< Zaburi 26 >

1 Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, nithibitishe katika haki, maana nimeishi maisha yasiyo na lawama; nimemtumainia Bwana bila kusitasita.
By David. Judge me, Yahweh, for I have walked in my integrity. I have trusted also in Yahweh without wavering.
2 Ee Bwana, unijaribu, unipime, uuchunguze moyo wangu na mawazo yangu;
Examine me, Yahweh, and prove me. Try my heart and my mind.
3 kwa maana upendo wako uko mbele yangu daima, nami natembea siku zote katika kweli yako.
For your loving kindness is before my eyes. I have walked in your truth.
4 Siketi pamoja na watu wadanganyifu, wala siandamani na wanafiki,
I have not sat with deceitful men, neither will I go in with hypocrites.
5 ninachukia kusanyiko la watenda mabaya na ninakataa kuketi pamoja na waovu.
I hate the assembly of evildoers, and will not sit with the wicked.
6 Ninanawa mikono yangu kwa kuwa sina hatia, naikaribia madhabahu yako, Ee Bwana,
I will wash my hands in innocence, so I will go about your altar, Yahweh,
7 nikitangaza sifa yako kwa sauti kubwa, huku nikisimulia matendo yako ya ajabu.
that I may make the voice of thanksgiving to be heard and tell of all your wondrous deeds.
8 Ee Bwana, naipenda nyumba yako mahali unakoishi, mahali ambapo utukufu wako hukaa.
Yahweh, I love the habitation of your house, the place where your glory dwells.
9 Usiiondoe nafsi yangu pamoja na watenda dhambi, wala uhai wangu pamoja na wamwagao damu,
Don’t gather my soul with sinners, nor my life with bloodthirsty men
10 ambao mikononi mwao kuna mipango miovu, ambao mikono yao ya kuume imejaa rushwa.
in whose hands is wickedness; their right hand is full of bribes.
11 Bali mimi ninaishi maisha yasiyo na lawama; nikomboe na unihurumie.
But as for me, I will walk in my integrity. Redeem me, and be merciful to me.
12 Miguu yangu imesimama katika uwanja tambarare; katika kusanyiko kuu nitamsifu Bwana.
My foot stands in an even place. In the congregations I will bless Yahweh.

< Zaburi 26 >