< Zaburi 60 >
1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Shushani Eduthi.” Utenzi wa Daudi wa kufundisha. Wakati alipopigana na Waaramu kutoka Aramu-Naharaimu na Aramu-Soba, naye Yoabu akarudi nyuma na kuwaua Waedomu 12,000 katika Bonde la Chumvi. Ee Mungu, umetukataa na kutokea ghafula juu yetu, umekasirika: sasa turejeshe upya!
Oh Bog, zavrgel si nas, razkropil si nas, razžaljen si bil; oh, ponovno se obrni k nam.
2 Umetetemesha nchi na kuipasua; uiponye mavunjiko yake, kwa maana inatetemeka.
Storil si, da zemlja trepeta, zlomil si jo; zaceli njene vrzeli, kajti trese se.
3 Umewaonyesha watu wako nyakati za kukata tamaa; umetunywesha mvinyo unaotuyumbisha.
Svojemu ljudstvu si pokazal težke stvari. Storil si nam, da pijemo vino osuplosti.
4 Kwa wale wanaokucha wewe, umewainulia bendera, ili iweze kutwekwa dhidi ya upinde.
Tem, ki se te bojijo, si dal prapor, da bi bil ta lahko dvignjen zaradi resnice. (Sela)
5 Tuokoe na utusaidie kwa mkono wako wa kuume, ili wale uwapendao wapate kuokolewa.
Da bodo tvoji ljubljeni lahko osvobojeni, reši s svojo desnico in me usliši.
6 Mungu amenena kutoka patakatifu pake: “Nitaigawa Shekemu kwa ushindi na kulipima Bonde la Sukothi.
Bog je spregovoril v svoji svetosti: »Veselil se bom, razdelil bom Sihem in odmeril Sukótsko dolino.
7 Gileadi ni yangu na Manase ni yangu; Efraimu ni kofia yangu ya chuma, nayo Yuda ni fimbo yangu ya utawala.
Gileád je moj in Manáse je moj; tudi Efrájim je moč moje glave, Juda je moj postavodajalec,
8 Moabu ni sinia langu la kunawia, juu ya Edomu natupa kiatu changu; nashangilia kwa kushindwa kwa Ufilisti.”
Moáb je moj lonec za pranje, nad Edóm bom vrgel svoj čevelj; Filisteja zmaguj zaradi mene.«
9 Ni nani atakayenipeleka hadi mji wenye ngome? Ni nani atakayeniongoza hadi nifike Edomu?
Kdo me bo privedel v utrjeno mesto? Kdo me bo vodil v Edóm?
10 Ee Mungu, si ni wewe uliyetukataa sisi, na hutoki tena na majeshi yetu?
Mar ne ti, oh Bog, ki si nas zavrgel? In ti, oh Bog, ki nisi odšel z našimi vojskami?
11 Tuletee msaada dhidi ya adui, kwa maana msaada wa mwanadamu haufai kitu.
Daj nam pomoč iz stiske, kajti prazna je človeška pomoč.
12 Kwa msaada wa Mungu tutapata ushindi, naye atawaponda adui zetu.
Zaradi Boga bomo delali hrabro, kajti on je ta, ki bo pomendral naše sovražnike.