< Zaburi 80 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Yungiyungi za Agano.” Zaburi ya Asafu. Ee Mchungaji wa Israeli tusikie, wewe umwongozaye Yosefu kama kundi; wewe uketiye katika kiti cha enzi katikati ya makerubi, angaza
to/for to conduct to(wards) lily testimony to/for Asaph melody to pasture Israel to listen [emph?] to lead like/as flock Joseph to dwell [the] cherub to shine [emph?]
2 mbele ya Efraimu, Benyamini na Manase. Uamshe nguvu zako, uje utuokoe.
to/for face: before Ephraim and Benjamin and Manasseh to rouse [emph?] [obj] might your and to go: come [emph?] to/for salvation to/for us
3 Ee Mungu, uturejeshe, utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
God to return: rescue us and to light face your and to save
4 Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, hata lini hasira yako itawaka na kufoka moshi dhidi ya maombi ya watu wako?
LORD God Hosts till how be angry in/on/with prayer people your
5 Umewalisha kwa mkate wa machozi, umewafanya wanywe machozi bakuli tele.
to eat them food: bread tears and to water: drink them in/on/with tears third
6 Tumekuwa chanzo cha ugomvi kwa jirani zetu, na adui zetu wanatudhihaki.
to set: make us strife to/for neighboring our and enemy our to mock to/for them
7 Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, nasi tuweze kuokolewa.
God Hosts to return: rescue us and to light face your and to save
8 Ulileta mzabibu kutoka Misri, ukawafukuza mataifa, ukaupanda.
vine from Egypt to set out to drive out: drive out nation and to plant her
9 Uliandaa shamba kwa ajili yake, mizizi ikawa imara, ukajaza nchi.
to turn to/for face: before her and to uproot root her and to fill land: country/planet
10 Milima ilifunikwa kwa kivuli chake, matawi yake yakafunika mierezi mikubwa.
to cover mountain: mount shadow her and branch her cedar God
11 Matawi yake yalienea mpaka Baharini, machipukizi yake mpaka kwenye Mto.
to send: depart foliage her till sea and to(wards) River shoot her
12 Mbona umebomoa kuta zake ili wote wapitao karibu wazichume zabibu zake?
to/for what? to break through wall her and to pluck her all to pass way: road
13 Nguruwe mwitu wanauharibu na wanyama wa kondeni hujilisha humo.
to tear off her swine from wood and creature field to pasture her
14 Turudie, Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote! Tazama chini kutoka mbinguni na uone! Linda mzabibu huu,
God Hosts to return: again please to look from heaven and to see: see and to reckon: visit vine this
15 mche ulioupanda kwa mkono wako wa kuume, mwana uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
and shoot which to plant right your and upon son: child to strengthen to/for you
16 Mzabibu wako umekatwa, umechomwa moto, unapowakemea, watu wako huangamia.
to burn in/on/with fire to cut from rebuke face your to perish
17 Mkono wako na utulie juu ya mtu aliyeko mkono wako wa kuume, mwana wa mtu uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
to be hand: power your upon man right your upon son: child man to strengthen to/for you
18 Ndipo hatutakuacha tena, utuhuishe, nasi tutaliitia jina lako.
and not to turn from you to live us and in/on/with name your to call: call to
19 Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
LORD God Hosts to return: rescue us to light face your and to save

< Zaburi 80 >