< Zaburi 128 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Heri ni wale wote wamchao Bwana, waendao katika njia zake.
Feliz es el adorador del Señor, que camina en sus caminos.
2 Utakula matunda ya kazi yako; baraka na mafanikio vitakuwa vyako.
Tendrás el fruto del trabajo de tus manos; feliz serás, y todo te irá bien.
3 Mke wako atakuwa kama mzabibu uzaao ndani ya nyumba yako; wana wako watakuwa kama machipukizi ya mizeituni kuizunguka meza yako.
Tu mujer será como una vid fértil en las partes más recónditas de tu casa; tus hijos serán como plantas de olivo alrededor de tu mesa.
4 Hivyo ndivyo atakavyobarikiwa mtu amchaye Bwana.
¡Mira! esta es la bendición del adorador del Señor.
5 Bwana na akubariki kutoka Sayuni siku zote za maisha yako, na uone mafanikio ya Yerusalemu,
Que el Señor te envíe bendiciones desde Sión; que veas el bien de Jerusalén todos los días de tu vida.
6 nawe ujaliwe kuishi uone watoto wa watoto wako. Amani iwe juu ya Israeli.
Pueda ver los hijos de sus hijos. La paz sea con Israel.

< Zaburi 128 >