< Zaburi 7 >

1 Ombolezo la Daudi kwa Bwana kwa sababu ya Kushi, Mbenyamini. Ee Bwana, Mungu wangu, ninakukimbilia wewe, uniokoe na kunikomboa na wote wanaonifuatia,
مزمور داوود، که به سبب سخنان کوش بنیامینی برای خداوند سرایید. ای خداوند، خدای من، به تو پناه می‌آورم؛ مرا از دست تعقیب‌کنندگانم نجات ده،
2 la sivyo watanirarua kama simba na kunichana vipande vipande, asiwepo wa kuniokoa.
و گرنه آنها همچون شیر مرا می‌درند و تکه‌تکه می‌کنند بدون آنکه کسی بتواند به نجاتم بشتابد.
3 Ee Bwana, Mungu wangu, kama nimetenda haya na kuna hatia mikononi mwangu,
ای خداوند، خدای من، اگر به کسی ظلم کرده‌ام،
4 au ikiwa nimemtenda uovu aliye na amani nami, au nimemnyangʼanya adui yangu pasipo sababu,
اگر خوبی را با بدی تلافی نموده‌ام و یا به ناحق دشمن خود را غارت کرده‌ام،
5 basi adui anifuatie na kunipata, auponde uhai wangu ardhini na kunilaza mavumbini.
آنگاه بگذار دشمن مرا تعقیب نموده، به دام اندازد و زندگی‌ام را تباه سازد.
6 Amka kwa hasira yako, Ee Bwana, inuka dhidi ya ghadhabu ya adui zangu. Amka, Mungu wangu, uamue haki.
ای خداوند، برخیز و با غضبت در مقابل خشم دشمنانم بایست! ای خدای من، برخیز و عدالت را برقرار نما.
7 Kusanyiko la watu na likuzunguke. Watawale kutoka juu.
همهٔ قومها را نزد خود جمع کن و از بالا بر ایشان داوری فرما.
8 Bwana na awahukumu kabila za watu. Nihukumu Ee Bwana, kwa kadiri ya haki yangu, kwa kadiri ya uadilifu wangu, Ewe Uliye Juu Sana.
ای خداوند که داور همهٔ مردم هستی، پاکی و بی‌گناهی مرا ببین و حکم بده.
9 Ee Mungu mwenye haki, uchunguzaye mawazo na mioyo, komesha ghasia za waovu na ufanye wenye haki waishi kwa amani.
ای خدای عادل که از افکار و دلهای ما باخبری، بدیها را از بین ببر و نیکان را استوار ساز.
10 Ngao langu ni Mungu Aliye Juu Sana, awaokoaye wanyofu wa moyo.
خدا سپر من است و از من محافظت می‌کند. او کسانی را که دلشان پاک و راست است، نجات می‌بخشد.
11 Mungu ni mwamuzi mwenye haki, Mungu aghadhibikaye kila siku.
خدا داور عادل است. او هر روز بر بدکاران خشمگین می‌شود.
12 Kama hakutuhurumia, atanoa upanga wake, ataupinda na kuufunga uzi upinde wake.
اگر آنها به سوی خدا بازگشت نکنند، او شمشیرش را تیز خواهد کرد. خدا کمان خود را کشیده و آماده کرده است.
13 Ameandaa silaha zake kali, ameweka tayari mishale yake ya moto.
او سلاحهای مرگبار و تیرهای آتشین خود را به دست گرفته است.
14 Yeye aliye na mimba ya uovu na achukuaye mimba ya ghasia huzaa uongo.
وجود اشخاص گناهکار پر از شرارت و ظلم است و اعمالشان نادرست.
15 Yeye achimbaye shimo na kulifukua hutumbukia katika shimo alilochimba mwenyewe.
آنها برای دیگران چاه می‌کنند، اما خود در آن می‌افتند
16 Ghasia azianzishazo humrudia mwenyewe, ukatili wake humrudia kichwani.
و در دام بداندیشی و ظلم خود گرفتار می‌شوند.
17 Nitamshukuru Bwana kwa ajili ya haki yake, na nitaliimbia sifa jina la Bwana Aliye Juu Sana.
خداوند را به خاطر عدالتش می‌ستایم و در وصف او که متعال است می‌سرایم.

< Zaburi 7 >