< Yuda 1 >

1 Yuda, mtumwa wa Yesu Kristo na nduguye Yakobo: Kwa wale walioitwa, wapendwa katika Mungu Baba na kuhifadhiwa salama ndani ya Yesu Kristo:
Juudaselt, Jeesuse Kristuse sulaselt ja Jaakobuse vennalt, Neile kutsutuile, kes on Jumalas Isas armastatud ja Jeesuses Kristuses hoitud:
2 Rehema, amani na upendo viwe kwenu kwa wingi.
Halastust ja rahu ja armastust olgu teil rohkesti!
3 Wapendwa, ingawa nilikuwa ninatamani sana kuwaandikia kuhusu wokovu ambao tunaushiriki sisi sote, niliona imenipasa kuwaandikia na kuwasihi kwamba mwitetee imani iliyokabidhiwa watakatifu kwa nafasi moja itoshayo.
Armsad, olles täis indu kirjutada teile meie ühisest päästest, leidsin vajalikuna kirjutada ja teid üles kutsuda võitlema usu eest, mis oli kord usaldatud Jumala pühale rahvale.
4 Kwa kuwa kuna watu waliojipenyeza kwa siri katikati yenu, watu walioandikiwa tangu zamani hukumu hii, waovu, wapotoshao neema ya Mungu wetu kuwa ufisadi wakimkana yeye aliye Bwana wetu wa pekee, Bwana Yesu Kristo.
Sest teie sekka on imbunud mõningad inimesed, kes juba ammu on kirja pandud kohtu jaoks. Need on jumalakartmatud inimesed, kes meie Jumala armu kõlvatuseks moonutades salgavad ära meie ainsa valitseja ja meie Issanda Jeesuse Kristuse.
5 Ingawa mmekwisha kujua haya yote, nataka niwakumbushe kuwa Bwana akiisha kuwaokoa watu wake kutoka nchi ya Misri, baadaye aliwaangamiza wale ambao hawakuamini.
Ja kuigi te seda kõike teate, tahan tuletada teile meelde, et Issand, kes rahva ühel korral päästis Egiptusest, hävitas teisel korral need, kes ei uskunud.
6 Nao malaika ambao hawakulinda nafasi zao, lakini wakayaacha makao yao, hawa amewaweka katika giza, wakiwa wamefungwa kwa minyororo ya milele kwa ajili ya hukumu Siku ile kuu. (aïdios g126)
Ja ingleid, kes ei hoidnud kinni oma kõrgest seisusest, vaid hülgasid oma eluaseme, on ta hoidnud pimeduses, seotuna igaveste ahelatega suure päeva kohtuks (aïdios g126)
7 Vivyo hivyo, Sodoma na Gomora na pia ile miji iliyokuwa kandokando, ambayo kwa jinsi moja na hao, walijifurahisha kwa uasherati na kufuata tamaa za mwili zisizo za asili, waliwekwa wawe mfano kwa kuadhibiwa katika moto wa milele. (aiōnios g166)
Nii nagu Soodom, Gomorra ja nende ümberkaudsed linnad, kes samal kombel hoorasid nagu need inglid ning ebaloomulikule ihale andusid, on hoiatavaks näiteks igavese tule karistusest. (aiōnios g166)
8 Vivyo hivyo, hawa waotao ndoto huutia mwili unajisi, hukataa kuwa chini ya mamlaka na kunena mabaya juu ya wenye mamlaka.
Aga samuti rüvetavad ka need unenägijad oma ihu, lükkavad tagasi taevase autoriteedi ja teotavad aukandjaid vaime.
9 Lakini hata malaika mkuu Mikaeli alipokuwa anashindana na ibilisi juu ya mwili wa Mose, hakuthubutu kumlaumu, bali alimwambia, “Bwana na akukemee!”
Ometi peaingel Miikaelgi, kui ta vaidles sõnasõjas kuradiga Moosese surnukeha pärast, ei julgenud lausuda teotavat otsust, vaid ütles: „Issand sõidelgu sind!“
10 Lakini watu hawa hunena mabaya dhidi ya mambo wasiyoyafahamu. Na katika mambo yale wanayoyafahamu kwa hisia kama wanyama wasio na akili, hayo ndiyo hasa yanayowaharibu.
Need aga teotavad kõike, millest nad midagi ei taipa, aga millest nad oma ihu tungide kaudu kui arutud loomad aru saavad, selles nad hävitavad end.
11 Ole wao! Kwa kuwa wanaifuata njia ya Kaini, wamekimbilia faida katika kosa la Balaamu na kuangamia katika uasi wa Kora.
Häda neile, sest nad on läinud Kaini teed ja tormanud tasu eest Bileami eksitusse, ja Korahi kombel vastu hakates on toonud endale hukatuse!
12 Watu hawa ni dosari katika karamu zenu za upendo, wakila pamoja nanyi bila hofu, wakijilisha pasipo hofu. Wao ni mawingu yasiyokuwa na maji, yakichukuliwa na upepo, miti isiyo na matunda wakati wa mapukutiko, ambayo hunyauka, iliyokufa mara mbili na kungʼolewa kabisa.
Nemad on teie armastussöömaaegadel häbiplekid, kes kartmatult teiega koos pidutsedes iseennast nuumavad. Nad on veeta pilved, mida tuul ringi kannab, viljatud sügispuud, kahekordselt surnud, juurtega üles kistud,
13 Wao ni mawimbi makali ya bahari, yakitoa povu la aibu yao wenyewe, ni nyota zipoteazo, ambao weusi wa giza ndio akiba waliowekewa milele. (aiōn g165)
metsikud merelained, mis vahutavad välja oma häbi, ekslevad tähed, kelle jaoks on määratud pilkane pimedus igaveseks ajaks. (aiōn g165)
14 Enoki, mtu wa saba kuanzia Adamu alitoa unabii kuhusu watu hawa, akisema: “Tazama, Bwana anakuja pamoja na maelfu kwa maelfu ya watakatifu wake,
Nendest on prohvetlikult kõnelenud Eenok, Aadama järglane seitsmendas sugupõlves: „Vaata, Issand tuleb mitmekümne tuhande pühaga
15 ili kumhukumu kila mmoja na kuwapatiliza wote wasiomcha Mungu kwa matendo yao yote ya uasi waliyoyatenda, pamoja na maneno yote ya kuchukiza ambayo wenye dhambi wamesema dhidi yake.”
pidama kohut kõigi üle ja karistama igaüht kõikide nende jumalakartmatute tegude eest, mida nad on teinud, ja kõikide ränkade sõnade eest, mida jumalakartmatud patused on tema vastu rääkinud.“
16 Watu hawa ni wenye kunungʼunika na wenye kutafuta makosa; wao hufuata tamaa zao mbaya, hujisifu kwa maneno makuu kuhusu wao wenyewe na kuwasifu mno watu wenye vyeo kwa ajili ya kujipatia faida.
Need on rahulolematud saatuse üle nurisejad, kes elavad oma himude järgi ja kelle suu räägib kiitlevaid sõnu, ja nad meelitavad inimesi omakasu pärast.
17 Lakini ninyi wapenzi, kumbukeni yale mitume wa Bwana Yesu Kristo waliyonena zamani.
Teie aga, armsad, pidage meeles, mida meie Issanda Jeesuse Kristuse apostlid ennustasid;
18 Kwa kuwa waliwaambia, “Siku za mwisho kutakuwa na watu wenye kudhihaki, watakaofuata tamaa zao wenyewe za upotovu.”
kui nad teile ütlesid: „Viimsel ajal tuleb pilkajaid, kes elavad oma jumalakartmatute himude järgi.“
19 Hawa ndio watu wanaowagawa ninyi, wafuatao tamaa zao za asili, wala hawana Roho.
Need on inimesed, kes tekitavad lõhenemisi, maised hinged, kellel ei ole Vaimu.
20 Lakini ninyi wapendwa, jijengeni katika imani yenu iliyo takatifu sana tena ombeni katika Roho Mtakatifu.
Teie aga, armsad, rajage endid oma kõige pühamale usule ja palvetage Pühas Vaimus,
21 Jilindeni katika upendo wa Mungu mkitazamia kwa furaha rehema ya Bwana wetu Yesu Kristo ili awalete katika uzima wa milele. (aiōnios g166)
ja hoidke endid nõnda Jumala armastuses ja oodake meie Issanda Jeesuse Kristuse halastust igaveseks eluks. (aiōnios g166)
22 Wahurumieni walio na mashaka;
Halastage nende peale, kes kahtlevad;
23 wengine waokoeni kwa kuwanyakua kutoka kwenye moto; nao wengine wahurumieni mkiwa na hofu, mkichukia hata vazi lenye mawaa na kutiwa unajisi na mwili.
päästke nad, tõmmake nad tulest välja; teiste peale halastage kartuses, vihates lihaliku loomuse poolt rüvetatud riideidki.
24 Kwake yeye awezaye kuwalinda ninyi msianguke na kuwaleta mbele za utukufu wake mkuu bila dosari na kwa furaha ipitayo kiasi:
Ent temale, kes suudab teid takistada komistamast ja asetada laitmatuna oma kirkuse palge ette ülevoolavas rõõmus,
25 kwake yeye Mungu pekee Mwokozi wetu, kwa Yesu Kristo Bwana wetu, utukufu, ukuu, uweza na mamlaka ni vyake tangu milele, sasa na hata milele! Amen. (aiōn g165)
ainsale Jumalale, meie Päästjale, Jeesuse Kristuse, meie Issanda läbi, olgu au, auhiilgus, võimus ja meelevald enne ajastuid, nüüd ja igavesti! Aamen. (aiōn g165)

< Yuda 1 >