< Zaburi 124 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Wa Daudi. Kama Bwana asingalikuwa upande wetu; Israeli na aseme sasa:
שיר המעלות לדוד לולי יהוה שהיה לנו-- יאמר-נא ישראל
2 kama Bwana asingalikuwa upande wetu, wakati watu walipotushambulia,
לולי יהוה שהיה לנו-- בקום עלינו אדם
3 wakati hasira yao ilipowaka dhidi yetu, wangalitumeza tungali hai,
אזי חיים בלעונו-- בחרות אפם בנו
4 mafuriko yangalitugharikisha, maji mengi yangalitufunika,
אזי המים שטפונו-- נחלה עבר על-נפשנו
5 maji yaendayo kasi yangalituchukua.
אזי עבר על-נפשנו-- המים הזידונים
6 Bwana asifiwe, yeye ambaye hakuruhusu turaruliwe kwa meno yao.
ברוך יהוה-- שלא נתננו טרף לשניהם
7 Tumeponyoka kama ndege kutoka mtego wa mwindaji; mtego umevunjika, nasi tukaokoka.
נפשנו-- כצפור נמלטה מפח יוקשים הפח נשבר ואנחנו נמלטנו
8 Msaada wetu ni katika jina la Bwana, Muumba wa mbingu na dunia.
עזרנו בשם יהוה-- עשה שמים וארץ

< Zaburi 124 >