< Zaburi 7 >
1 Ombolezo la Daudi kwa Bwana kwa sababu ya Kushi, Mbenyamini. Ee Bwana, Mungu wangu, ninakukimbilia wewe, uniokoe na kunikomboa na wote wanaonifuatia,
大卫指着便雅悯人古实的话,向耶和华唱的流离歌。 耶和华—我的 神啊,我投靠你! 求你救我脱离一切追赶我的人,将我救拔出来!
2 la sivyo watanirarua kama simba na kunichana vipande vipande, asiwepo wa kuniokoa.
恐怕他们像狮子撕裂我, 甚至撕碎,无人搭救。
3 Ee Bwana, Mungu wangu, kama nimetenda haya na kuna hatia mikononi mwangu,
耶和华—我的 神啊,我若行了这事, 若有罪孽在我手里,
4 au ikiwa nimemtenda uovu aliye na amani nami, au nimemnyangʼanya adui yangu pasipo sababu,
我若以恶报那与我交好的人— 连那无故与我为敌的,我也救了他,
5 basi adui anifuatie na kunipata, auponde uhai wangu ardhini na kunilaza mavumbini.
就任凭仇敌追赶我,直到追上, 将我的性命踏在地下, 使我的荣耀归于灰尘。 (细拉)
6 Amka kwa hasira yako, Ee Bwana, inuka dhidi ya ghadhabu ya adui zangu. Amka, Mungu wangu, uamue haki.
耶和华啊,求你在怒中起来, 挺身而立,抵挡我敌人的暴怒! 求你为我兴起!你已经命定施行审判!
7 Kusanyiko la watu na likuzunguke. Watawale kutoka juu.
愿众民的会环绕你! 愿你从其上归于高位!
8 Bwana na awahukumu kabila za watu. Nihukumu Ee Bwana, kwa kadiri ya haki yangu, kwa kadiri ya uadilifu wangu, Ewe Uliye Juu Sana.
耶和华向众民施行审判; 耶和华啊,求你按我的公义和我心中的纯正判断我。
9 Ee Mungu mwenye haki, uchunguzaye mawazo na mioyo, komesha ghasia za waovu na ufanye wenye haki waishi kwa amani.
愿恶人的恶断绝! 愿你坚立义人! 因为公义的 神察验人的心肠肺腑。
10 Ngao langu ni Mungu Aliye Juu Sana, awaokoaye wanyofu wa moyo.
神是我的盾牌; 他拯救心里正直的人。
11 Mungu ni mwamuzi mwenye haki, Mungu aghadhibikaye kila siku.
神是公义的审判者, 又是天天向恶人发怒的 神。
12 Kama hakutuhurumia, atanoa upanga wake, ataupinda na kuufunga uzi upinde wake.
若有人不回头,他的刀必磨快, 弓必上弦,预备妥当了。
13 Ameandaa silaha zake kali, ameweka tayari mishale yake ya moto.
他也预备了杀人的器械; 他所射的是火箭。
14 Yeye aliye na mimba ya uovu na achukuaye mimba ya ghasia huzaa uongo.
试看恶人因奸恶而劬劳, 所怀的是毒害,所生的是虚假。
15 Yeye achimbaye shimo na kulifukua hutumbukia katika shimo alilochimba mwenyewe.
他掘了坑,又挖深了, 竟掉在自己所挖的阱里。
16 Ghasia azianzishazo humrudia mwenyewe, ukatili wake humrudia kichwani.
他的毒害必临到他自己的头上; 他的强暴必落到他自己的脑袋上。
17 Nitamshukuru Bwana kwa ajili ya haki yake, na nitaliimbia sifa jina la Bwana Aliye Juu Sana.
我要照着耶和华的公义称谢他, 歌颂耶和华至高者的名。