< Ufunuo 11 >

1 Ndipo nikapewa mwanzi uliokuwa kama ufito wa kupimia, nikaambiwa, “Nenda ukapime hekalu la Mungu pamoja na madhabahu, nawe uwahesabu wale waabuduo humo.
Then a reed was given me to serve as a measuring rod; and a voice said, "Rise, and measure God's sanctuary--and the altar--and count the worshipers who are in it.
2 Lakini usiupime ua wa nje wa Hekalu, uache, kwa sababu ua huo wamepewa watu wa Mataifa. Hao wataukanyagakanyaga mji mtakatifu kwa muda wa miezi arobaini na miwili.
But as for the court which is outside the sanctuary, pass it over. Do not measure it; for it has been given to the Gentiles, and for forty-two months they will trample the holy city under foot.
3 Nami nitawapa mashahidi wangu wawili uwezo, nao watoe unabii kwa muda wa siku 1,260, wakiwa wamevaa nguo za gunia.”
And I will authorize My two witnesses to prophesy for 1,260 days, clothed in sackcloth.
4 Hawa ndio ile mizeituni miwili na vile vinara viwili vya taa visimamavyo mbele za Bwana Mungu wa dunia yote.
"These witnesses are the two olive-trees, and they are the two lamps which stand in the presence of the Lord of the earth.
5 Kama mtu yeyote akitaka kuwadhuru, moto hutoka vinywani mwao na kuwateketeza adui zao. Hivi ndivyo impasavyo kufa mtu yeyote atakayetaka kuwadhuru.
And if any one seeks to injure them--fire comes from their mouths and devours their enemies; and if any one seeks to injure them, he will in this way certainly be killed.
6 Watu hawa wanao uwezo wa kufunga anga ili mvua isinyeshe wakati wote watakapokuwa wanatoa unabii wao. Nao watakuwa na uwezo wa kuyabadili maji kuwa damu na kuipiga dunia kwa kila aina ya mapigo mara kwa mara kama watakavyo.
They have power given to them to seal up the sky, so that no rain may fall so long as they continue to prophesy; and power over the waters to turn them into blood, and to smite the earth with various plagues whenever they choose to do so.
7 Basi watakapokuwa wamemaliza ushuhuda wao, yule mnyama atokaye katika lile Shimo atapigana nao vita, atawashinda na kuwaua. (Abyssos g12)
"And when they have fully delivered their testimony, the Wild Beast which is to rise out of the bottomless pit will make war upon them and overcome them and kill them. (Abyssos g12)
8 Maiti zao zitabaki katika barabara ya mji mkubwa, ambao kwa fumbo unaitwa Sodoma na Misri, ambapo pia Bwana wao alisulubiwa.
And their dead bodies are to lie in the broad street of the great city which spiritually is designated 'Sodom' and 'Egypt,' where indeed their Lord was crucified.
9 Kwa muda wa siku tatu na nusu, watu wa kila kabila, jamaa, lugha na taifa wataziangalia hizo maiti zao na hawataruhusu wazikwe.
And men belonging to all peoples, tribes, languages and nations gaze at their dead bodies for three days and a half, but they refuse to let them be laid in a tomb.
10 Watu waishio duniani watazitazama kwa furaha maiti za hao manabii wawili na kushangilia kwa kupeana zawadi kwa sababu hao manabii waliwatesa watu waishio duniani.
The inhabitants of the earth rejoice over them and are glad and will send gifts to one another; for these two Prophets had greatly troubled the inhabitants of the earth."
11 Lakini baada ya zile siku tatu na nusu, pumzi ya uhai kutoka kwa Mungu ikawaingia, nao wakasimama kwa miguu yao na wote waliowaona wakaingiwa na hofu kuu.
But at the end of the three days and a half the breath of life from God entered into them, and they rose to their feet; and all who saw them were terrified.
12 Kisha wale manabii wawili wakasikia sauti kuu kutoka mbinguni ikiwaambia, “Njooni huku juu!” Nao wakapaa mbinguni katika wingu, wakati adui zao wakiwa wanawatazama.
Then they heard a loud voice calling to them out of Heaven, and bidding them come up; and they went up to Heaven in the cloud, and their enemies saw them go.
13 Saa iyo hiyo, kukatokea tetemeko kubwa la nchi na sehemu ya kumi ya mji ikaanguka. Watu elfu saba wakauawa katika tetemeko hilo, nao walionusurika wakaogopa sana, wakamtukuza Mungu wa mbinguni.
And just as that time there was a great earthquake, and a tenth part of the city was overthrown. 7,000 people were killed in the earthquake, and the rest were terrified and gave glory to the God of Heaven.
14 Ole ya pili imekwisha kupita, tazama ole ya tatu inakuja upesi.
The second Woe is past; the third Woe will soon be here.
15 Yule malaika wa saba akaipiga tarumbeta yake, pakawa na sauti kubwa mbinguni iliyosema: “Ufalme wa ulimwengu umekuwa ufalme wa Bwana wetu na wa Kristo wake, naye atatawala milele na milele.” (aiōn g165)
The seventh angel blew his trumpet; and there followed loud voices in Heaven which said, "The sovereignty of the world now belongs to our Lord and His Christ; and He will be King until the Ages of the Ages." (aiōn g165)
16 Nao wale wazee ishirini na wanne, waliokuwa wameketi mbele za Mungu, kwenye viti vyao vya enzi, wakaanguka kifudifudi, wakamwabudu Mungu,
Then the twenty-four Elders, who sit on thrones in the presence of God, fell on their faces and worshipped God,
17 wakisema: “Tunakushukuru, Bwana Mungu Mwenyezi, uliyeko na uliyekuwako, kwa kuwa umetwaa uweza wako mkuu na ukaanza kutawala.
saying, "We give thee thanks, O Lord God, the Ruler of all, Who art and wast, because Thou hast exerted Thy power, Thy great power, and hast become King.
18 Mataifa walikasirika nao wakati wa ghadhabu yako umewadia. Wakati umewadia wa kuwahukumu waliokufa na kuwapa thawabu watumishi wako manabii na watakatifu wako pamoja na wale wote wanaoliheshimu Jina lako, wakubwa kwa wadogo: na kuwaangamiza wale wanaoiangamiza dunia.”
The nations grew angry, and Thine anger has come, and the time for the dead to be judged, and the time for Thee to give their reward to Thy servants the Prophets and to Thy people, and to those who fear Thee, the small and the great, and to destroy those who destroy the earth."
19 Ndipo hekalu la Mungu lililoko mbinguni likafunguliwa, na sanduku la agano lake likaonekana humo ndani. Kukatokea mianga ya umeme wa radi, ngurumo, sauti za radi, tetemeko la nchi na mvua kubwa ya mawe.
Then the doors of God's sanctuary in Heaven were opened, and the Ark, in which His Covenant was, was seen in His sanctuary; and there came flashes of lightning, and voices, and peals of thunder, and an earthquake, and heavy hail.

< Ufunuo 11 >