< Zaburi 4 >

1 Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Zaburi ya Daudi. Nijibu nikuitapo, Ee Mungu wangu mwenye haki! Nipumzishe katika shida zangu; nirehemu, usikie ombi langu.
Zborovođi. Uz žičana glazbala. Psalam. Davidov. Kad zazovem, usliši me, Bože, pravdo moja, ti što me u tjeskobi izbavÄi: smiluj mi se, usliši moju molitvu!
2 Enyi watu, mtabadilisha utukufu wangu kuwa aibu mpaka lini? Mtapenda udanganyifu na kufuata miungu ya uongo mpaka lini?
Sinovi čovječji, dokle će vam srca ostati tvrda? Zašto ispraznost ljubite, opsjenu slijedite?
3 Fahamuni hakika kwamba Bwana amewatenga wale wamchao kwa ajili yake; Bwana atanisikia nimwitapo.
Znajte: Jahve čudesno uzvisuje prijatelja svoga; Gospodin će me uslišiti kad ga zazovem.
4 Katika hasira yako, usitende dhambi. Mkiwa vitandani mwenu, mtulie kimya mkiichunguza mioyo yenu.
Promislite u srcima i ne griješite, dršćite na svojim ležajima i zanijemite.
5 Toeni dhabihu zilizo haki; mtegemeeni Bwana.
Prinesite žrtve pravedne, u Jahvu se uzdajte!
6 Wengi wanauliza, “Ni nani awezaye kutuonyesha jema lolote?” Ee Bwana, tuangazie nuru ya uso wako.
Mnogi govore: “Tko će nam pokazati sreću?” Obasjaj nas, Jahve, svjetlom svoga lica!
7 Wewe umejaza moyo wangu kwa furaha kubwa kuliko watu waliopata nafaka na divai kwa wingi.
Više si u srce moje ulio radosti nego kad obilno rode pšenica i vino.
8 Nitajilaza chini na kulala kwa amani, kwa kuwa wewe peke yako, Ee Bwana, waniwezesha kukaa kwa salama.
Čim legnem, odmah u miru i usnem, jer mi samo ti, o Jahve, daješ miran počinak.

< Zaburi 4 >