< Zaburi 124 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Wa Daudi. Kama Bwana asingalikuwa upande wetu; Israeli na aseme sasa:
Cantique des montées. De David. Si Yahweh n’eût été pour nous, — qu’Israël le proclame, —
2 kama Bwana asingalikuwa upande wetu, wakati watu walipotushambulia,
si Yahweh n’eût été pour nous, quand les hommes se sont élevés contre nous!…
3 wakati hasira yao ilipowaka dhidi yetu, wangalitumeza tungali hai,
Ils nous auraient dévorés tout vivants, quand leur colère s’est allumée contre nous;
4 mafuriko yangalitugharikisha, maji mengi yangalitufunika,
les eaux nous auraient engloutis, le torrent eût passé sur notre âme;
5 maji yaendayo kasi yangalituchukua.
sur notre âme auraient passé les eaux impétueuses.
6 Bwana asifiwe, yeye ambaye hakuruhusu turaruliwe kwa meno yao.
Béni soit Yahweh, qui ne nous a pas livrés à leurs dents!
7 Tumeponyoka kama ndege kutoka mtego wa mwindaji; mtego umevunjika, nasi tukaokoka.
Notre âme, comme le passereau, s’est échappée du filet de l’oiseleur; le filet s’est rompu, et nous avons été délivrés.
8 Msaada wetu ni katika jina la Bwana, Muumba wa mbingu na dunia.
Notre secours est dans le nom de Yahweh, qui a fait les cieux et la terre.

< Zaburi 124 >