< Sefania 2 >

1 Kusanyikeni pamoja, kusanyikeni pamoja, enyi taifa lisilo na aibu,
Venez tous ensemble, réunissez-vous, nation indigne d’être aimée;
2 kabla ya wakati ulioamriwa haujafika na siku ile inayopeperusha kama makapi, kabla hasira kali ya Bwana haijaja juu yenu, kabla siku ya ghadhabu ya Bwana haijaja juu yenu.
Avant qu’un ordre enfante un jour comme la poussière qui passe, avant que vienne sur vous la colère de la fureur du Seigneur, avant que vienne sur vous le jour de l’indignation du Seigneur.
3 Mtafuteni Bwana, enyi nyote wanyenyekevu wa nchi, ninyi ambao hufanya lile analoamuru. Tafuteni haki, tafuteni unyenyekevu; labda mtahifadhiwa siku ya hasira ya Bwana.
Cherchez le Seigneur, vous tous humbles de la terre, qui avez exécuté ses jugements; cherchez la justice, cherchez la douceur; peut-être serez-vous à couvert au jour de la fureur du Seigneur.
4 Gaza utaachwa na Ashkeloni utaachwa magofu. Wakati wa adhuhuri Ashdodi utaachwa mtupu na Ekroni utangʼolewa.
Parce que Gaza a été détruite et Ascalon réduite en un désert; on chassera Azot, en plein midi, et Accaron sera déracinée.
5 Ole wenu ninyi ambao mnaishi kando ya bahari, enyi Wakerethi; neno la Bwana liko dhidi yenu, ee Kanaani, nchi ya Wafilisti. “Mimi nitawaangamiza, na hakuna atakayebaki.”
Malheur à vous qui habitez la région de la mer, nation d’hommes perdus: la parole du Seigneur a été prononcée contre vous, Chanaan, terre des Philistins, et je t’exterminerai, en sorte qu’il n’y ait pas en toi d’habitant.
6 Nchi kando ya bahari, mahali ambapo wanaishi Wakerethi, patakuwa mahali pa wachungaji na mazizi ya kondoo.
Et la région de la mer sera le lieu de repos des pasteurs, et le parc des troupeaux de menu bétail;
7 Itakuwa mali ya mabaki ya nyumba ya Yuda, hapo watapata malisho. Wakati wa jioni watajilaza chini katika nyumba za Ashkeloni. Bwana Mungu wao atawatunza, naye atawarudishia wafungwa wao.
Et cette région appartiendra à celui qui sera resté de la maison de Juda; là ils paîtront les troupeaux, dans les maisons d’Ascalon ils se reposeront le soir; parce que le Seigneur leur Dieu les visitera, et les ramènera de leur captivité.
8 “Nimeyasikia matukano ya Moabu nazo dhihaka za Waamoni, ambao waliwatukana watu wangu na kutoa vitisho dhidi ya nchi yao.
J’ai entendu les paroles outrageantes de Moab et les blasphèmes des fils d’Ammon, quand ils ont outragé mon peuple et l’ont bravé sur ses frontières.
9 Hakika, kama niishivyo,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, “hakika Moabu itakuwa kama Sodoma, Waamoni kama Gomora: mahali pa magugu na mashimo ya chumvi, nchi ya ukiwa milele. Mabaki ya watu wangu watawateka nyara; mabaki ya taifa langu watarithi nchi yao.”
À cause de cela, je vis, moi, dit le Seigneur des armées, le Dieu d’Israël, Moab sera comme Sodome, et les fils d’Ammon comme Gomorrhe; ils auront des épines sèches, et des morceaux de sel, et un désert pour toujours; les restes de mon peuple les pilleront, et ceux de ma nation qui auront survécu en seront les maîtres.
10 Hiki ndicho watarudishiwa kwa ajili ya kiburi chao, kwa kutukana na kudhihaki watu wa Bwana Mwenye Nguvu Zote.
Cela leur arrivera à cause de leur orgueil; parce qu’ils ont blasphémé, et ont bravé le peuple du Seigneur des armées.
11 Bwana atakuwa wa kuhofisha kwao atakapoangamiza miungu yote ya nchi. Mataifa katika kila pwani yatamwabudu, kila moja katika nchi yake.
Le Seigneur sera terrible contre eux, et il anéantira tous les dieux de la terre; et les hommes l’adoreront, chacun en son lieu, ainsi que toutes les îles des nations.
12 “Ninyi pia, ee Wakushi, mtauawa kwa upanga wangu.”
Mais vous aussi, Ethiopiens, vous serez tués par mon glaive.
13 Mungu atanyoosha mkono wake dhidi ya kaskazini na kuangamiza Waashuru, akiiacha Ninawi ukiwa na pakame kama jangwa.
Et il étendra sa main vers l’aquilon et perdra Assur; et il fera de la cité magnifique une solitude, et un lieu inaccessible, et comme un désert.
14 Makundi ya kondoo na ngʼombe yatajilaza pale, viumbe vya kila aina. Bundi wa jangwani na bundi waliao kwa sauti nyembamba wataishi juu ya nguzo zake. Mwangwi wa kuita kwao utapita madirishani, kifusi kitakuwa milangoni, boriti za mierezi zitaachwa wazi.
Et se coucheront au milieu d’elle les troupeaux, et toutes les bêtes des nations; et l’onocrotale et le hérisson demeureront sur ses linteaux: la voix de l’oiseau chantant retentira sur la fenêtre; le corbeau croassera sur le linteau, parce que j’anéantirai sa force.
15 Huu ndio mji uliotukuka na kuishi kwa furaha wakijisikia salama. Ulisema moyoni mwako, “Mimi ndimi, na wala hapana mwingine ila mimi.” Jinsi gani umekuwa gofu, mahali pa kulala wanyama pori! Wote wanaopita kando yake wanauzomea na kutikisa mkono kwa dharau.
Voilà la cité glorieuse qui demeurait dans la confiance; qui disait en son cœur: Moi je suis, et hors moi il n’y en a plus d’autre; comment est-elle devenue un désert, un repaire de bête sauvage? Quiconque la traversera, sifflera et agitera sa main.

< Sefania 2 >