< Yuda 1 >
1 Yuda, mtumwa wa Yesu Kristo na nduguye Yakobo: Kwa wale walioitwa, wapendwa katika Mungu Baba na kuhifadhiwa salama ndani ya Yesu Kristo:
To those who, having received the call, have been loved by God the Father and protected by Jesus Christ, From Jude, a servant of Jesus Christ, and the brother of James.
2 Rehema, amani na upendo viwe kwenu kwa wingi.
May mercy, peace, and love be yours in ever increasing measure.
3 Wapendwa, ingawa nilikuwa ninatamani sana kuwaandikia kuhusu wokovu ambao tunaushiriki sisi sote, niliona imenipasa kuwaandikia na kuwasihi kwamba mwitetee imani iliyokabidhiwa watakatifu kwa nafasi moja itoshayo.
Dear friends, while I was making every effort to write to you about our common salvation, I felt that I must write to you at once to encourage you to fight in defence of the faith that has once for all been entrusted to the keeping of Christ’s people.
4 Kwa kuwa kuna watu waliojipenyeza kwa siri katikati yenu, watu walioandikiwa tangu zamani hukumu hii, waovu, wapotoshao neema ya Mungu wetu kuwa ufisadi wakimkana yeye aliye Bwana wetu wa pekee, Bwana Yesu Kristo.
For there have crept in among you certain godless people, whose sentence has long since been pronounced, and who make the mercy of God an excuse for profligacy, and disown our only lord and master, Jesus Christ.
5 Ingawa mmekwisha kujua haya yote, nataka niwakumbushe kuwa Bwana akiisha kuwaokoa watu wake kutoka nchi ya Misri, baadaye aliwaangamiza wale ambao hawakuamini.
Now I want to remind you – but you already know it all – that, though the Lord delivered the people from Egypt, yet he afterwards destroyed those who refused to believe in him;
6 Nao malaika ambao hawakulinda nafasi zao, lakini wakayaacha makao yao, hawa amewaweka katika giza, wakiwa wamefungwa kwa minyororo ya milele kwa ajili ya hukumu Siku ile kuu. (aïdios )
and that even those angels, who did not keep to their appointed spheres, but left their proper homes, have been kept by him for the judgment of the great day in everlasting chains and black darkness. (aïdios )
7 Vivyo hivyo, Sodoma na Gomora na pia ile miji iliyokuwa kandokando, ambayo kwa jinsi moja na hao, walijifurahisha kwa uasherati na kufuata tamaa za mwili zisizo za asili, waliwekwa wawe mfano kwa kuadhibiwa katika moto wa milele. (aiōnios )
Like Sodom and Gomorrah and the towns near them, which gave themselves up to fornication, and fell into unnatural vice, these angels now stand out as a warning, undergoing, as they are, punishment in eternal fire. (aiōnios )
8 Vivyo hivyo, hawa waotao ndoto huutia mwili unajisi, hukataa kuwa chini ya mamlaka na kunena mabaya juu ya wenye mamlaka.
Yet in the same way these people, too, cherishing vain dreams, pollute our human nature, reject control, and malign the celestial beings.
9 Lakini hata malaika mkuu Mikaeli alipokuwa anashindana na ibilisi juu ya mwili wa Mose, hakuthubutu kumlaumu, bali alimwambia, “Bwana na akukemee!”
Yet even Michael, the archangel, when, in his dispute with the devil, he was arguing about the body of Moses, did not venture to charge him with maligning, but said merely “The Lord rebuke you!”
10 Lakini watu hawa hunena mabaya dhidi ya mambo wasiyoyafahamu. Na katika mambo yale wanayoyafahamu kwa hisia kama wanyama wasio na akili, hayo ndiyo hasa yanayowaharibu.
But these people malign whatever they do not understand; while they use such things as they know by instinct (like the animals that have no reason) for their own corruption.
11 Ole wao! Kwa kuwa wanaifuata njia ya Kaini, wamekimbilia faida katika kosa la Balaamu na kuangamia katika uasi wa Kora.
Alas for them! They walk in the steps of Cain; led astray by Balaam’s love of gain, they plunge into sin, and meet their ruin through rebellion like Korah.
12 Watu hawa ni dosari katika karamu zenu za upendo, wakila pamoja nanyi bila hofu, wakijilisha pasipo hofu. Wao ni mawingu yasiyokuwa na maji, yakichukuliwa na upepo, miti isiyo na matunda wakati wa mapukutiko, ambayo hunyauka, iliyokufa mara mbili na kungʼolewa kabisa.
These are the people who are blots on your “love-feasts,” when they feast together and provide without scruple for themselves alone. They are clouds without rain, driven before the winds; they are leafless trees without a vestige of fruit, dead through and through, torn up by the roots;
13 Wao ni mawimbi makali ya bahari, yakitoa povu la aibu yao wenyewe, ni nyota zipoteazo, ambao weusi wa giza ndio akiba waliowekewa milele. (aiōn )
they are wild sea waves, foaming with their own shame; they are “wandering stars,” for which the blackest darkness has been reserved for ever. (aiōn )
14 Enoki, mtu wa saba kuanzia Adamu alitoa unabii kuhusu watu hawa, akisema: “Tazama, Bwana anakuja pamoja na maelfu kwa maelfu ya watakatifu wake,
To these people, as to others, Enoch, the seventh in descent from Adam, declared – “See! The Lord has come with his hosts of holy ones around him,
15 ili kumhukumu kila mmoja na kuwapatiliza wote wasiomcha Mungu kwa matendo yao yote ya uasi waliyoyatenda, pamoja na maneno yote ya kuchukiza ambayo wenye dhambi wamesema dhidi yake.”
to execute judgment on all people, and to convict all godless people of all their godless acts, which in their ungodliness they have committed, and of all the harsh words which they have spoken against him, godless sinners that they are!”
16 Watu hawa ni wenye kunungʼunika na wenye kutafuta makosa; wao hufuata tamaa zao mbaya, hujisifu kwa maneno makuu kuhusu wao wenyewe na kuwasifu mno watu wenye vyeo kwa ajili ya kujipatia faida.
These people are always murmuring, and complaining of their lot; they follow where their passions lead them; they have arrogant words on their lips; and they flatter others for the sake of what they can get from them.
17 Lakini ninyi wapenzi, kumbukeni yale mitume wa Bwana Yesu Kristo waliyonena zamani.
But you should, dear friends, recall what was foretold by the apostles of our Lord Jesus Christ;
18 Kwa kuwa waliwaambia, “Siku za mwisho kutakuwa na watu wenye kudhihaki, watakaofuata tamaa zao wenyewe za upotovu.”
how they used to say to you – “As time draws to an end, there will be scoffers, who will be led by their godless passions.”
19 Hawa ndio watu wanaowagawa ninyi, wafuatao tamaa zao za asili, wala hawana Roho.
These are the people – animal and unspiritual – who cause divisions.
20 Lakini ninyi wapendwa, jijengeni katika imani yenu iliyo takatifu sana tena ombeni katika Roho Mtakatifu.
But you must, dear friends, build up your characters on the foundation of your most holy faith, pray under the guidance of the Holy Spirit,
21 Jilindeni katika upendo wa Mungu mkitazamia kwa furaha rehema ya Bwana wetu Yesu Kristo ili awalete katika uzima wa milele. (aiōnios )
and keep within the love of God, while waiting for the mercy of our Lord Jesus Christ, to bring you to eternal life. (aiōnios )
22 Wahurumieni walio na mashaka;
To some show pity, because they are in doubt. “Drag them out of the fire,” and save them.
23 wengine waokoeni kwa kuwanyakua kutoka kwenye moto; nao wengine wahurumieni mkiwa na hofu, mkichukia hata vazi lenye mawaa na kutiwa unajisi na mwili.
To others show pity, but with caution, hating the clothing polluted by their touch.
24 Kwake yeye awezaye kuwalinda ninyi msianguke na kuwaleta mbele za utukufu wake mkuu bila dosari na kwa furaha ipitayo kiasi:
To him who is able to guard you from falling, and to bring you into his glorious presence, blameless and rejoicing –
25 kwake yeye Mungu pekee Mwokozi wetu, kwa Yesu Kristo Bwana wetu, utukufu, ukuu, uweza na mamlaka ni vyake tangu milele, sasa na hata milele! Amen. (aiōn )
to the one God, our Saviour, be ascribed, through Jesus Christ, our Lord, glory, majesty, power, and dominion, as it was before time began, is now, and will be for all time to come. Amen. (aiōn )