< Zaburi 128 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Heri ni wale wote wamchao Bwana, waendao katika njia zake.
上行之詩。 凡敬畏耶和華、 遵行他道的人便為有福!
2 Utakula matunda ya kazi yako; baraka na mafanikio vitakuwa vyako.
你要吃勞碌得來的; 你要享福,事情順利。
3 Mke wako atakuwa kama mzabibu uzaao ndani ya nyumba yako; wana wako watakuwa kama machipukizi ya mizeituni kuizunguka meza yako.
你妻子在你的內室,好像多結果子的葡萄樹; 你兒女圍繞你的桌子,好像橄欖栽子。
4 Hivyo ndivyo atakavyobarikiwa mtu amchaye Bwana.
看哪,敬畏耶和華的人必要這樣蒙福!
5 Bwana na akubariki kutoka Sayuni siku zote za maisha yako, na uone mafanikio ya Yerusalemu,
願耶和華從錫安賜福給你! 願你一生一世看見耶路撒冷的好處!
6 nawe ujaliwe kuishi uone watoto wa watoto wako. Amani iwe juu ya Israeli.
願你看見你兒女的兒女! 願平安歸於以色列!

< Zaburi 128 >