< Hagai 1 >

1 Katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario wa Uajemi, katika siku ya kwanza ya mwezi wa sita, neno la Bwana lilikuja kupitia kwa nabii Hagai kwenda kwa Zerubabeli mwana wa Shealtieli, mtawala wa Yuda na kwa Yoshua mwana wa kuhani mkuu Yehosadaki:
En la seconde année du roi Darius, au sixième mois, au premier jour du mois, la parole du Seigneur fut adressée, par l’entremise d’Aggée, le prophète, à Zorobabel, chef de Juda, fils de Salathiel, et à Jésus, le grand-prêtre, fils de Josédec, disant:
2 Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Hawa watu husema, ‘Wakati haujawadia wa kujenga nyumba ya Bwana.’”
Voici ce que dit le Seigneur des armées: Ce peuple dit: Il n’est pas encore venu, le temps de bâtir la maison du Seigneur.
3 Kisha neno la Bwana likaja kupitia kwa nabii Hagai:
Et la parole du Seigneur fut adressée par l’entremise d’Aggée, le prophète, disant:
4 “Je, ni wakati wenu ninyi wa kuishi katika nyumba zenu zilizojengwa vizuri, wakati hii nyumba ikibaki, gofu?”
Est-ce qu’il est temps pour vous d’habiter dans des maisons lambrissées, quand cette maison est déserte?
5 Sasa hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Zitafakarini vyema njia zenu.
Et maintenant, voici ce que dit le Seigneur des armées: Appliquez vos cœurs à vos voies.
6 Mmepanda vingi, lakini mmevuna haba. Mnakula lakini hamshibi, mnakunywa, lakini hamtosheki. Mnavaa nguo, lakini hamsikii joto. Mnapata mishahara, lakini inatoweka kama imewekwa kwenye mfuko uliotobokatoboka.”
Vous avez semé beaucoup, et vous avez peu recueilli; vous avez mangé, et vous n’avez pas été rassasiés; vous avez bu, et vous n’avez pas été désaltérés; vous vous êtes couverts, et vous ne vous êtes pas réchauffés; et celui qui a accumulé des profits les a mis dans un sac percé.
7 Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Zitafakarini vyema njia zenu.
Voici ce que dit le Seigneur des armées: Appliquez vos cœurs à vos voies.
8 Pandeni milimani mkalete miti na kujenga nyumba, ili nipate kuifurahia, na nitukuzwe,” asema Bwana.
Montez sur la montagne, portez des bois, et bâtissez la maison, et elle me sera agréable, et je serai glorifié, dit le Seigneur.
9 “Mlitarajia mengi, kumbe, yametokea kidogo. Ulichokileta nyumbani nilikipeperusha. Kwa nini?” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Ni kwa sababu ya nyumba yangu, inayobaki katika hali ya magofu, wakati kila mmoja wenu anajishughulisha na nyumba yake mwenyewe.
Vous avez espéré plus, et il arrive moins; ce peu, vous l’ avez apporté dans votre maison, et j’ai soufflé dessus; pour quel motif, dit le Seigneur des armées? parce que ma maison est déserte, et que chacun de vous se hâte pour la sienne.
10 Kwa hiyo, kwa sababu yenu mbingu zimezuia umande wake na ardhi mavuno yake.
C’est pour cela qu’au-dessus de vous il a été défendu aux cieux de donner de la rosée, et qu’à la terre il a été défendu de donner ses productions.
11 Niliita ukame mashambani na milimani, kwenye nafaka, mvinyo mpya, mafuta pamoja na chochote kinachozalishwa na ardhi, juu ya watu na ngʼombe, pamoja na kazi za mikono yenu.”
Et j’ai appelé la sécheresse sur la terre, et sur les montagnes, et sur le blé, et sur le vin, et sur l’huile, et sur tout ce que produit la terre, et sur les hommes, et sur les bêtes, et sur tous les travaux de vos mains.
12 Kisha Zerubabeli mwana wa Shealtieli, Yoshua kuhani mkuu mwana wa Yehosadaki, pamoja na mabaki yote ya watu wakaitii sauti ya Bwana Mungu wao pamoja na ujumbe wa nabii Hagai, kwa sababu alikuwa ametumwa na Bwana Mungu wao. Watu walimwogopa Bwana.
Et Zorobabel, fils de Salathiel, et Jésus, fus de Josédec, le grand-prêtre, et tous ceux qui étaient restés du peuple, entendirent la voix du Seigneur leur Dieu, et les paroles d’Aggée, le prophète, qu’envoya vers eux le Seigneur leur Dieu; et le peuple fut saisi de crainte devant la face du Seigneur.
13 Kisha Hagai, mjumbe wa Bwana, akawapa watu ujumbe huu wa Bwana: “Mimi niko pamoja nanyi,” asema Bwana.
Et Aggée, envoyé du Seigneur dans les messages du Seigneur, parla, disant au peuple: Moi, je suis avec vous, dit le Seigneur.
14 Kwa hiyo Bwana akachochea roho ya Zerubabeli mwana wa Shealtieli, mtawala wa Yuda, na roho ya kuhani mkuu Yoshua mwana wa Yehosadaki, pamoja na roho za mabaki yote ya watu. Walikuja wakaanza kufanya kazi katika nyumba ya Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wao,
Et le Seigneur suscita l’esprit de Zorobabel, fils de Salathiel, chef de Juda, et l’esprit de Jésus, fils de Josédec, le grand prêtre, et l’esprit de tous ceux qui étaient restés du peuple, et ils entrèrent dans le temple, et ils travaillaient dans la maison du Seigneur des armées leur Dieu.
15 katika siku ya ishirini na nne mwezi wa sita, katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario.
Au vingt-quatrième jour, au sixième mois, en la seconde année du roi Darius;

< Hagai 1 >