< Warumi 2 >
1 Kwa hiyo huna udhuru wowote, wewe utoaye hukumu kwa mwingine, kwa maana katika jambo lolote unalowahukumu wengine, unajihukumu wewe mwenyewe kwa sababu wewe unayehukumu unafanya mambo hayo hayo.
Therefore you are without excuse, you person, you who judge, for what you judge in another you condemn in yourself. For you who judge practice the same things.
2 Basi tunajua kwamba hukumu ya Mungu dhidi ya wale wafanyao mambo kama hayo ni ya kweli.
But we know that God's judgment is according to truth when it falls on those who practice such things.
3 Hivyo wewe mwanadamu, utoapo hukumu juu yao na bado unafanya mambo yale yale, unadhani utaepuka hukumu ya Mungu?
But consider this, you person, you who judge those who practice such things although you do the same things. Will you escape from the judgment of God?
4 Au waudharau wingi wa wema, ustahimili na uvumilivu wake, bila kujua kuwa wema wa Mungu wakuelekeza kwenye toba?
Or do you think so little of the riches of his goodness, his delayed punishment, and his patience? Do you not know that his goodness is meant to lead you to repentance?
5 Lakini kwa sababu ya ukaidi wenu na mioyo yenu isiyotaka kutubu, mnajiwekea akiba ya ghadhabu dhidi yenu wenyewe kwa siku ile ya ghadhabu ya Mungu, wakati hukumu yake ya haki itakapodhihirishwa.
But it is to the extent of your hardness and unrepentant heart that you are storing up for yourself wrath on the day of wrath, that is, the day of the revelation of God's righteous judgment.
6 Kwa maana Mungu atamlipa kila mtu sawasawa na matendo yake.
He will pay back to every person according to his actions:
7 Wale ambao kwa kuvumilia katika kutenda mema hutafuta utukufu, heshima na maisha yasiyoharibika, Mungu atawapa uzima wa milele. (aiōnios )
to those who according to consistent, good actions have sought praise, honor, and incorruptibility, he will give eternal life. (aiōnios )
8 Lakini kwa wale watafutao mambo yao wenyewe na wale wanaokataa kweli na kuzifuata njia mbaya, kutakuwa na ghadhabu na hasira ya Mungu.
But to those who are self-seeking, who disobey the truth but obey unrighteousness, wrath and fierce anger will come.
9 Kutakuwa na taabu na dhiki kwa kila mmoja atendaye maovu, Myahudi kwanza na mtu wa Mataifa pia,
God will bring tribulation and distress on every human soul that has practiced evil, to the Jew first, and also to the Greek.
10 bali utukufu, heshima na amani kwa ajili ya kila mmoja atendaye mema, kwa Myahudi kwanza, kisha kwa mtu wa Mataifa.
But praise, honor, and peace will come to everyone who practices good, to the Jew first, and also to the Greek.
11 Kwa maana Mungu hana upendeleo.
For there is no favoritism with God.
12 Watu wote waliotenda dhambi pasipo sheria wataangamia pasipo sheria, nao wote wale waliotenda dhambi chini ya sheria watahukumiwa kwa sheria.
For as many as have sinned without the law will also perish without the law, and as many as have sinned with respect to the law will be judged by the law.
13 Kwa maana si wale wanaoisikia sheria ambao ni wenye haki mbele za Mungu, bali ni wale wanaoitii sheria ndio watakaohesabiwa haki.
For it is not the hearers of the law who are righteous before God, but it is the doers of the law who will be justified.
14 (Naam, wakati wa watu wa Mataifa, ambao hawana sheria, wanapofanya kwa asili mambo yatakiwayo na sheria, wao ni sheria kwa nafsi zao wenyewe, hata ingawa hawana sheria.
For when Gentiles, who do not have the law, do by nature the things of the law, they are a law to themselves, although they do not have the law.
15 Wao wanaonyesha kwamba lile linalotakiwa na sheria limeandikwa kwenye mioyo yao, ambayo pia dhamiri zao zikiwashuhudia, nayo mawazo yao yenye kupingana yatawashtaki au kuwatetea.)
By this they show that the actions required by the law are written in their hearts. Their conscience also bears witness to them, and their own thoughts either accuse or defend them to themselves
16 Hili litatukia siku hiyo Mungu atakapozihukumu siri za wanadamu kwa njia ya Yesu Kristo, kama isemavyo Injili yangu.
and also to God. That will happen on the day when God will judge the secrets of all people, according to my gospel, through Jesus Christ.
17 Tazama, wewe ukiwa unaitwa Myahudi na kuitegemea sheria na kujisifia uhusiano wako na Mungu,
But if you call yourself a Jew and rest upon the law and boast in God,
18 kama unajua mapenzi ya Mungu na kukubali lililo bora kwa sababu umefundishwa na hiyo sheria,
and know his will and approve of what is excellent because you have been instructed from the law;
19 kama unatambua kuwa wewe ni kiongozi wa vipofu, na mwanga kwa wale walio gizani,
and if you are convinced that you yourself are a guide to the blind, a light to those who are in darkness,
20 mkufunzi wa wajinga na mwalimu wa watoto wachanga, kwa kuwa una maarifa ya kweli katika hiyo sheria,
a corrector of the foolish, a teacher of little children, and that you have in the law the form of knowledge and of the truth, then how does this affect the way you live your life?
21 basi wewe, uwafundishaye wengine, mbona hujifunzi mwenyewe? Wewe uhubiriye kwamba mtu asiibe, wewe mwenyewe waiba?
You who teach others, do you not teach yourself? You who preach against stealing, do you steal?
22 Wewe usemaye mtu asizini, wewe mwenyewe wazini? Wewe uchukiaye miungu ya sanamu, wafanya jambo la kumchukiza katika mahekalu?
You who say that one must not commit adultery, do you commit adultery? You who hate idols, do you rob temples?
23 Wewe ujivuniaye sheria, wamwaibisha Mungu kwa kuvunja sheria?
You who boast in the law, do you dishonor God by breaking the law?
24 Kama ilivyoandikwa, “Kwa ajili yenu ninyi, Jina la Mungu linatukanwa miongoni mwa watu wa Mataifa.”
For “the name of God is blasphemed among the Gentiles because of you,” just as it has been written.
25 Kutahiriwa kuna thamani ikiwa unatii sheria, lakini kama unavunja sheria, kutahiriwa kwako kumekuwa kutokutahiriwa.
For circumcision indeed benefits you if you obey the law, but if you break the law, your circumcision becomes uncircumcision.
26 Hivyo, ikiwa wale wasiotahiriwa wanatimiza mambo ambayo sheria inataka, je, kutokutahiriwa kwao hakutahesabiwa kuwa sawa na kutahiriwa?
If, then, the uncircumcised person keeps the requirements of the law, will not his uncircumcision be considered as circumcision?
27 Ndipo wale ambao hawakutahiriwa kimwili lakini wanaitii sheria watawahukumu ninyi, ambao ingawa mmetahiriwa na kuijua sana sheria ya Mungu iliyoandikwa, lakini mwaivunja.
And will not the one who is naturally uncircumcised condemn you if he keeps the law? This is because you have the written law and circumcision, yet you break the law!
28 Kwa maana mtu si Myahudi kwa vile alivyo kwa nje, wala tohara ya kweli si kitu cha nje au cha kimwili.
For he is not a Jew who is merely one outwardly; neither is circumcision that which is merely outward in the flesh.
29 Lakini mtu ni Myahudi alivyo ndani, nayo tohara ya kweli ni jambo la moyoni, ni la Roho, wala si la sheria iliyoandikwa. Mtu wa namna hiyo hapokei sifa kutoka kwa wanadamu bali kwa Mungu.
But he is a Jew who is one inwardly, and circumcision is that of the heart, in the Spirit, not in the letter. The praise of such a person comes not from people but from God.