< Zaburi 30 >
1 Utenzi wa kuweka wakfu hekalu. Zaburi ya Daudi. Nitakutukuza wewe, Ee Bwana, kwa kuwa umeniinua kutoka vilindi, na hukuacha adui zangu washangilie juu yangu.
A psalm [the] song of [the] dedication of the house of David. I will exalt you O Yahweh for you have drawn up me and not you have allowed to rejoice enemies my to me.
2 Ee Bwana, Mungu wangu, nilikuita unisaidie na wewe umeniponya.
O Yahweh God my I cried for help to you and you healed me.
3 Ee Bwana, umenitoa Kuzimu, umeniokoa nisishuke kwenye shimo la mauti. (Sheol )
O Yahweh you brought up from Sheol life my you preserved alive me (from going down my *Q(K)*) [the] pit. (Sheol )
4 Mwimbieni Bwana, enyi watakatifu wake; lisifuni jina lake takatifu.
Sing praises to Yahweh O faithful [people] his and give thanks to [the] remembrance of holiness his.
5 Kwa maana hasira yake ni ya muda mfupi, bali upendo wake hudumu siku zote. Inawezekana kilio kiwepo usiku kucha, lakini asubuhi kukawa na furaha.
For a moment - [is] in anger his life [is] in favor his in the evening it passes [the] night weeping and to the morning a shout of joy.
6 Nilipofanikiwa nilisema, “Sitatikiswa kamwe.”
And I I said in prosperity my not I will be shaken for ever.
7 Ee Bwana, uliponijalia, uliuimarisha mlima wangu, lakini ulipouficha uso wako nilifadhaika.
O Yahweh in favor your you made stand to mountain my strength you hid face your I was disturbed.
8 Kwako wewe, Ee Bwana, niliita, kwa Bwana niliomba rehema:
To you O Yahweh I called out and to [the] Lord I sought favor.
9 “Kuna faida gani katika kuangamia kwangu? Katika kushuka kwangu shimoni? Je, mavumbi yatakusifu? Je, yatatangaza uaminifu wako?
What? [is the] profit in blood my in going down my to [the] pit ¿ will it give thanks to you dust ¿ will it declare faithfulness your.
10 Ee Bwana, unisikie na kunihurumia, Ee Bwana, uwe msaada wangu.”
Hear O Yahweh and show favor to me O Yahweh be a helper of me.
11 Uligeuza maombolezo yangu kuwa kucheza, ulinivua nguo za gunia ukanivika shangwe,
You turned wailing my into dancing to me you loosened sackcloth my and you girded me joy.
12 ili moyo wangu uweze kukusifu na usikae kimya. Ee Bwana Mungu wangu, nitakushukuru milele.
So that - it may sing praises to you honor and not it may be silent O Yahweh God my for ever I will give thanks to you.