< Zaburi 128 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Heri ni wale wote wamchao Bwana, waendao katika njia zake.
Un cántico para los peregrinos que van a Jerusalén. ¡Felices son los que alaban al Señor, todos los que siguen sus caminos!
2 Utakula matunda ya kazi yako; baraka na mafanikio vitakuwa vyako.
Ustedes comerán el producto de sus manos. Estarán felices y les irá bien.
3 Mke wako atakuwa kama mzabibu uzaao ndani ya nyumba yako; wana wako watakuwa kama machipukizi ya mizeituni kuizunguka meza yako.
Tu esposa será como una vid fructífera creciendo en tu casa. Tus hijos serán como retoños de olivo alrededor de tu mesa.
4 Hivyo ndivyo atakavyobarikiwa mtu amchaye Bwana.
Esta será la bendición del Señor para los que lo adoran.
5 Bwana na akubariki kutoka Sayuni siku zote za maisha yako, na uone mafanikio ya Yerusalemu,
Que el Señor te bendiga desde Sión; que veas a Jerusalén prosperar todos los días de tu vida.
6 nawe ujaliwe kuishi uone watoto wa watoto wako. Amani iwe juu ya Israeli.
Que veas a los hijos de tus hijos. ¡Y que Israel esté en paz!

< Zaburi 128 >