< Zaburi 128 >
1 Wimbo wa kwenda juu. Heri ni wale wote wamchao Bwana, waendao katika njia zake.
A Song of Ascents. How happy is every one that revereth Yahweh, who walketh in his ways!
2 Utakula matunda ya kazi yako; baraka na mafanikio vitakuwa vyako.
The labour of thine own hands, surely thou shalt eat. How happy thou, and well for thine!
3 Mke wako atakuwa kama mzabibu uzaao ndani ya nyumba yako; wana wako watakuwa kama machipukizi ya mizeituni kuizunguka meza yako.
Thy wife, like a fruitful vine, within the recesses of thy house, —Thy children, like plantings of olive-trees, round about thy table.
4 Hivyo ndivyo atakavyobarikiwa mtu amchaye Bwana.
Lo! thus, shall be blessed the man who revereth Yahweh.
5 Bwana na akubariki kutoka Sayuni siku zote za maisha yako, na uone mafanikio ya Yerusalemu,
Yahweh will bless thee, out of Zion, —and behold thou the welfare of Jerusalem, all the days of thy life!
6 nawe ujaliwe kuishi uone watoto wa watoto wako. Amani iwe juu ya Israeli.
And behold thou thy children’s children, —Prosperity on Israel!