< Zaburi 128 >
1 Wimbo wa kwenda juu. Heri ni wale wote wamchao Bwana, waendao katika njia zake.
A Song of the going up. Happy is the worshipper of the Lord, who is walking in his ways.
2 Utakula matunda ya kazi yako; baraka na mafanikio vitakuwa vyako.
You will have the fruit of the work of your hands: happy will you be, and all will be well for you.
3 Mke wako atakuwa kama mzabibu uzaao ndani ya nyumba yako; wana wako watakuwa kama machipukizi ya mizeituni kuizunguka meza yako.
Your wife will be like a fertile vine in the inmost parts of your house: your children will be like olive plants round your table.
4 Hivyo ndivyo atakavyobarikiwa mtu amchaye Bwana.
See! this is the blessing of the worshipper of the Lord.
5 Bwana na akubariki kutoka Sayuni siku zote za maisha yako, na uone mafanikio ya Yerusalemu,
May the Lord send you blessing out of Zion: may you see the good of Jerusalem all the days of your life.
6 nawe ujaliwe kuishi uone watoto wa watoto wako. Amani iwe juu ya Israeli.
May you see your children's children. Peace be on Israel.