< Zaburi 56 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Njiwa mkimya wa mbali.” Utenzi wa Daudi. Baada ya kukamatwa na Wafilisti huko Gathi. Ee Mungu unihurumie, maana watu wananifuatia vikali; mchana kutwa wanazidisha mashambulizi yao.
Bodi mi usmiljen, oh Bog, kajti človek me hoče požreti, borben je, dnevno me zatira.
2 Wasingiziaji wangu wananifuatia mchana kutwa, wengi wananishambulia kwa kiburi chao.
Moji sovražniki me hočejo vsak dan požreti, kajti mnogo jih je, ki se borijo zoper mene, oh ti Najvišji.
3 Wakati ninapoogopa, nitakutumaini wewe.
Kadar sem prestrašen, bom zaupal vate.
4 Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu, katika Mungu ninatumaini; sitaogopa. Mwanadamu apatikanaye na kufa, atanitenda nini?
V Bogu bom hvalil njegovo besedo, v Boga sem položil svoje trdno upanje; ne bom se bal, kaj mi more storiti meso.
5 Mchana kutwa wanayageuza maneno yangu, siku zote wanapanga shauri la kunidhuru.
Vsak dan pačijo moje besede. Vse njihove misli so zoper mene za zlo.
6 Wananifanyia hila, wanajificha, wanatazama hatua zangu, wakiwa na shauku ya kuutoa uhai wangu.
Zbirajo se skupaj, skrivajo se, gledajo moje korake, ko čakajo na mojo dušo.
7 Wasiepuke kwa vyovyote, Ee Mungu, katika hasira yako yaangushe mataifa.
Ali bodo pobegnili s krivičnostjo? V svoji jezi potri ljudstva, oh Bog.
8 Andika maombolezo yangu, orodhesha machozi yangu katika gombo lako: je, haya hayapo katika kumbukumbu zako?
Ti pripoveduješ o mojih tavanjih. Moje solze si polagaš v svoj meh. Mar niso v tvoji knjigi?
9 Ndipo adui zangu watarudi nyuma ninapoita msaada. Kwa hili nitajua kwamba Mungu yuko upande wangu.
Ko kličem k tebi, potem se bodo moji sovražniki obrnili proč. To vem, kajti Bog je zame.
10 Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu, katika Bwana, ambaye neno lake ninalisifu,
V Bogu bom hvalil njegovo besedo. V Gospodu bom hvalil njegovo besedo.
11 katika Mungu ninatumaini, sitaogopa. Mwanadamu anaweza kunitenda nini?
V Boga sem položil svoje trdno upanje; ne bom se bal, kaj mi lahko stori človek.
12 Ee Mungu, nina nadhiri kwako, nitakutolea wewe sadaka zangu za shukrani.
Tvoje zaobljube so nad menoj, oh Bog, povrnil ti bom hvalnice.
13 Kwa kuwa umeniokoa toka kwenye mauti na miguu yangu kwenye kujikwaa, ili niweze kuenenda mbele za Mungu katika nuru ya uzima.
Kajti mojo dušo si osvobodil pred smrtjo. Mar mojih stopal ne boš osvobodil pred padcem, da lahko hodim pred Bogom v svetlobi živih?

< Zaburi 56 >