< Ufunuo 13 >

1 Yule joka akajikita katika mchanga ulioko ufuoni mwa bahari. Nami nikamwona mnyama akitoka ndani ya bahari. Mnyama huyo alikuwa na pembe kumi na vichwa saba, akiwa na taji kumi kwenye hizo pembe zake, na juu ya kila kichwa kulikuwa na jina la kukufuru.
and he took his stand on the sea-shore. Then I saw, rising out of the sea, a wild Beast with ten horns and seven heads. On its horns were ten diadems, and on its heads were blasphemous names.
2 Mnyama yule niliyemwona alifanana na chui, lakini miguu yake ilikuwa kama ya dubu na kichwa chake kama cha simba. Lile joka likampa huyo mnyama nguvu zake, kiti chake cha enzi na mamlaka makubwa.
The Beast that I saw was like a leopard; but its feet were like a bear’s, and its mouth like the mouth of a lion. The Dragon gave it his power and his throne, and wide dominion.
3 Kimojawapo ya vichwa vya huyo mnyama kilikuwa kama kilichokwisha kupata jeraha la mauti, lakini jeraha hilo la mauti likapona. Ulimwengu wote ukashangaa ukamfuata huyo mnyama.
One of its heads seemed to me to have been mortally wounded, but its deadly wound had been healed. The whole earth followed the Beast, wondering;
4 Watu wakaliabudu lile joka kwa sababu lilikuwa limempa huyo mnyama mamlaka yake, pia wakamwabudu huyo mnyama na kuuliza, “Ni nani aliye kama huyu mnyama? Ni nani awezaye kupigana vita naye?”
and men worshiped the Dragon, because he had given his dominion to the Beast; while, as they worshiped the Beast, they said – “Who can compare with the Beast? And who can fight with it?”
5 Huyo mnyama akapewa kusema maneno ya kiburi na kukufuru na kutumia mamlaka yake kwa muda wa miezi arobaini na miwili.
The Beast was given a mouth that spoke proudly and blasphemously, and it was empowered to work its will for forty-two months.
6 Akafungua kinywa chake ili kumkufuru Mungu, akilitukana Jina lake na mahali aishipo na wale wakaao mbinguni.
It opened its mouth only to blaspheme God, to blaspheme his name and his tent – those who live in his tent in heaven.
7 Pia akaruhusiwa kufanya vita na watakatifu na kuwashinda. Akapewa uwezo juu ya watu wa kila kabila, jamaa, lugha na taifa.
It had been permitted to fight with Christ’s people and to conquer them, and it had received power over men of every tribe, and people, and language, and nation.
8 Nao watu wote waishio duniani watamwabudu huyo mnyama, yaani, wale wote ambao majina yao hayakuandikwa kwenye kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo aliyechinjwa tangu kuumbwa kwa ulimwengu.
All who are living on earth will worship it – all whose names have not been written in the Lamb’s book of life, the Lamb that has been sacrificed from the foundation of the world.
9 Yeye aliye na sikio na asikie.
Let those who have ears hear.
10 Ikiwa mtu ni wa kuchukuliwa mateka, atachukuliwa mateka. Ikiwa mtu ni wa kuuawa kwa upanga, atauawa kwa upanga. Hapa ndipo penye wito wa subira na imani ya watakatifu.
Whoever is destined for captivity goes into captivity. Whoever will kill with the sword must inevitably be killed with the sword. (Here there is need for endurance and faith on the part of Christ’s people.)
11 Kisha nikamwona mnyama mwingine, akipanda juu kutoka dunia. Alikuwa na pembe mbili kama mwana-kondoo, lakini akanena kama joka.
Then I saw, rising out of the earth, another wild Beast. It had two horns like those of a lamb, and its voice was like a dragon’s.
12 Akatumia mamlaka yote ya yule mnyama wa kwanza kwa niaba yake, naye akawafanya wote wakaao duniani kumwabudu yule mnyama wa kwanza, ambaye jeraha lake la mauti lilipona.
It exercises all the authority of the first Beast under its eyes; and it makes the earth and all who are living on it worship that first Beast, whose mortal wound was healed.
13 Naye akafanya ishara kuu na za ajabu, hata kusababisha moto kushuka toka mbinguni kuja duniani watu wakiona waziwazi.
It performs great marvels, even causing fire to fall from the heavens to the earth, before people’s eyes;
14 Kwa sababu ya zile ishara alizokuwa amepewa uwezo wa kuzifanya kwa niaba ya yule mnyama wa kwanza, akawadanganya wakaao duniani. Akawaamuru wasimamishe sanamu kwa heshima ya yule mnyama aliyekuwa amejeruhiwa kwa upanga lakini akaishi.
and in consequence of the marvels which it was allowed to perform under the eyes of the Beast, it is able to deceive all who are living on the earth. It tells those who live on the earth to make a statue in honour of the Beast, who, despite the wound from the sword, yet lived.
15 Akapewa uwezo wa kuipa pumzi ile sanamu ya yule mnyama wa kwanza, ili iweze kusema na kuwasababisha wale wote waliokataa kuiabudu hiyo sanamu kuuawa.
It was permitted to breathe life into the image of the Beast, so that the image of the Beast might speak; and it was also permitted to cause all who refused to worship the image of the Beast to be put to death.
16 Pia alimlazimisha kila mmoja, mdogo na mkubwa, tajiri na maskini, mtu huru na mtumwa, atiwe chapa kwenye mkono wake wa kuume au kwenye kipaji chake cha uso,
High and low, rich and poor, free and enslaved – it causes a brand to be put on the right hand or on the forehead of every one of them,
17 ili kwamba mtu yeyote asiweze kununua wala kuuza isipokuwa amekuwa na hiyo chapa, ambayo ni jina la huyo mnyama au tarakimu za jina lake.
so that no one is able to buy or sell, except those that bear this brand – either the name of the Beast or the number indicated by the letters of his name.
18 Hapa ndipo penye hekima. Yeye aliye na ufahamu na ahesabu tarakimu za huyo mnyama, kwa maana ni tarakimu za kibinadamu. Tarakimu zake ni 666.
(Here there is need for discernment.) The person with ability can compute the number of the Beast; for the number indicates a person’s name. Its number is six hundred and sixty-six.

< Ufunuo 13 >