< Zaburi 128 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Heri ni wale wote wamchao Bwana, waendao katika njia zake.
A Song of degrees. Blessed [is] every one that feareth the LORD; that walketh in his ways.
2 Utakula matunda ya kazi yako; baraka na mafanikio vitakuwa vyako.
For thou shalt eat the labor of thy hands: happy [shalt] thou be, and [it shall be] well with thee.
3 Mke wako atakuwa kama mzabibu uzaao ndani ya nyumba yako; wana wako watakuwa kama machipukizi ya mizeituni kuizunguka meza yako.
Thy wife [shall be] as a fruitful vine by the sides of thy house: thy children like olive plants around thy table.
4 Hivyo ndivyo atakavyobarikiwa mtu amchaye Bwana.
Behold, that thus shall the man be blessed that feareth the LORD.
5 Bwana na akubariki kutoka Sayuni siku zote za maisha yako, na uone mafanikio ya Yerusalemu,
The LORD shall bless thee out of Zion: and thou shalt see the good of Jerusalem all the days of thy life.
6 nawe ujaliwe kuishi uone watoto wa watoto wako. Amani iwe juu ya Israeli.
Yes, thou shalt see thy children's children, [and] peace upon Israel.

< Zaburi 128 >