< Ufunuo 10 >
1 Kisha nikamwona malaika mwingine mwenye nguvu akishuka kutoka mbinguni. Alikuwa amevikwa wingu na upinde wa mvua juu ya kichwa chake. Uso wake ulingʼaa kama jua na miguu yake ilikuwa kama nguzo za moto.
Then I saw another strong angel coming down from Heaven. He was robed in a cloud, and over his head was the rainbow. His face was like the sun, and his feet resembled pillars of fire.
2 Mkononi mwake alikuwa ameshika kijitabu kilichokuwa kimefunguliwa. Akauweka mguu wake wa kuume juu ya bahari na mguu wake wa kushoto akauweka juu ya nchi kavu.
In his hand he held a small scroll unrolled; and, planting his right foot on the sea and his left foot on the land,
3 Naye akapiga kelele kwa sauti kuu kama simba anayenguruma. Alipopiga kelele, zile radi saba zikatoa ngurumo zake.
he cried out in a loud voice which resembled the roar of a lion. And when he had cried out, each of the seven peals of thunder uttered its own message.
4 Nazo zile radi saba zilipotoa ngurumo, nilitaka kuanza kuandika, lakini nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, “Yatie muhuri hayo yaliyosemwa na hizo radi saba na usiyaandike.”
And when the seven peals of thunder had spoken, I was about to write down what they had said; but I heard a voice from Heaven which told me to keep secret all that the seven peals of thunder had said, and not write it down.
5 Kisha yule malaika niliyekuwa nimemwona akiwa amesimama juu ya bahari na juu ya nchi akainua mkono wake wa kuume kuelekea mbinguni.
Then the angel that I saw standing on the sea and on the land, lifted his right hand toward Heaven.
6 Naye akaapa kwa Yule aishiye milele na milele, aliyeumba mbingu na vyote vilivyomo, dunia na vyote viijazavyo, pamoja na bahari na vyote vilivyomo ndani yake, akasema, “Hakuna kungoja tena! (aiōn )
And in the name of Him who lives until the Ages of the Ages, the Creator of Heaven and all that is in it, of the earth and all that is in it, and of the sea and all that is in it, he solemnly declared, (aiōn )
7 Lakini katika siku zile ambazo huyo malaika wa saba atakapokaribia kuipiga hiyo tarumbeta yake, siri ya Mungu itatimizwa, kama vile alivyowatangazia watumishi wake manabii.”
"There shall be no further delay; but in the days when the seventh angel blows his trumpet--when he begins to do so--then the secret purposes of God are realized, in accordance with the good news which He gave to His servants the Prophets."
8 Ndipo ile sauti niliyokuwa nimeisikia kutoka mbinguni ikasema nami tena ikaniambia, “Nenda, chukua kile kitabu kilichofunguliwa kilichoko mkononi mwa yule malaika aliyesimama juu ya bahari na juu ya nchi kavu.”
Then the voice which I had heard speaking from Heaven once more addressed me. It said, "Go and take the little book which lies open in the hand of the angel who is standing on the sea and on the land."
9 Basi nikamwendea nikamwomba yule malaika anipe kile kitabu kidogo. Akaniambia, “Chukua na ukile. Kitakuwa kichungu tumboni mwako, lakini kinywani mwako kitakuwa kitamu kama asali.”
So I went to the angel and asked him to give me the little book. "Take it," he said, "and eat the whole of it. You will find it bitter when you have eaten it, although in your mouth it will taste as sweet as honey."
10 Hivyo nikakichukua kile kitabu kidogo kutoka mkononi mwa yule malaika nikakila. Kilikuwa kitamu kama asali kinywani mwangu, lakini baada ya kukila, tumbo langu likatiwa uchungu.
So I took the roll out of the angel's hand and ate the whole of it; and in my mouth it was as sweet as honey, but when I had eaten it I found it very bitter.
11 Kisha nikaambiwa, “Imekupasa kutoa unabii tena kuhusu makabila mengi, mataifa, lugha na wafalme.”
And a voice said to me, "You must prophesy yet further concerning peoples, nations, languages, and many kings."