< Zaburi 128 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Heri ni wale wote wamchao Bwana, waendao katika njia zake.
Blessed is every one that fears the LORD; that walks in his ways.
2 Utakula matunda ya kazi yako; baraka na mafanikio vitakuwa vyako.
For you shall eat the labor of your hands: happy shall you be, and it shall be well with you.
3 Mke wako atakuwa kama mzabibu uzaao ndani ya nyumba yako; wana wako watakuwa kama machipukizi ya mizeituni kuizunguka meza yako.
Your wife shall be as a fruitful vine by the sides of your house: your children like olive plants round about your table.
4 Hivyo ndivyo atakavyobarikiwa mtu amchaye Bwana.
Behold, that thus shall the man be blessed that fears the LORD.
5 Bwana na akubariki kutoka Sayuni siku zote za maisha yako, na uone mafanikio ya Yerusalemu,
The LORD shall bless you out of Zion: and you shall see the good of Jerusalem all the days of your life.
6 nawe ujaliwe kuishi uone watoto wa watoto wako. Amani iwe juu ya Israeli.
Yes, you shall see your children’s children, and peace on Israel.

< Zaburi 128 >