< Ufunuo 18 >

1 Baada ya haya nikaona malaika mwingine akishuka kutoka mbinguni, akiwa na mamlaka makuu na dunia ikamulikiwa na mngʼao wake.
Pärast seda ma nägin taevast alla tulevat veel üht inglit, kellel oli suur autoriteet, ja kogu maa lõi tema auhiilgusest särama.
2 Naye akalia kwa nguvu kwa sauti kubwa, akisema: “Umeanguka! Umeanguka Babeli Mkuu! Umekuwa makao ya mashetani na makazi ya kila pepo mchafu, makazi ya kila ndege na kila mnyama achukizaye.
Ta hüüdis võimsa häälega: „Langenud! Langenud on suur Paabel! Temast on saanud kurjade vaimude eluase, kõigi rüvedate vaimude lemmikpaik, kõigi rüvedate lindude lemmikpaik, kõigi rüvedate, vastikute loomade lemmikpaik.
3 Kwa maana mataifa yote yamekunywa mvinyo wa ghadhabu ya uasherati wake. Nao wafalme wa dunia wamefanya uzinzi nao, nao wafanyabiashara wa dunia wametajirika kutokana na wingi wa utajiri wake.”
Sest tema abielurikkumise veinist on joovastunud kõik rahvad; temaga on hooranud maailma kuningad ning maailma kaupmehed on rikastunud tema luksusest!“
4 Kisha nikasikia sauti nyingine kutoka mbinguni ikisema: “Tokeni katikati yake, enyi watu wangu, ili msije mkashiriki dhambi zake, ili msije mkapatwa na pigo lake lolote;
Ja ma kuulsin taevast veel üht häält, mis ütles: „Tulge temast välja, mu rahvas, et te ei saaks tema pattude osaliseks, ja et teid ei tabaks tema nuhtlused!
5 kwa kuwa dhambi zake zimelundikana hadi mbinguni, naye Mungu ameukumbuka uhalifu wake.
Sest tema patud on ulatunud taevani ning Jumalal on meeles tema ülekohtused teod.
6 Mtendee kama yeye alivyotenda; umlipe mara mbili kwa ajili ya yale aliyotenda. Katika kikombe chake mchanganyie mara mbili ya kile alichochanganya.
Tehke talle samamoodi, nagu tema on teinud, ning makske talle kahekordselt ta tegude eest. Valage talle kahekordne kogus tema enese karikast!
7 Mpatie mateso na huzuni nyingi sawa na utukufu na anasa alizojipatia. Kwa kuwa moyoni mwake hujivuna, akisema, ‘Mimi ninatawala kama malkia; mimi si mjane, wala sitaona huzuni kamwe.’
Nii palju kui tema on iseennast ülistanud ja toretsenud, niisama palju mõõtke temale piina ja leina! Sest ta ütleb oma südames: „Ma elan kuningannana, ma ei ole lesk ega pea iial nägema leina.“
8 Kwa hiyo mapigo yatampata kwa siku moja: mauti, maombolezo na njaa. Naye atateketezwa kwa moto, kwa maana Bwana Mungu amhukumuye ana nguvu.
Sellepärast tabavad teda ühel päeval karistused – surmatõbi ja lein ja nälg, ning ta põletatakse ära tulega, sest võimas on Issand Jumal, kes on mõistnud kohut tema üle.“
9 “Wafalme wa dunia waliozini naye na kushiriki anasa zake watakapoona moshi wa kuungua kwake, watamlilia na kumwombolezea.
Ja tema pärast nutavad ja halavad maailma kuningad, kes temaga on abielu rikkunud ja tema luksust nautinud, kui nad näevad tema põlemise suitsu.
10 Kwa hofu kubwa ya mateso yake, watasimama mbali na kulia na wakisema: “‘Ole! Ole, ee mji mkubwa, ee Babeli mji wenye nguvu! Hukumu yako imekuja katika saa moja!’
Hirmust tema piina ees seisavad nad kaugel ja hüüavad: „Oh häda, häda, suur linn, sa võimas Paabeli linn! Ühe tunniga on tulnud su kohtumõistmine!“
11 “Wafanyabiashara wa dunia watalia na kumwomboleza kwa sababu hakuna anunuaye bidhaa zao tena:
Ja maailma kaupmehed nutavad ja halavad tema pärast, sest enam ei osta keegi nende kaubalaste:
12 Bidhaa za dhahabu, za fedha, za vito vya thamani na vya lulu, kitani safi, nguo za rangi ya zambarau, hariri, nguo nyekundu, aina zote za miti ya udi, na vifaa vyote vya pembe za ndovu, vifaa vyote vya miti yenye thamani kuliko yote, shaba, chuma na marmar,
ei kulda, hõbedat, kalliskive ega pärleid; ei peenlinast, purpurit, siidi ega erepunast kangast; ei mingisugust lõhnapuitu, esemeid elevandiluust, tehtud väärispuidust, vasest, rauast või marmorist;
13 bidhaa za mdalasini, vikolezi, za uvumba, manemane, na uvumba wenye harufu nzuri, za divai, na mafuta ya zeituni, za unga mzuri na ngano; ngʼombe na kondoo; farasi na magari; na miili na roho za wanadamu.
ei kaneeli ega vürtsi, lõhnarohte, mürri ega viirukit, veini ega õli, peenjahu ega nisu; ei veiseid ega lambaid; hobuseid ega vankreid; orje ega inimhingi.
14 “Watasema, ‘Yale matunda ambayo roho yako iliyatamani yamekoma. Utajiri wako wote na fahari yako vimetoweka, wala haviwezi kupatikana tena kamwe!’
Nad ütlevad: „Viljad, mida te ihkasite, on teie juurest kadunud. Kogu teie luksus ja hiilgus on kadunud sootuks, ja seda ei leita enam.“
15 Wale wafanyabiashara waliotajirika kwa bidhaa hizo kutoka kwake watasimama mbali naye kwa hofu kubwa ya mateso yanayompata. Watalia na kuomboleza wakipiga kelele wakisema:
Nende asjade kaupmehed, kes said selle linna kaudu rikkaks, seisavad eemal hirmul tema piina pärast, nuttes ja halades.
16 “‘Ole! Ole, ee mji mkubwa, uliyekuwa umevikwa mavazi ya kitani safi, ya rangi ya zambarau na nyekundu, ukimetameta kwa dhahabu, vito vya thamani na lulu!
Nad ütlevad: „Häda, häda, suur linn, riietatud peenesse linasesse, purpurisse ja erepunasesse, ning ehitud kulla, kalliskivide ja pärlitega.
17 Katika muda wa saa moja utajiri wote mkubwa kama huu umeangamia!’ “Kila nahodha, na wote wasafirio kwa meli, na wote wapatao kipato chao kutokana na bahari, watasimama mbali.
Sest ühe tunniga on ära hävitatud nii suur rikkus!“Ja kõik laevaomanikud, kaptenid ja meremehed – kõik, kes merel elatist teenivad – seisid eemal
18 Watakapouona moshi wa kuungua kwake watalia wakisema, ‘Je, kulipata kuwako mji mkubwa kama huu?’
ja kisendasid, nähes ta põlemise suitsu: „Kas on kunagi olnud selle suure linna sarnast?“
19 Nao watajirushia mavumbi vichwani mwao, huku wakilia na kuomboleza, wakisema: “‘Ole! Ole, ee mji mkubwa, mji ambao wote wenye meli baharini walitajirika kupitia kwa mali zake! Katika saa moja tu ameangamizwa!
Ja nad raputasid endale põrmu pea peale ning kisendasid nuttes ja halades: „Häda, häda, suur linn, kus said tema jõukusest rikkaks kõik, kes omasid laevu merel. Üheainsa tunniga on ta hävitatud!“
20 Furahia kwa ajili yake, ee mbingu! Furahini watakatifu, mitume na manabii! Mungu amemhukumu kwa vile alivyowatendea ninyi.’”
Rõõmustage tema üle, taevas, ning Jumala rahvas ja apostlid ja prohvetid, sest ta sai Jumalalt sama kohtuotsuse, mille tema kord langetas teile.
21 Kisha malaika mmoja mwenye nguvu akainua jiwe kubwa kama la kusagia akalitupa baharini akisema: “Hivyo ndivyo mji mkubwa Babeli utakavyotupwa chini kwa nguvu wala hautaonekana tena.
Ja üks võimas ingel tõstis üles otsekui suure veskikivi ja heitis selle merre, hüüdes: „Nõnda järsult visatakse ära suur linn Paabel, ja teda ei leita iial enam!
22 Nyimbo za wapiga vinubi na waimbaji, wapiga filimbi na wapiga tarumbeta kamwe hazitasikika tena ndani yako. Ndani yako kamwe hataonekana tena fundi mwenye ujuzi wa aina yoyote. Wala sauti ya jiwe la kusagia kamwe haitasikika tena.
Kandlemängu ja laulu, flöödiviisi ja pasunahäält ei kuulda sinu sees enam. Ja ühtegi käsitöömeistrit ei leidu enam su sees; Ka veskimürinat ei kuulda enam sinu sees.
23 Mwanga wa taa hautaangaza ndani yako tena. Sauti ya bwana arusi na bibi arusi kamwe haitasikika ndani yako tena. Wafanyabiashara wako walikuwa watu maarufu wa dunia. Mataifa yote yalipotoshwa kwa uchawi wako.
Ja lambi valgust ei paista sinu sees enam. Ja pruudi ja peigmehe häält ei kuulda enam sinu sees. Sest sinu kaupmehed olid maa peal tähtsad isikud ja sinu nõidus eksitas kõiki rahvaid.
24 Ndani yake ilionekana damu ya manabii na ya watakatifu na wote waliouawa duniani.”
Jah, sinust on leitud prohvetite ja Jumala rahva verd ja kõikide verd, kes on tapetud maa peal!“

< Ufunuo 18 >