< 1 Nyakati 7 >

1 Isiakari alikuwa na wana wanne Tola, Pua, Yashubi, na Shimironi.
Et les enfants d'Issacar, furent ces quatre Tolah, Puah, Jasub et Simron.
2 Wana wa Tola walikuwa Uzi, Refaia, Yerie, Yamai, Ibisami, Shemueli. Walikua vichwa katika nyumba za baba yao, toka uzao wa Tola na waliorodheshwa kama mashujaa hodari miongoni mwa kizazi chao. Katika siku za Daudi walikua na idadi ya 22, 600.
Et les enfants de Tolah furent Huzi, Réphaja, Jériel, Jahmaï, Jibsam, et Samuël; chefs des maisons de leurs pères qui étaient de Tolah; gens forts et vaillants en leurs générations. Le compte qui en fut fait aux jours de David fut de vingt-deux mille six cents.
3 Mwana wa Uzi alikua Izrahia. Mwana wake alikua Michaeli, Obadia, Yoeli, na Ishia, wote watano walikua viongozi wa ukoo
Les enfants de Huzi, Jizrahia; et les enfants de Jizrahia, Micaël, Hobadia, Joël, et Jiscija, en tout cinq chefs.
4 Pamoja nao walikua na jeshi la watu elfu thelathini na sita kwa mapambano, Kwa mujibu wa orodha zilizomilikiwa na koo za mababu zao, kwa kuwa walikuwa na wake wengi pamoja na wana.
Et avec eux, suivant leurs générations, et selon les familles de leurs pères, [il y eut] en troupes de gens de guerre trente-six mille hommes; car ils eurent plusieurs femmes et plusieurs enfants.
5 Kaka zao, kabila la Isakari, walikua na wanaume wa vita themanini na saba, kwa mujibu wa orodha zilizomilikiwa na koo za mababu zao.
Et leurs frères selon toutes les familles d'Issacar, hommes forts et vaillants, étant comptés tous selon leur généalogie, furent quatre-vingt et sept mille.
6 Wana watatu wa Benjamini walikuwa Bela, Beka, na Yediaeli.
[Les enfants] de Benjamin furent trois, Bélah, Béker, et Jédihaël.
7 Wana watano wa Bela walikuwa Ezibono, Uzi, Uzieli, Yerimoti, na Iri. Walikua ni wanajeshi na waanzilishi wa koo. Watu wao walikuwa na idadi ya wanaume wa vita 22, 034, kwa mujibu wa orodha zilizomilikiwa na koo za mababu zao.
Et les enfants de Bélah furent, Etsbon, Huzi, Huziël, Jérimoth, et Hiri; cinq chefs des familles des pères, hommes forts et vaillants; et leur dénombrement selon leur généalogie monta à vingt-deux mille et trente-quatre.
8 Wana wa Beka walikuwa Zemira, Yoashi, Elieza, Elionai, Omri, Yeremoti, Abiya, Anatoti, na Alemeti. Wote hawa walikuwa wana wake.
Et les enfants de Béker [furent], Zemira, Joas, Elihézer, Eliohenaï, Homri, Jérimoth, Abija, Hanathoth, et Halemeth; tous ceux-là furent enfants de Béker.
9 Orodha ya koo zao ilikua na idadi ya 20, 200 viongozi wa familia na wanaume wa vita.
Et leur dénombrement selon leur généalogie, selon leurs générations, [et] les chefs des familles de leurs pères, monta à vingt mille deux cents hommes, forts et vaillants.
10 Mwana wa Yediaeli alikuwa Bilhani. Wana wa Bilhani walikuwa Yeushi, Benjamini, Ehudi, Kenaana, Zetani, Tarishishi, na Ahishahari.
Et Jédihaël eut pour fils Bilhan. Et les enfants de Bilhan furent, Jéhus, Benjamin, Ehud, Kénahana, Zethan, Tarsis, et Ahisahar.
11 Wote hawa waikuwa wana wa Yediaeli. Waliorodheshwa katika ukoo orodha ilikuwa 17, 200 viongozi na wanaume wa vita imara kwa kazi ya jeshi.
Tous ceux-là furent enfants de Jédihaël, selon les chefs [des familles] des pères, forts et vaillants, dix-sept mille deux cents hommes, marchant en bataille.
12 (Shupimu na Hupimu walikuwa wana wa Iri, na Hushimu alikuwa mwana wa Aheri.)
Suppim et Huppim furent enfants de Hir; et Husim fut fils d'Aher.
13 Wana wa Naftali walikuwa Yazieli, Guni, Yezeri, na Shalumu. Hawa walikuwa wajukuu wa Bilhahi.
Les enfants de Nephthali furent Jahtsiël, Guni, Jetser, et Sallum, [petits-] fils de Bilha.
14 Manasse alikua na mtoto wa kiume aliitwa Asrieli, Ambaye suria wake wa Kiaramia alimzalia. Pia alimzaa na Makiri, baba wa Gileadi.
Les enfants de Manassé, Asriël, que [la femme de Galaad] enfanta. Or la concubine Syrienne de Manassé avait enfanté Makir père de Galaad.
15 Makiri alimchukua mke wake kutoka Hupite na Shupite. Jina la dada yake lilikuwa Maaka. Mwingine wa uzao wa Manasse alikuwa Zalofehadi, ambaye alikuwa na mabinti pekee.
Et Makir prit une femme de la parenté de Huppim et de Suppim; car ils avaient une sœur nommée Mahaca. Et le nom d'un des petits-fils de Galaad fut Tselophcad; et Tselophcad n'eut que des filles.
16 Maaka mke wa Makiri, alimzaa mwana na alimuita Pereshi. Kaka yake aliitwa Shereshi, na wana wake walikuwa Ulamu na Rakemu.
Et Mahaca, femme de Makir, enfanta un fils et l'appela Pérés, et le nom de son frère Serés, dont les enfants furent, Ulam et Rékem.
17 Mwana wa Ulami alikuwa Bedani. Hawa walikuwa uzao wa Gileadi mwana wa Makiri mwana wa Manase.
Et le fils d'Ulam fut Bedan. Ce sont là les enfants de Galaad, fils de Makir, fils de Manassé.
18 Dada wa Gileadi Hamoleketi alimzaa Ishihodi, Abi Ezeri, na Mahila.
Mais sa sœur Moleketh enfanta Ishud, Abihézer, et Mahla.
19 Wana wa Shemida walikuwa Ahiana, Shekemu, Liki, na Aniamu.
Et les enfants de Semidah furent, Ahiam, Sekem, Likhi, et Aniham.
20 Uzao wa Efraimu ulikuwa kama ifuatavyo: Efraimu mwana wa Shutela. Shutela mwana wa Beredi. Beredi mwana wa Tahati.
Or les enfants d'Ephraïm furent, Sutelah; Béred son fils, Tahath son fils, Elhada son fils, Tahath son fils.
21 Tahati mwana wa Eleada. Eleada mwana wa Shutela. (Eza na Eleadi waliuawa na wanaume wa Gati, wenyeji wa nchi, walipoenda kuiba mifugo yao.
Zabad son fils, Sutelah son fils, et Hézer, et Elhad. Mais ceux de Gad, nés au pays, les mirent à mort, parce qu'ils étaient descendus pour prendre leur bétail.
22 Efraimu baba yao aliomboleza kwa siku nyingi, na kaka zake walikuja kumfariji.
Et Ephraïm leur père [en] mena deuil plusieurs jours; et ses frères vinrent pour le consoler.
23 Alilala na mkewe. Akapata mimba akamzaa mwana. Efraimu akamuita Beria, kwa sababu maafa yalishakuja nyumbani mwake.
Puis il vint vers sa femme, qui conçut, et enfanta un fils; et elle l'appela Bériha, parce qu'[il fut conçu] dans l'affliction arrivée en sa maison.
24 Binti yake alikuwa Sheera, ambaye alijenga miji juu na chini Beth Horon na Uzzen Sheerah.)
Et sa fille Séera, qui bâtit la basse et la haute Beth-horon, et Uzen-Séera.
25 Mwana wake alikuwa Rafa. Mwana wa Rafa alikuwa Reshefi. Mwana wa Reshafi alikuwa Tela. Mwana wa Tela alikuwa Tahani.
Son fils fut Repha, puis Reseph, et Telah son fils, Tahan son fils,
26 Mwana wa Tahani alikuwa Ladani. Mwana wa Ladani alikuwa Amihudi. Mwana wa Amihudi alikuwa Elishama.
Lahdan son fils, Hammihud son fils, Elisamah son fils,
27 Mwana wa Elishama alikuwa Nuni. Mwana wa Nuni alikuwa Joshua.
Nun son fils, Josué son fils.
28 Mali zao na makazi yao yalikuwa Betheli na yalizungukwa na vijiji. Waliongeza upande wa mashariki hadi Naarani na upande wa magharibi hadi Gezeri na vijiji vyake, na Shekemu na vijiji vyake hadi Aya na vijiji vyake.
Leur possession et habitation fut Béthel, avec les villes de son ressort, et du côté d'Orient, Naharan; et du côté d'Occident, Guézer, avec les villes de son ressort, et Sichem, avec les villes de son ressort, jusqu'à Haza, avec les villes de son ressort.
29 Katika mipaka pamoja na Manasse kulikuwa na Beti shani na vijiji vyake, Taanaki na vijiji vyake, Megido na vijiji vyake, na Dori na vijiji vyake. Katika huu mji waliishi uzao wa Josefu mwana wa Israeli.
Et dans les lieux qui étaient aux enfants de Manassé, Bethséan, avec les villes de son ressort, Tahanac, avec les villes de son ressort, Méguiddo, avec les villes de son ressort, Dor, avec les villes de son ressort. Les enfants de Joseph, fils d'Israël, habitèrent dans ces villes.
30 Wana wa Asha walikuwa Imna, Ishiva, Ishivi, na Beria. Sera alikuwa dada yao.
Les enfants d'Aser furent, Jimna, Jisua, Isaï, Bériha, et Sérah leur sœur.
31 Wana wa Beria walikuwa Heberi na Malchieli, Ambaye alikuwa baba wa Birzaiti.
Et les enfants de Bériha furent, Héber, et Malkiël, qui fut père de Birzavith.
32 Wana wa Heberi walikuwa Yafeti, Shomer, na Hotamu. dada yao alikuwa Shua.
Et Héber engendra Japhlet, Somer, Hotham, et Suah leur sœur.
33 Wana wa Yafeti walikuwa Pasach, Bimhali, na Ashivati. hawa walikuwa watoto wa yafeti.
Les enfants de Japhlet furent Pasah, Bimhal, et Hasvath. Ce sont là les enfants de Japhlet.
34 shoma, kaka wa Yafeti alikuwa na wana hawa: Roga, Yehuba, Aram.
Et les enfants de Semer furent Ahi, Rohega, Jéhubba, et Aram.
35 Kaka yake Shema, Helemu, alikuwa na wana hawa: Zofa, Imna, Sheleshi na Amali.
Et les enfants d'Hélem son frère furent, Tsophah, Jimnah, Sellés, et Hamal.
36 Wana wa Zofa walikuwa Sua, Harinefa, Shua, Beri, IMra,
Les enfants de Tsophah furent Suah, Harnepher, Suhal, Béri, Jimra,
37 Beza, Hodi, Shamma, Shilsha, Ithrani, na Beera.
Betser, Hod, Samma, Silsa, Jithran, et Béera.
38 Wana wa Yeta walikuwa Jefune, Pispa, na Ara.
Et les enfants de Jéther furent, Jephunné, Pispa, et Ara.
39 Wana wa Ulla walikwa Ara, Hannieli, na Rizia.
Et les enfants de Hulla furent, Arah, Hanniël, et Ritsia.
40 Hawa wote walikuwa uzao wa Asha. Walikua mababu wa ukoo, viongozi wa familia, wananume wa kipekee, wanaume wa vita, na machifu kati ya viongozi. Kulikuwa na wanaume elfu ishirini na sita walioorodheshwa waliokuwa imara kwa kazi ya jeshi, kwa mujibu wa idadi iliyo orodheshwa.
Tous ceux-là furent enfants d'Aser, chefs des maisons des pères, gens d'élite, forts et vaillants, chefs des principaux, et leur dénombrement selon leur généalogie, qui fut fait quand on s'assemblait pour aller à la guerre, fut de vingt-six mille hommes.

< 1 Nyakati 7 >