< Zaburi 128 >
1 Wimbo wa kwenda juu. Heri ni wale wote wamchao Bwana, waendao katika njia zake.
Cántico gradual. BIENAVENTURADO todo aquel que teme á Jehová, que anda en sus caminos.
2 Utakula matunda ya kazi yako; baraka na mafanikio vitakuwa vyako.
Cuando comieres el trabajo de tus manos, bienaventurado tú, y tendrás bien.
3 Mke wako atakuwa kama mzabibu uzaao ndani ya nyumba yako; wana wako watakuwa kama machipukizi ya mizeituni kuizunguka meza yako.
Tu mujer será como parra que lleva fruto á los lados de tu casa; tus hijos como plantas de olivas alrededor de tu mesa.
4 Hivyo ndivyo atakavyobarikiwa mtu amchaye Bwana.
He aquí que así será bendito el hombre que teme á Jehová.
5 Bwana na akubariki kutoka Sayuni siku zote za maisha yako, na uone mafanikio ya Yerusalemu,
Bendígate Jehová desde Sión, y veas el bien de Jerusalem todos los días de tu vida.
6 nawe ujaliwe kuishi uone watoto wa watoto wako. Amani iwe juu ya Israeli.
Y veas los hijos de tus hijos, y la paz sobre Israel.