< Zaburi 128 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Heri ni wale wote wamchao Bwana, waendao katika njia zake.
A song for pilgrims going up to Jerusalem. Happy are all those who worship the Lord, everyone who follows his ways!
2 Utakula matunda ya kazi yako; baraka na mafanikio vitakuwa vyako.
You will eat what your own hands have produced. You will be happy and do well.
3 Mke wako atakuwa kama mzabibu uzaao ndani ya nyumba yako; wana wako watakuwa kama machipukizi ya mizeituni kuizunguka meza yako.
Your wife will be like a fruitful vine growing in your home. Your children will be like the shoots of an olive tree around your table.
4 Hivyo ndivyo atakavyobarikiwa mtu amchaye Bwana.
This will certainly be the Lord's blessing on those who worship him.
5 Bwana na akubariki kutoka Sayuni siku zote za maisha yako, na uone mafanikio ya Yerusalemu,
May the Lord go on blessing you from Zion; may you see Jerusalem prosper all the days of your life.
6 nawe ujaliwe kuishi uone watoto wa watoto wako. Amani iwe juu ya Israeli.
May you see your children's children. May Israel be at peace!

< Zaburi 128 >