< Zaburi 81 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya Asafu. Mwimbieni kwa furaha, Mungu aliye nguvu yetu; mpigieni kelele za shangwe Mungu wa Yakobo!
Au chef de musique. Sur Guitthith. D’Asaph. Chantez joyeusement à Dieu, notre force; poussez des cris de joie vers le Dieu de Jacob.
2 Anzeni wimbo, pigeni matari, pigeni kinubi na zeze kwa sauti nzuri.
Entonnez le cantique, et faites résonner le tambourin, la harpe agréable, avec le luth.
3 Pigeni baragumu za pembe za kondoo dume wakati wa Mwandamo wa Mwezi, na wakati wa mwezi mpevu, katika siku ya Sikukuu yetu;
Sonnez de la trompette à la nouvelle lune, au temps fixé, au jour de notre fête;
4 hii ni amri kwa Israeli, agizo la Mungu wa Yakobo.
Car c’est un statut pour Israël, une ordonnance du Dieu de Jacob:
5 Aliiweka iwe kama sheria kwa Yosefu alipotoka dhidi ya Misri, huko tulikosikia lugha ambayo hatukuielewa.
Il l’établit comme un témoignage en Joseph, lorsqu’il sortit à travers le pays d’Égypte, où j’entendis une langue que je ne connaissais pas.
6 Asema, “Nimeondoa mzigo mabegani mwao; mikono yao iliwekwa huru kutoka kwenye kikapu.
J’ai retiré son épaule de dessous le fardeau, ses mains ont été déchargées des corbeilles.
7 Katika shida yako uliniita nami nikakuokoa, nilikujibu katika mawingu yenye ngurumo; nilikujaribu katika maji ya Meriba.
Dans la détresse tu as crié, et je t’ai délivré; je t’ai répondu du lieu secret du tonnerre; je t’ai éprouvé auprès des eaux de Meriba. (Sélah)
8 “Enyi watu wangu, sikieni, nami nitawaonya: laiti kama mngenisikiliza, ee Israeli!
Écoute, mon peuple, et je témoignerai au milieu de toi; Israël, oh! si tu voulais m’écouter!
9 Hamtakuwa na mungu mgeni miongoni mwenu; msimsujudie mungu wa kigeni.
Il n’y aura point au milieu de toi de dieu étranger, et tu ne te prosterneras pas devant un dieu de l’étranger.
10 Mimi ni Bwana Mungu wako, niliyekutoa nchi ya Misri. Panua sana kinywa chako nami nitakijaza.
Moi, je suis l’Éternel, ton Dieu, qui t’ai fait monter du pays d’Égypte; ouvre ta bouche toute grande, et je la remplirai.
11 “Lakini watu wangu hawakutaka kunisikiliza; Israeli hakutaka kunitii.
Mais mon peuple n’a pas écouté ma voix, et Israël n’a pas voulu de moi.
12 Basi niliwaacha katika ukaidi wa mioyo yao wafuate mashauri yao wenyewe.
Alors je les ai abandonnés à l’obstination de leur cœur: ils ont marché selon leurs conseils.
13 “Laiti kama watu wangu wangalinisikiliza, kama Israeli wangalifuata njia zangu,
Oh! si mon peuple m’avait écouté! si Israël avait marché dans mes voies!
14 ningaliwatiisha adui zao kwa haraka, na kuugeuza mkono wangu dhidi ya watesi wao!
J’aurais bientôt subjugué leurs ennemis, et tourné ma main contre leurs adversaires.
15 Wale wanaomchukia Bwana wangalinyenyekea mbele zake, na adhabu yao ingedumu milele.
Ceux qui haïssent l’Éternel se seraient soumis à lui; et leur temps, à eux, aurait été à toujours;
16 Bali ninyi mngalilishwa ngano iliyo bora, na kuwatosheleza kwa asali itokayo kwenye mwamba.”
Et il les aurait nourris de la moelle du froment, et je t’aurais rassasié du miel du rocher.

< Zaburi 81 >