< Zaburi 3 >

1 Zaburi ya Daudi. Alipomkimbia mwanawe Absalomu. Ee Bwana, tazama adui zangu walivyo wengi! Ni wengi kiasi gani wanaoinuka dhidi yangu!
Psalam. Davidov. Kad je David bježao pred sinom Abšalomom. Jahve, koliko je tlačitelja mojih, koliki se podižu na me!
2 Wengi wanasema juu yangu, “Mungu hatamwokoa.”
Mnogi su što o meni zbore: “Nema mu spasenja u Bogu!”
3 Lakini wewe, Ee Bwana, ni ngao pande zote; umeniwekea utukufu na kuinua kichwa changu.
Ti si ipak štit moj, Jahve; slavo moja, ti mi glavu podižeš.
4 Ninamlilia Bwana kwa sauti kuu, naye ananijibu kutoka mlima wake mtakatifu.
Iza sveg glasa Jahvi zavapih, i on me usliša sa svete gore svoje.
5 Ninajilaza na kupata usingizi; naamka tena, kwa maana Bwana hunitegemeza.
Sad mogu leć' i usnuti, i onda ustat' jer me Jahve drži.
6 Sitaogopa makumi elfu ya adui, wanaojipanga dhidi yangu kila upande.
Ne bojim se tisuća ljudi što me opsjedaju dušmanski.
7 Ee Bwana, amka! Niokoe, Ee Mungu wangu! Wapige adui zangu wote kwenye taya, vunja meno ya waovu.
Ustani, o Jahve! Spasi me, o Bože moj! Ti udaraš po obrazu sve neprijatelje moje, opakima zube razbijaš.
8 Kwa maana wokovu watoka kwa Bwana. Baraka yako na iwe juu ya watu wako.
U Jahve je spasenje: na tvom narodu tvoj je blagoslov!

< Zaburi 3 >