< Ufunuo 10 >
1 Kisha nikamwona malaika mwingine mwenye nguvu akishuka kutoka mbinguni. Alikuwa amevikwa wingu na upinde wa mvua juu ya kichwa chake. Uso wake ulingʼaa kama jua na miguu yake ilikuwa kama nguzo za moto.
Kisha nikabhona malaika jhongi mbaha iselela pasi kuhoma kumbinguni. Ajhele akongibhu mu mabhengu, na kwajhele ni upinde bhwa fula panani pa mutu bhwa muene. Pamihu pa muene pajhele kama lijobha ni magolo gha muene ghajhele kama nguzo sya muoto.
2 Mkononi mwake alikuwa ameshika kijitabu kilichokuwa kimefunguliwa. Akauweka mguu wake wa kuume juu ya bahari na mguu wake wa kushoto akauweka juu ya nchi kavu.
Akamulili gombo lidebe mu kibhoko kya muene lya lyajhele lifunulibhu, ni muene abhekili kigolo kya muene kya kulia panani pa bahari ni kigolo kya muene kya kushoto panani pa ndema.
3 Naye akapiga kelele kwa sauti kuu kama simba anayenguruma. Alipopiga kelele, zile radi saba zikatoa ngurumo zake.
Kisha akwesili sauti jha panani kama simba paiunguruma, na wakati akwesili sauti radi saba syaunguruimi nikaburuma.
4 Nazo zile radi saba zilipotoa ngurumo, nilitaka kuanza kuandika, lakini nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, “Yatie muhuri hayo yaliyosemwa na hizo radi saba na usiyaandike.”
Wakati radi saba siburuimi nikaribileghe kulemba, lakini napeliki sauti kuhoma kumbinguni jhijobha, “Tunzayi jhijhelayi siri khela ambakyo radi saba sijobhili. Usijhilembi.”
5 Kisha yule malaika niliyekuwa nimemwona akiwa amesimama juu ya bahari na juu ya nchi akainua mkono wake wa kuume kuelekea mbinguni.
Kisha malaika jhanambwene ajhemili panani pa bahari ni pandema, ajhemili kibhoko kya muene panani kumbinguni
6 Naye akaapa kwa Yule aishiye milele na milele, aliyeumba mbingu na vyote vilivyomo, dunia na vyote viijazavyo, pamoja na bahari na vyote vilivyomo ndani yake, akasema, “Hakuna kungoja tena! (aiōn )
ni kulapa kwa jhola jhaiishi milele ni milele- jhaabhombili mbingu ni fyoha fya fijhele, padunia ni fyoha fyafijhele, ni bahari ni fyoha fyafijhele: “Kubetalepi kujha kuchelebhwa kabhele. (aiōn )
7 Lakini katika siku zile ambazo huyo malaika wa saba atakapokaribia kuipiga hiyo tarumbeta yake, siri ya Mungu itatimizwa, kama vile alivyowatangazia watumishi wake manabii.”
Lakini ligono lela, wakati malaika ghwa saba paibeta kukaribila kukhobha tarumbeta lya muene, ndipo siri jha K'yara jhibeta kujha jhitimisibhu, kama kya atangasili kwa bhatumishi bha muene manabii.”
8 Ndipo ile sauti niliyokuwa nimeisikia kutoka mbinguni ikasema nami tena ikaniambia, “Nenda, chukua kile kitabu kilichofunguliwa kilichoko mkononi mwa yule malaika aliyesimama juu ya bahari na juu ya nchi kavu.”
Sauti jha napeliki kuhoma kumbinguni jha nijobhili kabhele: “Lotayi, tolai gombo lidebe lyalifunulibhu ambalyo lijhele mu kibhoko kya malaika jhaajhemili panani pa bahari ni panani pa ndema.”
9 Basi nikamwendea nikamwomba yule malaika anipe kile kitabu kidogo. Akaniambia, “Chukua na ukile. Kitakuwa kichungu tumboni mwako, lakini kinywani mwako kitakuwa kitamu kama asali.”
Kisha nikalota kwa malaika ni kun'jobhela anipelai gombo lidebe. Anijobhili, “tolai ligombo na uliajhi. Libetakulikheta lileme lya jhobhi lijhelayi ni uchungu, lakini mu ndomo bhwa jhobhi libeta kujha linogha kama bhuokhi.”
10 Hivyo nikakichukua kile kitabu kidogo kutoka mkononi mwa yule malaika nikakila. Kilikuwa kitamu kama asali kinywani mwangu, lakini baada ya kukila, tumbo langu likatiwa uchungu.
Natolili gombo lidebe kuhoma mu mabhoko gha malaika ni kulya. Linogheghe kama bhuokhi mu ndomo bhwa nene, lakini baada jha kulya, lileme lya nene lyajhele ni uchungu.
11 Kisha nikaambiwa, “Imekupasa kutoa unabii tena kuhusu makabila mengi, mataifa, lugha na wafalme.”
Kisha baadhi jha sauti syanijobhili, “Usilondeka kutabiri kabhele kuhusu bhanu bhamehele, mataifa, lugha, ni bhafalme.”