< Zaburi 128 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Heri ni wale wote wamchao Bwana, waendao katika njia zake.
Sang til Festrejserne. Salig enhver, som frygter HERREN og gaar paa hans Veje!
2 Utakula matunda ya kazi yako; baraka na mafanikio vitakuwa vyako.
Dit Arbejdes Frugt skal du nyde, salig er du, det gaar dig vel!
3 Mke wako atakuwa kama mzabibu uzaao ndani ya nyumba yako; wana wako watakuwa kama machipukizi ya mizeituni kuizunguka meza yako.
Som en frugtbar Vinranke er din Hustru inde i dit Hus, som Oliekviste er dine Sønner rundt om dit Bord.
4 Hivyo ndivyo atakavyobarikiwa mtu amchaye Bwana.
Se, saa velsignes den Mand, der frygter HERREN.
5 Bwana na akubariki kutoka Sayuni siku zote za maisha yako, na uone mafanikio ya Yerusalemu,
HERREN velsigne dig fra Zion, at du maa se Jerusalems Lykke alle dit Livs Dage
6 nawe ujaliwe kuishi uone watoto wa watoto wako. Amani iwe juu ya Israeli.
og se dine Sønners Sønner! Fred over Israel!

< Zaburi 128 >