< Zaburi 128 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Heri ni wale wote wamchao Bwana, waendao katika njia zake.
The song of greces. Blessid ben alle men, that dreden the Lord; that gon in hise weies.
2 Utakula matunda ya kazi yako; baraka na mafanikio vitakuwa vyako.
For thou schalt ete the trauels of thin hondis; thou art blessid, and it schal be wel to thee.
3 Mke wako atakuwa kama mzabibu uzaao ndani ya nyumba yako; wana wako watakuwa kama machipukizi ya mizeituni kuizunguka meza yako.
Thi wijf as a plenteous vyne; in the sidis of thin hous. Thi sones as the newe sprenges of olyue trees; in the cumpas of thi bord.
4 Hivyo ndivyo atakavyobarikiwa mtu amchaye Bwana.
Lo! so a man schal be blessid; that dredith the Lord.
5 Bwana na akubariki kutoka Sayuni siku zote za maisha yako, na uone mafanikio ya Yerusalemu,
The Lord blesse thee fro Syon; and se thou the goodis of Jerusalem in alle the daies of thi lijf.
6 nawe ujaliwe kuishi uone watoto wa watoto wako. Amani iwe juu ya Israeli.
And se thou the sones of thi sones; se thou pees on Israel.

< Zaburi 128 >