< Tito 3 >
1 Wakumbushe watu kuwanyenyekea watawala na kuwatii wenye mamlaka, wawe tayari kutenda kila lililo jema.
Remind them to submit to the governments, authorities, to obey the rule over them, to be ready unto every good work,
2 Wasimnenee mtu yeyote mabaya, wasiwe wagomvi, bali wawe wapole, wakionyesha unyenyekevu kwa watu wote.
to speak evil of no one, that they should be peaceable, gentle, showing all meekness to all men.
3 Maana sisi wenyewe wakati fulani tulikuwa wajinga, wasiotii, tukiwa watumwa wa tamaa mbaya na anasa za kila aina. Tuliishi katika uovu na wivu, tukichukiwa na kuchukiana sisi kwa sisi.
For when we also were without understanding, being disobedient, deceived, serving divers lusts and pleasures, living in sin and envy, hateful, hating one another;
4 Lakini wema na upendo wa Mungu Mwokozi wetu ulipofunuliwa,
but when the goodness and philanthropy of God our Saviour appeared,
5 alituokoa, si kwa sababu ya matendo ya haki tuliyotenda, bali kwa sababu ya rehema zake. Alituokoa kwa kutuosha kwa kuzaliwa mara ya pili na kwa kufanywa wapya kwa njia ya Roho Mtakatifu,
not from works which are in righteousness, which we did, but according to his own mercy he saved us, by the washing of regeneration, and the renewal of the Holy Ghost,
6 ambaye Mungu alitumiminia kwa wingi kwa njia ya Yesu Kristo Mwokozi wetu,
whom he poured out on us richly, through Jesus Christ our Saviour;
7 ili kwamba, tukiisha kuhesabiwa haki kwa neema yake, tupate kuwa warithi tukiwa na tumaini la uzima wa milele. (aiōnios )
in order that, being justified by his faith, we may be made heirs according to the hope of eternal life. (aiōnios )
8 Hili ni neno la kuaminiwa. Nami nataka uyasisitize mambo haya, ili wale ambao wamemwamini Mungu wapate kuwa waangalifu kujitoa kwa ajili ya kutenda mema wakati wote. Mambo haya ni mazuri tena ya manufaa kwa kila mtu.
The word is faithful, and I wish you to be established concerning these things, in order that those having believed in God may think to excel in good works. These things are beautiful and useful to the people:
9 Lakini jiepushe na maswali ya kipuzi, mambo ya koo, mabishano na ugomvi kuhusu sheria, kwa sababu hayana faida, tena ni ubatili.
but reject foolish questions, and genealogies, and strife, and controversies about law; for they are unprofitable and vain.
10 Mtu anayesababisha mafarakano, mwonye mara ya kwanza, kisha mwonye mara ya pili. Baada ya hapo, usihusike naye tena.
Reject a heretical man after the first and second admonition;
11 Kwa kuwa unajua kwamba mtu kama huyo amepotoka na tena ni mwenye dhambi. Yeye amejihukumu mwenyewe.
knowing that such an one is turned away, and is sinning, being self-condemned.
12 Mara nitakapomtuma Artema au Tikiko kwako, jitahidi kuja unione huko Nikopoli, kwa sababu nimeamua kukaa huko wakati wa majira ya baridi.
When I shall send Artemas or Tychicus to you, hasten to come to me at Nicopolis: for I have determined to spend the winter there.
13 Fanya kila uwezalo uwasafirishe Zena yule mwanasheria na Apolo na uhakikishe kwamba wana kila kitu wanachohitaji katika safari yao.
Send on Zenas the lawyer and Apollos speedily, in order that nothing may be lacking to them.
14 Watu wetu hawana budi kujifunza kutenda mema, ili waweze kuyakimu mahitaji ya kila siku, wasije wakaishi maisha yasiyokuwa na matunda.
And let our people indeed learn to excel in good works for necessary uses, in order that they may not be unfruitful.
15 Wote walio pamoja nami wanakusalimu. Wasalimu wale wanaotupenda katika imani. Neema iwe nanyi nyote. Amen.
All who are with me salute you. Salute those who love us with the love of friendship in the faith. Grace be with you all.