< Zaburi 24 >
1 Zaburi ya Daudi. Dunia ni mali ya Bwana, na vyote vilivyomo ndani yake, ulimwengu, na wote waishio ndani yake,
JAPWILIM en leowa jappa o audepa kan, jap o meakaroj me kaujon poa.
2 maana aliiwekea misingi yake baharini na kuifanya imara juu ya maji.
Pwe a kotin pajonedier ni kailan madau, o a kotin wiadar pon pil akan.
3 Nani awezaye kuupanda mlima wa Bwana? Ni nani awezaye kusimama patakatifu pake?
Ij me pan kodalan pon dol en leowa? O ij me pan kak uda ni mol en Ieowa jaraiui?
4 Ni yule mwenye mikono safi na moyo mweupe, yule ambaye hakuinulia sanamu nafsi yake au kuapa kwa kitu cha uongo.
me pa a kan jota japun o kin mauki padak japun, o me jota kin kaula likam.
5 Huyo atapokea baraka kutoka kwa Bwana, na hukumu ya haki kutoka kwa Mungu Mwokozi wake.
I me pan kamaula ren Ieowa, o a pan pun kila ren Kot a jaunkamaur.
6 Hiki ndicho kizazi cha wale wamtafutao, wale wautafutao uso wako, Ee Mungu wa Yakobo.
I kainok, me kin peiki on Kot, me kin rapaki jilan omui, Kot en Iakop.
7 Inueni vichwa vyenu, enyi malango, inukeni enyi milango ya kale, ili mfalme wa utukufu apate kuingia.
Komail ritinada wanim laud o lanada wanim nin jappa, pwe Nammarki linan en kotilon!
8 Ni nani huyu Mfalme wa utukufu? Ni Bwana aliye na nguvu na uweza, ni Bwana aliye hodari katika vita.
Ij Nanmarki linan men et? I Ieowa rojon o manaman, Ieowa me rajon nan mauin.
9 Inueni vichwa vyenu, enyi malango, viinueni juu enyi milango ya kale, ili Mfalme wa utukufu apate kuingia.
Komail ritinda wanim laud o lanada wanim ni jappa, pwe Nanmarki linan en kotilon!
10 Ni nani yeye, huyu Mfalme wa utukufu? Ni Bwana Mwenye Nguvu Zote; yeye ndiye Mfalme wa utukufu.
Ij Nanmarki linan men et? I Ieowa Jepaot; I Nanmarki linan.