< Zaburi 81 >
1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya Asafu. Mwimbieni kwa furaha, Mungu aliye nguvu yetu; mpigieni kelele za shangwe Mungu wa Yakobo!
to/for to conduct upon [the] Gittith to/for Asaph to sing to/for God strength our to shout to/for God Jacob
2 Anzeni wimbo, pigeni matari, pigeni kinubi na zeze kwa sauti nzuri.
to lift: raise melody and to give: cry out tambourine lyre musical with harp
3 Pigeni baragumu za pembe za kondoo dume wakati wa Mwandamo wa Mwezi, na wakati wa mwezi mpevu, katika siku ya Sikukuu yetu;
to blow in/on/with month: new moon trumpet in/on/with full moon to/for day feast our
4 hii ni amri kwa Israeli, agizo la Mungu wa Yakobo.
for statute: decree to/for Israel he/she/it justice: judgement to/for God Jacob
5 Aliiweka iwe kama sheria kwa Yosefu alipotoka dhidi ya Misri, huko tulikosikia lugha ambayo hatukuielewa.
testimony in/on/with Joseph to set: make him in/on/with to come out: come he upon land: country/planet Egypt lip: language not to know to hear: hear
6 Asema, “Nimeondoa mzigo mabegani mwao; mikono yao iliwekwa huru kutoka kwenye kikapu.
to turn aside: remove from burden shoulder his palm his from pot to pass
7 Katika shida yako uliniita nami nikakuokoa, nilikujibu katika mawingu yenye ngurumo; nilikujaribu katika maji ya Meriba.
in/on/with distress to call: call to and to rescue you to answer you in/on/with secrecy thunder to test you upon water Meribah (Selah)
8 “Enyi watu wangu, sikieni, nami nitawaonya: laiti kama mngenisikiliza, ee Israeli!
to hear: hear people my and to testify in/on/with you Israel if to hear: hear to/for me
9 Hamtakuwa na mungu mgeni miongoni mwenu; msimsujudie mungu wa kigeni.
not to be in/on/with you god be a stranger and not to bow to/for god foreign
10 Mimi ni Bwana Mungu wako, niliyekutoa nchi ya Misri. Panua sana kinywa chako nami nitakijaza.
I LORD God your [the] to ascend: establish you from land: country/planet Egypt to enlarge lip your and to fill him
11 “Lakini watu wangu hawakutaka kunisikiliza; Israeli hakutaka kunitii.
and not to hear: hear people my to/for voice my and Israel not be willing to/for me
12 Basi niliwaacha katika ukaidi wa mioyo yao wafuate mashauri yao wenyewe.
and to send: let go him in/on/with stubbornness heart their to go: follow in/on/with counsel their
13 “Laiti kama watu wangu wangalinisikiliza, kama Israeli wangalifuata njia zangu,
if people my to hear: hear to/for me Israel in/on/with way: conduct my to go: walk
14 ningaliwatiisha adui zao kwa haraka, na kuugeuza mkono wangu dhidi ya watesi wao!
like/as little enemy their be humble and upon enemy their to return: turn back hand my
15 Wale wanaomchukia Bwana wangalinyenyekea mbele zake, na adhabu yao ingedumu milele.
to hate LORD to deceive to/for him and to be time their to/for forever: enduring
16 Bali ninyi mngalilishwa ngano iliyo bora, na kuwatosheleza kwa asali itokayo kwenye mwamba.”
and to eat him from fat wheat and from rock honey to satisfy you