwa ajili ya mfalme.
And two parts of you, that is, all that goe out on the Sabbath day, shall keepe the watch of the house of the Lord about the King.
8 Ni lazima mumzunguke mfalme, kila mmoja na silaha zake kwenye mkono wake. Yeyote aingiaye ndani ya safu, auwawe. Lazima mkae pamoja na mfalme kila atokapo na kila aingiapo.
And ye shall compasse the King rounde about, euery man with his weapon in his hande, and whosoeuer commeth within the ranges, let him be slayne: be you with the King, as he goeth out and in.
9 Hivyo mamia ya maamri jeshi wakatii kila kitu Yehoyada kuhani alichokiamuru. Kila mmoja akachukua watu wake, wale ambao walitakiwa kuja kutumika siku ya hiyo Sabato, na wale ambao wataacha kuitumika kwenye hiyo Sabato; ndipo wakaja kwa Yehoyada kuhani.
And the captaines of the hundreths did according to all that Iehoiada the Priest commaded, and they tooke euery man his men that entred in to their charge on the Sabbath with them that went out of it on the Sabbath, and came to Iehoiada the Priest.
10 Kisha Yehoyada yule kuhani akawapa mikuki na ngao mamia wa maamri jeshi ambayo ilikuwa mali ya mfalme Daudi ambayo ilikuwa kwenye nyumba ya Yahwe.
And the Priest gaue to the captaines of hundreths the speares and the shieldes that were King Dauids, and were in the house of the Lord.
11 Basi walinzi wakasimama, kila mtu na silaha kwenye mkono wake, kutoka upande wa kuume wa hekalu, kwenda upande wa kushoto, karibu na madhabahu ya hekelu, wakimzunguka mfalme.
And the garde stoode, euery man with his weapon in his hande, from the right side of the house to the left side, about the altar and about the house, round about the King.
12 Kisha Yehoyada akamleta nje mtoto wa mfalme Yoashi, na kumvalisha taji la kifalme, na kumpatia mikataba ya agano. Kisha wakamfanya mfalme na kummiminia mafuta. Wakapiga makofi wakisema, “Mfalme na aishi!”
Then he brought out the Kings sonne, and put the crowne vpon him and gaue him the Testimonie, and they made him King: also they anoynted him, and clapt their handes, and sayde, God saue the King.
13 Wakati Athalia aliposikia sauti za walinzi na za watu, alikuja kwa wale watu kwenye nyumba ya Yahwe.
And when Athaliah heard the noyse of the running of the people, shee came in to the people in the house of the Lord.
14 Akatazama, na, kisha, yule mfalme alikuwa amesimama kwenye nguzo, kama ilivyokuwa desturi, na manahodha na wapiga mabaragumu walikuwa karibu na mfalme. Watu wote wa nchi hiyo walikuwa wakifurahi na kupiga matarumbeta. Kisha Athalia akachana mavazi yake kwa hasira na kupiga kelele, “Uhaini! Uhaini!”
And when shee looked, beholde, the King stoode by a pillar, as the maner was, and the princes and the trumpetters by the King, and al the people of the land reioyced, and blew with trumpets. Then Athaliah rent her clothes, and cryed, Treason, treason.
15 Ndipo Yehoyada yule kuhani akawaagiza maamri jeshi wa mamia ambao waliokuwa juu ya jeshi, akisema, “Mtoeni kwenye safu.” Atakayemfuata, muueni kwa upanga.” Kwa kuwa kuhani alisema, “Msimwache auawe kwenye nyumba ya Yahwe.”
But Iehoiada the Priest commanded the captaines of the hundreths that had the rule of the hoste, and sayde vnto them, Haue her forth of the ranges, and he that followeth her, let him die by the sworde: for the Priest had sayd, Let her not be slaine in the house of the Lord.
16 Hivyo wakamtwaa kadiri walivyokuwa wakiikaribia hiyo sehemu iliyokuwa na farasi wakaingia chini, na akauawa huko.
Then they laid hands on her, and she went by the way, by the which the horses goe to the house of the King, and there was she slaine.
17 Kisha Yehoyada akafanya agano kati ya Yahwe na mfalme na watu, ambao wangekuwa watu wa Yahwe, na pia kati ya mfalme na watu.
And Iehoiada made a couenant betweene the Lord, and the King and the people, that they should be the Lordes people: likewise betweene the King and the people.
18 Basi watu wote wa nchi wakaenda kwenye nyumba ya Baali na kuingusha chini. Wakaangusha madhabahu ya Baali na sanamu zake wakazivunja vipande vipande, na kumuua Matani, mfalme wa Baali, mbele ya haya madhabahu. Kisha Yehoyada kuhani akawachagua walinzi juu ya hekalu la Yahwe.
Then all the people of the lande went into the house of Baal, and destroyed it with his altars, and his images brake they downe courageously, and slewe Mattan the Priest of Baal before the altars: and the Priest set a garde ouer the house of the Lord.
19 Yehoyada akawachukua maamiri jeshi wa mamia, Wakari, walinzi, na watu wote wa nchi, na kwa pamoja wakamleta chini mfalme kutoka kwenye nyumba ya Yahwe na wakaenda kwenye nyumba ya mfalme, wakaingia kwa njia ya lango la walinzi. Yoashi akachukua nafasi yake kwenye kiti cha enzi cha mfalme.
Then he tooke the captaines of hudreths, and the other captaines, and the garde, and all the people of the lande: and they brought the King from the house of the Lord, and came by the way of the gate of the garde to the Kings house: and he sate him downe on the throne of the Kings.
20 Hivyo watu wote wa nchi wakamsifu, na nchi ilikuwa kimya baada ya Athalia kuuawa kwa upanga kwenye nyumba ya mfalme.
And all the people of the land reioyced, and the citie was in quiet: for they had slaine Athaliah with the sworde beside the Kings house.
21 Yoashi alikuwa na umri wa miaka saba tangu alipoanza kutawala.
Seuen yeere olde was Iehoash when he began to reigne.