< Zaburi 22 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa utenzi wa “Kulungu wa Alfajiri.” Zaburi ya Daudi. Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? Kwa nini uko mbali hivyo kuniokoa? Mbali hivyo na maneno ya kuugua kwangu?
For the Chief Musician; set to “The Doe of the Morning.” A Psalm by David. My God, my God, why have you forsaken me? Why are you so far from helping me, and from the words of my groaning?
2 Ee Mungu wangu, ninalia mchana, lakini hunijibu, hata usiku, sinyamazi.
My God, I cry in the daytime, but you don’t answer; in the night season, and am not silent.
3 Hata hivyo umesimikwa katika kiti cha enzi kama Uliye Mtakatifu; wewe ni sifa ya Israeli.
But you are holy, you who inhabit the praises of Israel.
4 Kwako wewe baba zetu waliweka tumaini lao, walikutumaini nawe ukawaokoa.
Our fathers trusted in you. They trusted, and you delivered them.
5 Walikulilia wewe na ukawaokoa, walikutegemea wewe nao hawakuaibika.
They cried to you, and were delivered. They trusted in you, and were not disappointed.
6 Mimi ni mnyoo wala si mwanadamu, wanaume wamenibeza, na watu wamenidharau.
But I am a worm, and no man; a reproach of men, and despised by the people.
7 Wote wanionao hunidhihaki, hunivurumishia matusi, wakitikisa vichwa vyao:
All those who see me mock me. They insult me with their lips. They shake their heads, saying,
8 Husema, “Anamtegemea Bwana, basi Bwana na amwokoe. Amkomboe basi, kwa maana anapendezwa naye.”
“He trusts in Yahweh. Let him deliver him. Let him rescue him, since he delights in him.”
9 Hata hivyo ulinitoa tumboni, ukanifanya nikutegemee, hata nilipokuwa ninanyonya matiti ya mama yangu.
But you brought me out of the womb. You made me trust while at my mother’s breasts.
10 Nimekabidhiwa kwako tangu kuzaliwa, toka tumboni mwa mama yangu umekuwa Mungu wangu.
I was thrown on you from my mother’s womb. You are my God since my mother bore me.
11 Usiwe mbali nami, kwa maana shida iko karibu na hakuna wa kunisaidia.
Don’t be far from me, for trouble is near. For there is no one to help.
12 Mafahali wengi wamenizunguka, mafahali wa Bashani wenye nguvu wamenizingira.
Many bulls have surrounded me. Strong bulls of Bashan have encircled me.
13 Simba wangurumao wanaorarua mawindo yao hupanua vinywa vyao dhidi yangu.
They open their mouths wide against me, lions tearing prey and roaring.
14 Nimemiminwa kama maji, mifupa yangu yote imetoka katika viungo vyake. Moyo wangu umegeuka kuwa nta, umeyeyuka ndani yangu.
I am poured out like water. All my bones are out of joint. My heart is like wax. It is melted within me.
15 Nguvu zangu zimekauka kama kigae, ulimi wangu umegandamana na kaakaa la kinywa changu, kwa sababu umenilaza katika mavumbi ya kifo.
My strength is dried up like a potsherd. My tongue sticks to the roof of my mouth. You have brought me into the dust of death.
16 Mbwa wamenizunguka, kundi la watu waovu limenizingira, wametoboa mikono yangu na miguu yangu.
For dogs have surrounded me. A company of evildoers have enclosed me. They have pierced my hands and feet.
17 Naweza kuhesabu mifupa yangu yote, watu wananikodolea macho na kunisimanga.
I can count all of my bones. They look and stare at me.
18 Wanagawana nguo zangu wao kwa wao, na vazi langu wanalipigia kura.
They divide my garments among them. They cast lots for my clothing.
19 Lakini wewe, Ee Bwana, usiwe mbali. Ee Nguvu yangu, uje haraka unisaidie.
But don’t be far off, Yahweh. You are my help. Hurry to help me!
20 Okoa maisha yangu na upanga, uhai wangu wa thamani kutoka nguvu za mbwa.
Deliver my soul from the sword, my precious life from the power of the dog.
21 Niokoe kutoka kinywani mwa simba, niokoe kutoka pembe za mafahali mwitu.
Save me from the lion’s mouth! Yes, you have rescued me from the horns of the wild oxen.
22 Nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu, katika kusanyiko nitakusifu wewe.
I will declare your name to my brothers. Among the assembly, I will praise you.
23 Ninyi ambao mnamcha Bwana, msifuni! Ninyi nyote wazao wote wa Yakobo, mheshimuni yeye! Mcheni yeye, ninyi wazao wote wa Israeli!
You who fear Yahweh, praise him! All you descendants of Jacob, glorify him! Stand in awe of him, all you descendants of Israel!
24 Kwa maana hakupuuza wala kudharau mateso ya aliyeonewa; hakumficha uso wake bali alisikiliza kilio chake ili amsaidie.
For he has not despised nor abhorred the affliction of the afflicted, neither has he hidden his face from him; but when he cried to him, he heard.
25 Kwako wewe hutoka kiini cha sifa zangu katika kusanyiko kubwa, nitatimiza nadhiri zangu mbele ya wale wakuchao wewe.
My praise of you comes in the great assembly. I will pay my vows before those who fear him.
26 Maskini watakula na kushiba, wale wamtafutao Bwana watamsifu: mioyo yenu na iishi milele!
The humble shall eat and be satisfied. They shall praise Yahweh who seek after him. Let your hearts live forever.
27 Miisho yote ya dunia itakumbuka na kumgeukia Bwana, nazo jamaa zote za mataifa watasujudu mbele zake,
All the ends of the earth shall remember and turn to Yahweh. All the relatives of the nations shall worship before you.
28 kwa maana ufalme ni wa Bwana naye hutawala juu ya mataifa.
For the kingdom is Yahweh’s. He is the ruler over the nations.
29 Matajiri wote wa dunia watasherehekea na kuabudu. Wote waendao mavumbini watapiga magoti mbele yake, wote ambao hawawezi kudumisha uhai wao.
All the rich ones of the earth shall eat and worship. All those who go down to the dust shall bow before him, even he who can’t keep his soul alive.
30 Wazao wa baadaye watamtumikia yeye; vizazi vijavyo vitajulishwa habari za Bwana.
Posterity shall serve him. Future generations shall be told about the Lord.
31 Watatangaza haki yake kwa watu ambao hawajazaliwa bado, kwa maana yeye ametenda hili.
They shall come and shall declare his righteousness to a people that shall be born, for he has done it.

< Zaburi 22 >