< Luka 12 >

1 Wakati huo, umati mkubwa wa watu maelfu, walipokuwa wamekusanyika hata wakawa wanakanyagana, Yesu akaanza kuzungumza kwanza na wanafunzi wake, akawaambia: “Jihadharini na chachu ya Mafarisayo, yaani, unafiki wao.
In the meantime, when many thousands of the people were gathered together, so much that they trampled on each other, he began to say to his disciples first of all, “Beware of the yeast of the Pharisees, which is hypocrisy.
2 Hakuna jambo lolote lililositirika ambalo halitafunuliwa, au lililofichwa ambalo halitajulikana.
But there is nothing concealed that will not be revealed, and nothing hidden that will not be known.
3 Kwa hiyo, lolote mlilosema gizani litasikiwa nuruni. Na kile mlichonongʼona masikioni mkiwa kwenye vyumba vya ndani, kitatangazwa juu ya paa.
So whatever you have said in the darkness will be heard in the light, and what you have spoken in the ear in the inner rooms will be proclaimed upon the housetops.
4 “Nawaambieni rafiki zangu, msiwaogope wale wauao mwili, lakini baada ya hilo hawawezi kufanya lolote zaidi.
I say to you my friends, do not be afraid of those who kill the body, and after that they have no more that they can do.
5 Lakini nitawaambia nani wa kumwogopa: Mwogopeni yule ambaye baada ya kuua mwili, ana mamlaka ya kuwatupa motoni. Naam, nawaambia, mwogopeni huyo! (Geenna g1067)
But I will warn you about whom to fear. Fear the one who, after he has killed, has authority to throw you into hell. Yes, I say to you, fear him. (Geenna g1067)
6 Mnajua kwamba shomoro watano huuzwa kwa senti mbili? Lakini Mungu hamsahau hata mmoja wao.
Are not five sparrows sold for two small coins? Yet not one of them is forgotten in the sight of God.
7 Naam, hata nywele za vichwa vyenu zote zimehesabiwa. Hivyo msiogope, kwa maana ninyi ni wa thamani kubwa kuliko shomoro wengi.
But even the hairs of your head are all numbered. Do not fear. You are more valuable than many sparrows.
8 “Ninawaambia kwamba yeyote atakayenikiri mbele ya watu, Mwana wa Adamu naye atamkiri mbele za malaika wa Mungu.
I say to you, everyone who confesses me before men, the Son of Man will also confess before the angels of God,
9 Lakini yeye atakayenikana mimi mbele ya watu, Mwana wa Adamu naye atamkana mbele ya malaika wa Mungu.
but he who denies me before men will be denied before the angels of God.
10 Naye kila atakayenena neno baya dhidi ya Mwana wa Adamu atasamehewa, lakini yeyote atakayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa.
Everyone who speaks a word against the Son of Man, it will be forgiven him, but to him who blasphemes against the Holy Spirit, it will not be forgiven.
11 “Watakapowapeleka katika masinagogi, na mbele ya watawala na wenye mamlaka, msiwe na wasiwasi kuhusu namna mtakavyojitetea au mtakavyosema.
When they bring you before the synagogues, the rulers, and the authorities, do not worry about how you will speak in your defense, or what you will say,
12 Kwa maana Roho Mtakatifu atawafundisha wakati huo huo mnachopaswa kusema.”
for the Holy Spirit will teach you in that hour what you should say.”
13 Mtu mmoja katika umati wa watu akamwambia Yesu, “Mwalimu, mwambie ndugu yangu tugawane naye urithi wetu.”
Then someone from the crowd said to him, “Teacher, tell my brother to divide the inheritance with me.”
14 Lakini Yesu akamwambia, “Rafiki, ni nani aliyeniweka mimi kuwa hakimu wenu au msuluhishi juu yenu?”
Jesus said to him, “Man, who made me a judge or a mediator over you?”
15 Ndipo Yesu akawaambia, “Jihadharini! Jilindeni na aina zote za choyo. Kwa maana maisha ya mtu hayatokani na wingi wa mali alizo nazo.”
He said to them, “Watch that you keep yourselves from all greedy desires, because a person's life does not consist of the abundance of his possessions.”
16 Kisha akawaambia mfano huu: “Shamba la mtu mmoja tajiri lilizaa sana.
Then Jesus told them a parable, saying, “The field of a rich man yielded abundantly,
17 Akawaza moyoni mwake, ‘Nifanye nini? Sina mahali pa kuhifadhi mavuno yangu.’
and he reasoned with himself, saying, 'What will I do, because I do not have a place to store my crops?'
18 “Ndipo huyo tajiri akasema, ‘Nitafanya hivi: Nitabomoa ghala zangu za nafaka na kujenga nyingine kubwa zaidi na huko nitayahifadhi mavuno yangu yote na vitu vyangu.
He said, 'This is what I will do. I will pull down my barns and build bigger ones, and there I will store all of my grain and other goods.
19 Nami nitaiambia nafsi yangu, “Nafsi, unavyo vitu vingi vizuri ulivyojiwekea akiba kwa miaka mingi. Pumzika; kula, unywe, ufurahi.”’
I will say to my soul, “Soul, you have many goods stored up for many years. Rest easy, eat, drink, be merry.”'
20 “Lakini Mungu akamwambia, ‘Mpumbavu wewe! Usiku huu uhai wako unatakiwa. Sasa hivyo vitu ulivyojiwekea akiba vitakuwa vya nani?’
But God said to him, 'Foolish man, tonight your soul is required of you, and the things you have prepared, whose will they be?'
21 “Hivyo ndivyo ilivyo kwa wale wanaojiwekea mali lakini hawajitajirishi kwa Mungu.”
That is what someone is like who stores up treasure for himself and is not rich toward God.”
22 Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Kwa hiyo nawaambia, msisumbukie maisha yenu kwamba mtakula nini; au msumbukie miili yenu kwamba mtavaa nini.
Jesus said to his disciples, “Therefore I say to you, do not worry about your life, what you will eat—or about your body, what you will wear.
23 Maisha ni zaidi ya chakula, na mwili ni zaidi ya mavazi.
For life is more than food, and the body is more than clothes.
24 Fikirini ndege! Wao hawapandi wala hawavuni, hawana ghala wala popote pa kuhifadhi nafaka; lakini Mungu huwalisha. Ninyi ni wa thamani zaidi kuliko ndege!
Consider the ravens, that they do not sow or reap. They have no storeroom or barn, but God feeds them. How much more valuable you are than the birds!
25 Ni nani miongoni mwenu ambaye kwa kujitaabisha kwake anaweza kujiongezea hata saa moja zaidi katika maisha yake?
Which of you by being anxious can add a cubit to his lifespan?
26 Kama hamwezi kufanya jambo dogo kama hilo, kwa nini basi kuyasumbukia hayo mengine?
If then you are not able to do such a very little thing, why do you worry about the rest?
27 “Angalieni maua jinsi yameavyo: Hayafanyi kazi wala hayafumi. Lakini nawaambia, hata Solomoni katika fahari yake yote hakuvikwa vizuri kama mojawapo ya hayo maua.
Consider the lilies—how they grow. They do not labor, neither do they spin. Yet I say to you, even Solomon in all his glory was not clothed like one of these.
28 Basi ikiwa Mungu huyavika hivi majani ya shambani, ambayo leo yapo, na kesho yanatupwa motoni, si atawavika ninyi vizuri zaidi, enyi wa imani haba!
If God so clothes the grass in the field, which exists today, and tomorrow is thrown into the oven, how much more will he clothe you, O you of little faith!
29 Wala msisumbuke mioyoni mwenu mtakula nini au mtakunywa nini. Msiwe na wasiwasi juu ya haya.
Do not look for what you will eat and what you will drink, and do not be anxious.
30 Watu wa mataifa ya duniani husumbuka sana kuhusu vitu hivi vyote, lakini Baba yenu anafahamu kuwa mnahitaji haya yote.
For all the nations of the world look for these things, and your Father knows that you need them.
31 Bali utafuteni Ufalme wa Mungu, na haya yote atawapa pia.
But seek his kingdom, and these things will be added to you.
32 “Msiogope enyi kundi dogo, kwa maana Baba yenu ameona vyema kuwapa ninyi Ufalme.
Do not fear, little flock, because your Father is very pleased to give you the kingdom.
33 Uzeni mali zenu mkawape maskini. Jifanyieni mifuko isiyochakaa, mkajiwekee hazina mbinguni isiyokwisha, mahali ambapo mwizi hakaribii wala nondo haharibu.
Sell your possessions and give to the poor. Make for yourselves purses which will not wear out—treasure in the heavens that does not run out, where no thief comes near, and no moth destroys.
34 Kwa sababu mahali hazina yako ilipo, hapo ndipo moyo wako utakapokuwa pia.
For where your treasure is, there your heart will be also.
35 “Kuweni tayari mkiwa mmevikwa kwa ajili ya huduma na taa zenu zikiwa zinawaka,
Let your long clothing be tucked in at your belt, and let your lamps be kept burning,
36 kama watumishi wanaomngojea bwana wao arudi kutoka kwenye karamu ya arusi, ili ajapo na kubisha mlango waweze kumfungulia mara.
and be like people looking for their master when he returns from the marriage feast, so that when he comes and knocks, they may immediately open the door for him.
37 Heri wale watumishi ambao bwana wao atakapokuja atawakuta wakiwa wanakesha. Amin, nawaambia, atajifunga mkanda wake na kuwaketisha ili wale, naye atakuja na kuwahudumia.
Blessed are those servants whom the master will find watching when he comes. Truly I say to you, he will tuck in his long clothing at his belt, and have them sit down at the table, and he will come and serve them.
38 Itakuwa heri kwa watumwa hao ikiwa bwana wao atakapokuja atawakuta wamekesha hata kama atakuja mnamo usiku wa manane, au karibu na mapambazuko.
If the master comes in the second watch of the night, or if even in the third watch, and finds them ready, blessed are those servants.
39 Lakini fahamuni jambo hili: Kama mwenye nyumba angalijua saa mwizi atakuja, asingaliiacha nyumba yake kuvunjwa.
But understand this, that if the master of the house had known the hour the thief was coming he would not have let his house be broken into.
40 Ninyi nanyi hamna budi kuwa tayari, kwa sababu Mwana wa Adamu atakuja saa msiyotazamia.”
Be ready also, because you do not know the hour when the Son of Man comes.”
41 Ndipo Petro akamuuliza, “Bwana, mfano huu unatuambia sisi peke yetu au watu wote?”
Peter said, “Lord, are you telling this parable only to us, or also to everyone?”
42 Yesu akamjibu, “Ni yupi basi wakili mwaminifu na mwenye busara, ambaye bwana wake atamfanya msimamizi juu ya watumishi wake wote, ili awape watumishi wengine chakula chao wakati unaofaa?
The Lord said, “Who then is the faithful and wise manager whom his lord will set over his other servants to give them their portion of food at the right time?
43 Heri mtumishi yule ambaye bwana wake atakaporudi atamkuta akifanya hivyo.
Blessed is that servant whom his lord finds doing that when he comes.
44 Amin nawaambia, atamweka mtumishi huyo kuwa msimamizi wa mali yake yote.
Truly I say to you that he will set him over all his property.
45 Lakini kama yule mtumishi atasema moyoni mwake, ‘Bwana wangu anakawia kurudi,’ kisha akaanza kuwapiga wale watumishi wa kiume na wa kike, na kula na kunywa na kulewa.
But if that servant says in his heart, 'My lord delays his return,' and begins to beat the male and female servants, and to eat and drink, and to become drunk,
46 Basi bwana wa mtumishi huyo atakuja siku asiyodhani na saa asiyoijua. Atamkata vipande vipande na kumweka katika sehemu moja pamoja na wale wasioamini.
the lord of that servant will come in a day when he does not expect, and in an hour that he does not know, and will cut him in pieces and appoint a place for him with the unfaithful.
47 “Yule mtumishi anayefahamu vyema mapenzi ya bwana wake na asijiandae wala kufanya kama apendavyo bwana wake, atapigwa kwa mapigo mengi.
That servant, having known his lord's will, and not having prepared or done according to his will, will be beaten with many blows.
48 Lakini yeyote ambaye hakujua naye akafanya yale yastahiliyo kupigwa, atapigwa kidogo. Yeyote aliyepewa vitu vingi, atadaiwa vingi; na yeyote aliyekabidhiwa vingi, kwake vitatakiwa vingi.
But the one who did not know and did what deserved a beating, he will be beaten with a few blows. But everyone who has been given much, from them much will be required, and the one who has been entrusted with much, even more will be asked.
49 “Nimekuja kuleta moto duniani; laiti kama ungekuwa tayari umewashwa!
I came to cast fire upon the earth, and how I wish that it were already kindled.
50 Lakini ninao ubatizo ambao lazima nibatizwe, nayo dhiki yangu ni kuu mpaka ubatizo huo ukamilike!
But I have a baptism to be baptized with, and how I am distressed until it is completed!
51 Mnadhani nimekuja kuleta amani duniani? La, nawaambia sivyo, nimekuja kuleta mafarakano.
Do you think that I came to bring peace on the earth? No, I tell you, but rather division.
52 Kuanzia sasa, kutakuwa na watu watano katika nyumba moja, watatu dhidi ya wawili, na wawili dhidi ya watatu.
For from now on there will be five in one house divided—three people against two, and two people against three.
53 Watafarakana baba dhidi ya mwanawe na mwana dhidi ya babaye, mama dhidi ya bintiye na binti dhidi ya mamaye, naye mama mkwe dhidi ya mkwewe na mkwe dhidi ya mama mkwe wake.”
They will be divided, father against son, and son against father; mother against daughter, and daughter against mother; mother-in-law against her daughter-in-law, and daughter-in-law against mother-in-law.”
54 Pia Yesu akauambia ule umati wa watu, “Mwonapo wingu likitokea magharibi, mara mwasema, ‘Mvua itanyesha,’ nayo hunyesha.
Jesus was saying to the crowds also, “When you see a cloud rising in the west, immediately you say, 'A shower is coming,' and so it happens.
55 Nanyi mwonapo upepo wa kusini ukivuma, ninyi husema, ‘Kutakuwa na joto,’ na huwa hivyo.
When a south wind is blowing, you say, 'There will be a scorching heat,' and it happens.
56 Enyi wanafiki! Mnajua jinsi ya kutambua kuonekana kwa dunia na anga. Inakuwaje basi kwamba mnashindwa kutambua wakati huu wa sasa?
Hypocrites, you know how to interpret the appearance of the earth and the heavens, but how is it that you do not know how to interpret the present time?
57 “Kwa nini hamwamui wenyewe lililo haki?
Why do you not judge what is right for yourselves?
58 Uwapo njiani na mshtaki wako kwenda kwa hakimu, jitahidi kupatana naye mkiwa njiani. La sivyo, atakupeleka kwa hakimu, naye hakimu atakukabidhi kwa afisa, naye afisa atakutupa gerezani.
For when you go with your adversary before the magistrate, on the way make an effort to settle the matter with him so that he does not drag you to the judge, and so that the judge does not deliver you to the officer, and the officer does not throw you into prison.
59 Nakuambia, hautatoka humo hadi uwe umelipa senti ya mwisho.”
I say to you, you will never come out from there until you have paid the very last bit of money.”

< Luka 12 >