< Zaburi 128 >
1 Wimbo wa kwenda juu. Heri ni wale wote wamchao Bwana, waendao katika njia zake.
A song of degrees. Blessed is euery one that feareth the Lord and walketh in his wayes.
2 Utakula matunda ya kazi yako; baraka na mafanikio vitakuwa vyako.
When thou eatest the labours of thine hands, thou shalt be blessed, and it shall be well with thee.
3 Mke wako atakuwa kama mzabibu uzaao ndani ya nyumba yako; wana wako watakuwa kama machipukizi ya mizeituni kuizunguka meza yako.
Thy wife shalbe as the fruitfull vine on the sides of thine house, and thy children like the oliue plantes round about thy table.
4 Hivyo ndivyo atakavyobarikiwa mtu amchaye Bwana.
Lo, surely thus shall the man be blessed, that feareth the Lord.
5 Bwana na akubariki kutoka Sayuni siku zote za maisha yako, na uone mafanikio ya Yerusalemu,
The Lord out of Zion shall blesse thee, and thou shalt see the wealth of Ierusalem all the dayes of thy life.
6 nawe ujaliwe kuishi uone watoto wa watoto wako. Amani iwe juu ya Israeli.
Yea, thou shalt see thy childrens children, and peace vpon Israel.